JamiiCheck imefuatilia hotuba iliyotolewa na Stephen Wasira akiwa kwenye mkutano wa kampeni za uchaguzi wa serikali za mitaa mkoani Mwanza tarehe 26-11-2024 ambapo mbali na mambo mengine alisema kuwa Rais Samia ameongoza kwa kipindi cha miaka minne, na pia serikali yake imejenga madarasa 986