20% kapotelea wapi?

Sosinsa Unswe

Member
Joined
Oct 30, 2016
Posts
91
Reaction score
76
Wana JF nawasabahi,
Natumai sikukuu ya Maulid imeenda vyema na wachache ambao wanauguliwa na ndugu jamaa na marafiki Mungu awape uponyaji.

Nimejitokeza hapa ili kuwauliza wana JF kama kuna mtu ana taarifa sahihi za alipo msanii 20%,yuko wapi,kaacha music?kama jibu ni ndio anafanya shughuli gani huko aliko?na kama anaendelea na Music yuko kwa producer gani?Man Walter a.k.a man watet/man maji?

Kifupi hadi nafikia kuleta uzi huu mbele yenu sioni msanii mwenye mashairi ya mafunzo kama 20%.Inaniwia vigumu kuwasikiliza wasanii wengine maana maudhui yao ni mapenzi tu asubuhi mpaka jioni.

Japo Darasa kanishika kwa kipindi hiki.
Kwa anayefahamu juu ya 20% aliko na maisha yake ya sasa karibu utiririke
 
Jaribu kum mpigia afande sele kijiwe chap cha bangi kimoja
 
Zamu yake ya kumtafuta bdo now tunamtafuta Ben kwanza
 
Hivi karibuni nilisikia karudiana na Man Walter wakatoa wimbo ila siusikii naona umebuma
 
Mbona katoa nyimbo hivi karibuni unaitwa sitoi. Una mjumbe mzuri tu kwa wale wakataa mimba man walter ndani.
 

Kapotelea kimoja katika Mashamba ya Bangi Mkuu. Sijui una swali jingine tena?
 

Huyu aliwahi kuimba bange bange bange ilisababisha mi nisoteee...naona anasota huyo sasa
 
bange bange tu! tuwatafute watu wengine huyuu! mambo yakiwa siyo atakuja tu!
 
mkuu huyu kijana anaishi kijiji cha kimanzichana KM 50 kusini mwa jiji la makelele dsm pia ametoa nyimbo kazaa semahazija bamba kivile
 
Alitudharau, tulimpenda tukamwinua tukampigia kura kwa wingi tukampa tuzo tano akatuletea udwanzi wa kutupotezea na kutohudhuria sherehe kutushukuru,NA SISI TUMEMPOTEZEA.
 
Watu humu mnaoongea tu...ila mimi niseme bila ushabiki, wasanii km 20% ndio wanapaswa kubeba tuzo ktk jamiii, sio hawa wanaoimba utumbo utumbo maneno yasio na msingi album nzima wanaimba mapenz au majigambo na matusi!!!!...tatzo kubwa ni media, na usasa ambao una sapoti upumbavu na ujinga ktk jamii..hivyo wanamziki wote wenye misingi halisi na vipaji vya kutoa burudani +elimu ya maana ktk jamii wanapigwa chini....mifereji ya kipato na umaarufu wanatengenezewa madunya, wenye nyimbo dizain ya bubble gum , Dunia inazid kugeuzwa chaka bovu la watu wasiojielewa, .

Ndio maana watu wazima km mimi na 20% tunaamua ku stay back..na kuangalia maana hatuwez ingia kwenye ushenz ili tusaminike..bora tuonekane wanywa gongo, maskini etc!!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…