Pre GE2025 2025 ni mwaka wa uchaguzi, tunahitaji Rais atakaye futa hii elimu ya kipuuzi

Pre GE2025 2025 ni mwaka wa uchaguzi, tunahitaji Rais atakaye futa hii elimu ya kipuuzi

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Cashman

JF-Expert Member
Joined
Jun 8, 2018
Posts
3,017
Reaction score
5,294
Tuna raslimali nyingi sana kama madini lakini vinatufaidisha kwa kiwango cha chini sana.Hatuna mitambo ya kuchimba madini hayo,hatuna vifaa vya kisasa kwa ajili ya kilimo,vyote tunaagiza nje,ila tuna vyuo vikuu vingi,pesa nyingi inawekezwa kwenye elimu,tunasoma degrii za manunuzi kwa kuwa kipaumbele chetu ni kununua na siyo kuzalisha.

Nani Rais yule atakayefikiri nje ya boksi na kuufuta kabisa mfumo huu wa elimu ya magharibi?

Tunasoma mambo mengi ya kipumbavu kupoteza muda tu ili miaka ya kuhitimu iwe mitatu,minne au mitano. Lakini ukweli ni kwamba wahitimu ni majanga matupu hawana vitu vya maana kabisa zaidi ya kuongeza misamiati ya fani walizosomea tu.

Dunia imebadilika sana.Kuna vitu vingi mtu anaweza kujisomea mwenyewe tu na akafanya mambo makubwa bila kutumia mfumo wa elimu tulio nao.Mfano kuna watu wamesoma coding bila kufanya mtihani hata mmoja unaosimamiwa na profesa.Wanajisimamia wenyewe katika miradi wanayofanyia majaribio na wanafikia hadi kuwa wabobevu.

Kuna umuhimu wa kufumua kabisa mfumo wa elimu kwa kuanza na wasimamizi wa mfumo huu.Wote wapewe mtihani kueleza ni jinsi gani tutatatua changamoto zetu kwa kubadili aina hii ya mfumo wa elimu.Najua wengi wataandika siasa.Akiandika siasa afutwe kazi bila huruma maana hao ndio wanatuangusha.

Waletwe walimu kutoka China na wapewe nguvu ya kuleta nidhamu.Wanafunzi wanaoonesha uzembe wafukuzwe bila huruma. Tunahitaji Rais asiye mvivu wa kufikiri na anayechukia mambo ya siasa.

Sent from my Infinix X626 using JamiiForums mobile app
 
(Education Sheetstem) na chama cha Mcc iz the problem braza jaribu ku Google hio makitu.
 
Under CCM nothing will happen
Si CCM pekee,hata kwa wapinzani sioni mtu mwenye maono hayo.Wengi wanawaza vyeo tu.Wanaowaza kuhusu nchi,watu na mustakabali wa maendeleo yao kwa namna tofauti siwaoni.
Nchi hii maamuzi magumu yanahitajika

Sent from my Infinix X626 using JamiiForums mobile app
 
Kumbuka fomu ya urais ni moja mzee. Kwahiyo maza anakanyagia mpaka 2030 upende usipende na hatuna usalama wa taifa ila tuna usalama wa Ccm na viongozi wake.
 
Tuna raslimali nyingi sana kama madini lakini vinatufaidisha kwa kiwango cha chini sana.Hatuna mitambo ya kuchimba madini hayo,hatuna vifaa vya kisasa kwa ajili ya kilimo,vyote tunaagiza nje,ila tuna vyuo vikuu vingi,pesa nyingi inawekezwa kwenye elimu,tunasoma degrii za manunuzi kwa kuwa kipaumbele chetu ni kununua na siyo kuzalisha.

Nani Rais yule atakayefikiri nje ya boksi na kuufuta kabisa mfumo huu wa elimu ya magharibi?

Tunasoma mambo mengi ya kipumbavu kupoteza muda tu ili miaka ya kuhitimu iwe mitatu,minne au mitano. Lakini ukweli ni kwamba wahitimu ni majanga matupu hawana vitu vya maana kabisa zaidi ya kuongeza misamiati ya fani walizosomea tu.

Dunia imebadilika sana.Kuna vitu vingi mtu anaweza kujisomea mwenyewe tu na akafanya mambo makubwa bila kutumia mfumo wa elimu tulio nao.Mfano kuna watu wamesoma coding bila kufanya mtihani hata mmoja unaosimamiwa na profesa.Wanajisimamia wenyewe katika miradi wanayofanyia majaribio na wanafikia hadi kuwa wabobevu.

Kuna umuhimu wa kufumua kabisa mfumo wa elimu kwa kuanza na wasimamizi wa mfumo huu.Wote wapewe mtihani kueleza ni jinsi gani tutatatua changamoto zetu kwa kubadili aina hii ya mfumo wa elimu.Najua wengi wataandika siasa.Akiandika siasa afutwe kazi bila huruma maana hao ndio wanatuangusha.

Waletwe walimu kutoka China na wapewe nguvu ya kuleta nidhamu.Wanafunzi wanaoonesha uzembe wafukuzwe bila huruma. Tunahitaji Rais asiye mvivu wa kufikiri na anayechukia mambo ya siasa.

Sent from my Infinix X626 using JamiiForums mobile app
Mfumo wa Elimu na Mifumo yote kwa Ujumla ni hatari kuamuliwa na utashi wa MTU mmoja aliyepo madarakani. Kwavile sasa tunaandaa DIRA ya TAIFA kwanini usipeleke maoni yako ya jinsi unavyotaka mfumo wetu wa Elimu Uwe kufikiwa 2050. Huu ni mtizamo tu.
Ahsante
 
Elimu yetu ni majanga imejikita kwenye uongozi sehemu nyingi.Haiwezekani Mungu katupa madini halafu tunakosa elimu ya kuyachimba na vifaa ambavyo tukiacha kununua v8 ishirini tunanunua vifaa vya kuchimba na kuuza wenyewe madini yetu.Siasa nayo inatuvuruga hakuna hata mwanasiasa mmoja hata wa upinzani anayeongelea elimu bora na mabadiliko.Kilimo ni uti wa mgongo ila kuna chuo kimoja kikuu cha kilimo.Maeneo ya viwanda yamekuwa ya viwanda vya kuuza maneno (ibada)Tunahitaji akili na madiliko,mbona mchina na India wameweza.Ila pia wazazi waanze kubadili elimu za watoto wao na kuwapeleka kwenye masomo yatakayowawezesha kufanya kazi wakimaliza masomo.Masomo ya vitendo yamekuwa hadimu sana kila mtoto anaandaliwa kuwa boss hii ni hatari
 
Back
Top Bottom