2025 CCM watakuja na manifesto gani tutakayoiamini kama manifesto za miaka 60 hazijatekelezwa?

2025 CCM watakuja na manifesto gani tutakayoiamini kama manifesto za miaka 60 hazijatekelezwa?

Sky Eclat

JF-Expert Member
Joined
Oct 17, 2012
Posts
57,761
Reaction score
216,011
Uchumi wa wananchi mmoja mmoja ni mgumu sana, vijana wanashinda vijiweni kwasababu hawana kazi. Wengi hujiingiza katika ulevi , kucheza kamari na kuvuta bange kutokana na kukosa kitu cha kufanya.

Serikali imeweka tozo kila mahali, hawa hawa wasio na kipato maalum bado wanakamuliwa ili kuiongezea serikali pato. Hawa wachumi wetu wanashindwa kufanya tafiti na kuja na jawabu la kuongeza kipato cha mtu mmoja mmoja. Hizi ahadi zipo hata kwenye ilani ya 2020 lakini hazija tekelezwa. Watatuambia nini kipya tuwaamini?

Mpaka sasa hivi sera ya kumtua mama ndoo kichwani bado ni ndoto. Maji salama kupatikana ni changamoto sehemu nyingi za nchi hasa vijijini na hata baadhi ya miji. Kukosekana kwa maji kunazalisha magonjwa wakati uhakika wa matibabu pia haupo.

Wananchi wanaomba huduma za maji, shule, zahanati na barabara, ikitokea mradi mmoja umefanikiwa mfano kujengewa shule, wanyonge watalazimishwa kumshukuru Rais kwa kuwaletea shule kama vile unavyomshukuru Mungu kwa kukupa uhai.

Uchumi wa mtu mmoja mmoja ukiimarika, serikali itajipunguzia mzigo kwani wananchi wakipata viongozi wazuri wanaweza kutatua changamoto zao wenyewe.

Enzi zao la kahawa limeshamiri kule Moshi, wakulima waliacha 10% ya mauzo ya kila gunia katika mfuko wa maendeleo wa kijiji. Baada ya mauzo wanakaa kikao na kijadiliana tatizo lao kubwa linalowakabili kijijini. Kwa njia hii waliweza kujenga shule, kuvuta maji salama na hata kuweka lami barabara zao.

Kule Lindi na Mtwara zao la korosho lilipo shamiri na wakulima kuanza kuhesabu milioni na ushee za mauzo, wengi walianza kuboresha makazi yao. Nyumba za udongo zilibadilishwa kuwa za saruji na kuezekwa kwa mabati.

2025 CCM mtatuambia nini ambacho hatujawahi kukisikia?
 
CCM ilipofikia bila kuondoka kizazi hiki hakitaona mabadiliko yoyote. Kwavile wao wenyewe wanakiri wameshindwa hata kujenga nidhamu tu kwa watumishi wa umma na kuishia kujenga nidhamu ya woga hawastahili kuendelea kutupa watu wa kutuongoza.

Tunahitaji uelekeo mpya bila CCM bila wanasiasa wenye makandokando ya CCM na wanamtandao wao walio upinzani.
 
CCM ilipofikia bila kuondoka kizazi hiki hakitaona mabadiliko yoyote. Kwavile wao wenyewe wanakiri wameshindwa hata kujenga nidhamu tu kwa watumishi wa umma na kuishia kujenga nidhamu ya woga hawastahili kuendelea kutupa watu wa kutuongoza.

Tunahitaji uelekeo mpya bila CCM bila wanasiasa wenye makandokando ya CCM na wanamtandao wao walio upinzani.
Kama wameshindwa kujenga nidhamu katika ofisi za serikali, tunawaamini vipi na uwajibikaji wa pesa za umma. Hakuna uwazi wa matumizi bali tunaongezewa tozo kila uchao.
 
Uchumi wa wananchi mmoja mmoja ni mgumu sana, vijana wanashinda vijiweni kwasababu hawana kazi. Wengi hujiingiza katika ulevi , kucheza kamari na kuvuta bange kutokana na kukosa kitu cha kufanya.

Serikali imeweka tozo kila mahali, hawa hawa wasio na kipato maalum bado wanakamuliwa ili kuiongezea serikali pato. Hawa wachumi wetu wanashindwa kufanya tafiti na kuja na jawabu la kuongeza kipato cha mtu mmoja mmoja. Hizi ahadi zipo hata kwenye ilani ya 2020 lakini hazija tekelezwa. Watatuambia nini kipya tuwaamini?

Mpaka sasa hivi sera ya kumtua mama ndoo kichwani bado ni ndoto. Maji salama kupatikana ni changamoto sehemu nyingi za nchi hasa vijijini na hata baadhi ya miji. Kukosekana kwa maji kunazalisha magonjwa wakati uhakika wa matibabu pia haupo.

Wananchi wanaomba huduma za maji, shule, zahanati na barabara, ikitokea mradi mmoja umefanikiwa mfano kujengewa shule, wanyonge watalazimishwa kumshukuru Rais kwa kuwaletea shule kama vile unavyomshukuru Mungu kwa kukupa uhai.

Uchumi wa mtu mmoja mmoja ukiimarika, serikali itajipunguzia mzigo kwani wananchi wakipata viongozi wazuri wanaweza kutatua changamoto zao wenyewe.

Enzi zao la kahawa limeshamiri kule Moshi, wakulima waliacha 10% ya mauzo ya kila gunia katika mfuko wa maendeleo wa kijiji. Baada ya mauzo wanakaa kikao na kijadiliana tatizo lao kubwa linalowakabili kijijini. Kwa njia hii waliweza kujenga shule, kuvuta maji salama na hata kuweka lami barabara zao.

Kule Lindi na Mtwara zao la korosho lilipo shamiri na wakulima kuanza kuhesabu milioni na ushee za mauzo, wengi walianza kuboresha makazi yao. Nyumba za udongo zilibadilishwa kuwa za saruji na kuezekwa kwa mabati.

2025 CCM mtatuambia nini ambacho hatujawahi kukisikia?
1.Tutatawaambia Kuwa awamu ya tano watumishi walifanya kazi kwa uoga.
2. Tumeweza kurekebisha mitambo ya umeme kwani karibia nchi nzima nyaya zilikuwa uchi kwa sababu ndani ya miaka 5 hakuna marekebisho yoyote yaliyofanyika hilo uongozi wa awamu ya sita ( Kama inavyoelezwa na wapambe) imefanya marekebisho hayo.

3. Tumefanikisha kuleta tozo kila mahali ili Watanzania wenye kazi na wasio na kazi wachangie maendeleo ya nchi. Hata kipindi kigumu cha kupanda kwa bei ya mafuta sisi CCM tumethubutu kurudisha ile tozo ya sh100 ili Watanzania waache kula chakula cha mafuta .

4. Tumefanikisha kukiimarisha chama kwani tuliwaondoa viongozi wote ambao walioshiriki kuwaumiza wananchi katika awamu ya tano na sasa CCM ina wenyewe imerudi na tutashinda kwa gori la mkono.

5 Katika ilani ijayo tutawaeleza pia Watanzania jinsi wanavyokula asali, Hata wewe mwenyewe unakula asali. Asali ya maji huli????

6. Tutaeleza pia jinsi demokrasia ilivyoimarika hadi kufunguliwa kwa kesi za michongo kwa viongozi wa kisiasa kisha tukawasamehe na kuwaambia wananchi wakawahoji wafuasi wa chadema sababu za kiongozi wao kufungwa.

7. Kwenye ilani tutaeleza pia jinsi Serikali ya CCM ilivyochochea Kupanda kwa bei ya bidhaa kama mafuta huku Zanzibar ikipiga marufuku na kutoa onyo kwa mfanyabishara yeyote atakayepandisha bidhaa atakiona cha mtema kuni.

8. Tutawaambia pia jinsi demokrasia na separation of power ilivyokuwa Katika uongozi kiasi kwamba hadi speaker wa bunge alifurushwa baada ya kuipinga serikali na hadi sasa hajulikan alipo huku shule ya uongozi ya polepole tukiifyekelea mbali.

9 Kwenye ilani pia tutaeleza jinsi machinga walivyoisoma namba kwa kuvunjiwa mabanda yao yasiyoeleweka kisha tukawapanga kwenye maeneo maalumu sasa hiyo mtunyime kula ndugu wananchi????? Mmesahau masoko yenu yalivyoungua??? Mtatupa kura au mtatunyima kura?????

10. Pia tutaeleza namna gani uchumi ulivyopanda kwa kukopa madeni mengi rafiki toka kwa mabeberu na sasa nchi inasonga mbele. Miradi imekamilika, Tumekamikisha mradi wa umeme kwani sasa umeme haukatiki katiki kama zamani, maji yanapatikana, hata zile cranes tumenunua.

KILA MBUZI AMEFANIKIWA KULA KULINGANA NA UREFU WA KAMBA YAKE. AU NASEMA UONGO NDUGU ZANGU [emoji23]


HII NDIO ILANI YA CCM IJAYO.
 
CCM hawawezi kila awamu kujifanya ni CCM mpya! CCM ni ile ile, wakae pembeni wajipange upya tuweke chama kingine 2025.

Chadema ikipata intellectuals wa maana na kujipanga upya, kuacha siasa za matusi na kubeba ajenda za maana hii ni fursa kubwa kuliko hata ile ya Dr Slaa na EL.

FM bora ukafanye retret na wazee wenye hekima na vijana wachache aina ya Mnyika ili mkusanye silaha upya na kujipanga upya! CCM wanasamehana ili kuondoa vita ya ndani isiyo na msingi. Tafakarini mipasuko yenu imesababishwa na nini? Tena very fair bila chuki. Irudi Chadema ya nguvu ya umma.

Njia ni nyeupe kwa Chadema ila mabadiliko ya msingi, kusamehana ( mengi yalitokea na kila upande una makosa). Hii ndio njia salama kwa muda huu mfupi kuelekea 2025
 
Uchumi wa wananchi mmoja mmoja ni mgumu sana, vijana wanashinda vijiweni kwasababu hawana kazi. Wengi hujiingiza katika ulevi , kucheza kamari na kuvuta bange kutokana na kukosa kitu cha kufanya.

2025 CCM mtatuambia nini ambacho hatujawahi kukisikia?
2025, hatutawaambia chochote kwa sababu mmezoea manifesto za kuambiwa!. 2025, hatuji tena na manifesto za maneno na ahadi, 2025, hatuwaambiaa bali tunawaonyesha kilichofanyika.

Jee uliona matokeo ya
kwenye uchaguzi mkuu wa 2020?.

Sasa 2025 ndio itakuwa balaa!.
Ushindi ni 99.9%.
P
 
Back
Top Bottom