Majigambo yake yameisha. Amepigwa kipigo cha mbwa koko! Amepigwa na Bwana Mkubwa!
Loo, aibu yake! Alivyoona amefaulu kuwaingiza mtegoni ndugu zetu, kwa hila zake, alifikiri atadumu kuwa mwerevu. Sasa ameshushwa chini kabisa. Kila mtu anamzomea, hata watoto wadogo wanambeza!
Alijiinua juu kwa...