Twajaa utimamu wa uwazimu, bila dhima twamhukumu imamu
Huzunini twajifanyia karamu, Ramadhani twabugia kharamu
Wenye wehu tumewapa hatamu, dhiki yetu itadumu dawamu
Maumivu yatujia kwa jamu, watoto wetu watatulaumu
Isikize yangu nudhumu, niambapo kwa yangu taalimu
Niseme hilaze bin-Adamu...