2025 jimbo la Tandahimba litakuwa la kwanza kubebwa na wapinzani

2025 jimbo la Tandahimba litakuwa la kwanza kubebwa na wapinzani

Shimoyo

Member
Joined
Feb 10, 2021
Posts
11
Reaction score
7
Salaam.

Kila anayefuatilia masuala yahusuyo siasa atakubaliana nami kwamba katika mkoa wa Mtwara, jimbo la Tandahimba ndilo linaongoza kwa siasa za upinzani.

Katika uchaguzi mkuu uliopita CCM walilikomboa jimbo hili toka mikononi mwa CUF ambapo mbunge aliyeshinda uchaguzi mkuu wa 2015 alitokana na chama hiki wakati katika ngazi ya halmashauri, chama hiki kilijizolea viti 27 kati ya 32 vya udiwani.

Licha ya CCM kulirejesha jimbo hili mikononi mwake katika uchaguzi mkuu uliopita kwa kujipatia mbunge na madiwani 31 kati ya 32, bado upinzani una wafuasi wengi sana katika jimbo hili. Katika siku za hivi karibuni hasa kuanzia kipindi yalipofanyika mabadiliko ya mkuu wa wilaya ambapo Rais Samia alimhamisha Bw. Sebastian Waryuba na nafasi yake kuchukuliwa na Col. Patrick Sawala aliyetokea wilaya ya Rufiji wananchi wanapitia wakati mgumu sana.

Baada tu ya ujio wa mkuu huyu mpya wa wilaya chuki ya wananchi dhidi ya Chama cha Mapinduzi na serikali yake imeongezeka mara dufu na hivyo kuupa upinzani turufu ya kushinda uchaguzi 2025. Licha ya kadhia nyingi zinazowapata wananchi, lakini hii ya askari wa jeshi la Polisi kuzunguka vijijini na kwenye mitaa ya mji wa Tandahimba wakikamata pikipiki hata zilizopo kwenye matengenezo inazidi kuichonganisha serikali na wananchi wake huku ikizidisha chuki ya wananchi dhidi ya chama tawala.

Askari wa jeshi la Polisi wa hapa wilayani hawana kazi nyingine wanayofanya zaidi ya hii ya kukamata mapikipiki mitaani na vijijini. Kwa hapa Tandahimba, kila askari yuko kwenye kitengo cha Usalama Barabani. Ukamataji huu hufanyika siku saba za wiki kuanzia saa 12 asubuhi hadi saa 12 jioni. Huwa wanajaa kwenye magari mawili madogo ( Landcruiser) na huambatana na lori ya polisi ambayo hutumika kuzibeba pikipiki na kuzifikisha kituoni.

Ikumbukwe kwamba katika wilaya ya Tandahimba, 85% ya wakazi wenye umri unaoanzia miaka 25 wanamiliki pikipiki. Hapa Tandahimba pikipiki ni nyingi kama ilivyo kwa manispaa ya Shinyanga inayoongoza kwa kuwa na baiskeli nyingi. Kutokana na wingi huu wa pikipiki, viongozi wa jeshi la polisi wakishirikiana na mkuu wa wilaya wameamua kutumia hii kamatakamata kuwa mtaji wa kujipatia fedha kwa manufaa binafsi. Kuna OCD anaitwa Tesha. Huyu ndiye "master plan" wa mchongo huu. Huyu ndiye huruhusu wale askari kuendesha hii operation isiyo na kikomo. Na ndiye anayemfikishia DC fungu lake.

Kwanini wananchi wanalalamikia utaratibu huu unaokiuka haki? Ni kutokana na sababu zifuatazo:

i. Ukamataji huu haufanyiki barabarani badala yake askari huzunguka mitaani na vijijini na hukamata pikipiki hata zilizopo kwa mafundi. Pia huwa wanajificha vichochoroni hasa kwenye barabara za kuelekea maeneo ya vijijini.

ii. Asilimia kubwa ya wamiliki wa pikipiki hizo hulipishwa faini pasipo kupatiwa risiti za EFD badala yake huwapatia risiti za kuandika kwa mkono (hapa serikali inapoteza mapato yake).

iii. Kuna wengine hulipishwa faini ya Tsh. 30,000 kwa kila kosa na wanapohoji juu ya viwango hivyo vilivyofutwa na serikali kupitia bunge letu tukufu, hujitetea kwamba hawajaletewa waraka unaowaelekeza kutoza viwango vya sasa (Tsh. 10,000 kwa kila kosa).

iv. Ukamataji huu huendana na vipigo kwa waendesha pikipiki hao hasa kwa vijana.

v. Utendaji kazi wao hauzingatii idara mbalimbali zilizowekwa kisheria kwenye jeshi hilo kama vile Idara ya Usalama Barabarani, Idara ya Uchunguzi wa Makosa ya Jinai n.k. Askari wote hufanya kazi moja ya kukamata pikipiki mitaani.

vi. Kadhia hii ipo hapa Tandahimba pekee tofauti na ilivyo kwenye halmashauri au hata miji jirani kama Nanyamba, Newala, Masasi na hata Mtwara Manispaa.

vi. Biashara zinadorora hapa mjini kwa kuwa wateja walio wengi toka vijijini wanasita kuja mjini kwa kuhofia kukamatwa. Badala yake wanasafiri kwenda miji jirani kama Newala ambako hufanya manunuzi ya mahitaji yao bila bugudha ya askari Polisi.

vii. Makosa yaliyo mengi yanatozwa faini ni ya kubambika kwani wakishakutajia hayo makosa unatakiwa kulipa faini pasi kuhoji.

Mwisho kabisa nikuombe Rais Samia, mchunguze mkuu huyu wa wilaya na ikibainika kwamba ni kweli anashirikiana na askari hawa wasio waaminifu basi tengua uteuzi wake kwani anakuhujumu wewe binafsi, serikali yako pamoja na Chama cha Mapinduzi.

Ikikupendeza mwagize IGP Simon Sirro amshushe cheo huyu Kamanda wa Polisi wa Wilaya aitwaye Tesha. Huyu ni mla rushwa na hana maadili ya kiaskari.

Kama Mh. Rais hutayazingatia haya basi jiandae kulipoteza jimbo hili kwenye uchaguzi mkuu ujao utakaofanyika 2025.
 
Kiukweli askari wa Tandahimba ni wasumbufu sana kwa waendesha pikipiki. Nilienda likizo mwezi Agost mwaka huu. Siku moja wakati natoka kijijini naelekea Tandahimba mjini nikawakuta polisi wamesimamisha gari mikoroshoni halafu ghafla wakatokezea barabarani wakanizuia. Dah, ilikuwa mbinde yaani. Walinieleza kwamba nina makosa 9 hivyo natakiwa kulipa faini shilingi 90,000. Ililazimika tufike kituoni kisha nikamtaarifu ndugu yangu mmoja hivi ni mtumishi wa halmashauri. Alipofika tukalazimika kulipa faini ya shilingi 20,000 tu kwani pikipiki haikuwa na bima halafu haikuwa na kioo cha upande mmoja. Hivyo nakubaliana nawe kwamba hawa askari wa Tandahimba huwabambikia sana raia kesi au makosa hasa kwa waendesha pikipiki.
 
Kiukweli askari wa Tandahimba ni wasumbufu sana kwa waendesha pikipiki. Nilienda likizo mwezi Agost mwaka huu. Siku moja wakati natoka kijijini naelekea Tandahimba mjini nikawakuta polisi wamesimamisha gari mikoroshoni halafu ghafla wakatokezea barabarani wakanizuia. Dah, ilikuwa mbinde yaani. Walinieleza kwamba nina makosa 9 hivyo natakiwa kulipa faini shilingi 90,000. Ililazimika tufike kituoni kisha nikamtaarifu ndugu yangu mmoja hivi ni mtumishi wa halmashauri. Alipofika tukalazimika kulipa faini ya shilingi 20,000 tu kwani pikipiki haikuwa na bima halafu haikuwa na kioo cha upande mmoja. Hivyo nakubaliana nawe kwamba hawa askari wa Tandahimba huwabambikia sana raia kesi au makosa hasa kwa waendesha pikipiki.
Ni nchi nzima mkuu polisi wanasumbua sn kupita kiasi kumbuka 60% ni ndugu wa wakubwa
 
Mi mtu akiongelea uchaguzi kwenye hii nchi isiyo na Tume Huru sijui huwa namuonaje!!
 
Ni nchi nzima mkuu polisi wanasumbua sn kupita kiasi kumbuka 60% ni ndugu wa wakubwa
Hawa polisi wa Tandahimba ni zaidi ya waporaji mkuu. Yaani wanazunguka hata majumbani na madukani kupora mapikipiki kisha huyapeleka kituoni ambako ukienda kufuatilia unapigwa faini kubwa ambayo itakuduwaza na hupewi hata EFD receipt.
 
Hawa polisi wa Tandahimba ni zaidi ya waporaji mkuu. Yaani wanazunguka hata majumbani na madukani kupora mapikipiki kisha huyapeleka kituoni ambako ukienda kufuatilia unapigwa faini kubwa ambayo itakuduwaza na hupewi hata EFD receipt.
Kuna RCP mmoja nilikaa naye last week kwenye story tu za kawaida nikamuuliza kwanini traffic wanachukua pesa waziwazi na nyie mpo? alijibu 60% ni ndugu wa wakubwa hivyo huwezi kumfanya chochote utaishia kumtisha tisha kidogo basi
 
Sio kwa Tandahimba ninayoifahamu mimi. Hapa CCM wana mlima watavuja jasho sana 2025.
Mkuu hili jimbo lina watu makini sana, ila kinachoshangaza inapofika nyakati za uchaguzi aidha wa kwenye vyama vya siasa ( hasa kwa chama tawala) utastaajabu hao watu wanaoomba kugombea hizo nyadhifa.

Wengi wao ni wale wasio na elimu ya kutosha hivyo hawana hata uwezo wa kukemea au hata kufikisha malalamiko kwenye taasisi au viongozi wa ngazi mbalimbali serikalini juu ya uovu wanaofanyiwa wananchi.

Haya yote yanatokea huku Tandahimba ikiwa na mbunge (Bw. Katani Ahmadi Katani) na mwenyekiti wa CCM ( Bw. Omari Nang'uta).

Yaani ni kama vile wananchi hawa wamekosa mtu wa kuwasemea. Uonevu huu unaofanywa na jeshi la polisi hapa wilayani ni kwa sababu ya udhaifu wa hawa viongozi wetu, hasa uwezo mdogo wa kielimu walionao.
 
Kiukweli askari wa Tandahimba ni wasumbufu sana kwa waendesha pikipiki. Nilienda likizo mwezi Agost mwaka huu. Siku moja wakati natoka kijijini naelekea Tandahimba mjini nikawakuta polisi wamesimamisha gari mikoroshoni halafu ghafla wakatokezea barabarani wakanizuia. Dah, ilikuwa mbinde yaani. Walinieleza kwamba nina makosa 9 hivyo natakiwa kulipa faini shilingi 90,000. Ililazimika tufike kituoni kisha nikamtaarifu ndugu yangu mmoja hivi ni mtumishi wa halmashauri. Alipofika tukalazimika kulipa faini ya shilingi 20,000 tu kwani pikipiki haikuwa na bima halafu haikuwa na kioo cha upande mmoja. Hivyo nakubaliana nawe kwamba hawa askari wa Tandahimba huwabambikia sana raia kesi au makosa hasa kwa waendesha pikipiki.
Mkuu, hiyo kamatakata ya jana ilikuwa si ya kitoto. Yaani walikuwa wanapita maeneo ya maduka kisha wanakusanya pikipiki za wateja hasa waliotoka vijijini na kuzipeleka kituoni ambako wengi wao hutozwa faini pasi kupewa risiti halali za EFD.
 
Nchi hii mwananchi wa kawaida hajawai kuheshimika.Ndo maana unaona kuna mambo ya ovyo ovyo kila mahali yanayofanywa na vyombo vya serikali dhidi ya wananchi.Hadi siku mwananchi atakapotambua thamani yake ndio siku atakayoanza kuheshimika.ila sio mbaya polepole tutafika tu.Kwasasa wacha tuendelee kupiga kelele labda zitaamsha waliolala usingizi wa pono.
 
Pigania katiba mpya hamtaki tungekuwa na katiba bora huyu OCD tungemshitak kwenye independent judiciary
 
Back
Top Bottom