2025 nitachukua fomu kupitia CCM na nitampinga huyo mnaetaka asipingwe

2025 nitachukua fomu kupitia CCM na nitampinga huyo mnaetaka asipingwe

Mganguzi

JF-Expert Member
Joined
Aug 3, 2022
Posts
1,604
Reaction score
3,715
Kwanini nguvu kubwa inatumika kutulazimisha tuvunje kanuni na katiba Kwa kututisha? awamu ya tano inamalizika 2025 ndipo tuanze awamu ya SITA.

Kanuni za kawaida za chama ni kuchukua fomu ama kutangaza nia, watu washindanishwe apatikane alie bora.

Kwa Nini Jakaya na Makamba wanataka tule chakula bila kukipika? Kama mtu ni mzuri na kafanya mambo makubwa kwanini mnaogopa kumshindanisha na wengine? Au mnamaslahi binafsi hivyo mnaogopa mkimshindanisha ataanguka? Huyu ni Rais ambae kama atapata ridhaa ya watanzania kipindi chake rasmi kitaanza 2025. Kwa Sasa anaongoza kipindi Cha mpito.

Mimi binafsi nimewaona wastaafu wetu kama watu waliolewa mvinyo ya utawala! Kama nilivyowahi kutangaza mwanzo narudia Tena 2025 Mimi nitachukua fomu ya urais kupitia CCM, na nitampinga yeyote atakaeingia kwenye kinyang'anyiro hicho!

Kwa hoja .endapo fomu ya urais nitanyimwa nitakwenda mahakamani haraka sana na kuzuia uhuni wa aina yoyote. Mimi nitashindana nae na nitamshinda saa mbili asubuhi!
 
Kwanini nguvu kubwa inatumika kutulazimisha tuvunje kanuni na katiba Kwa kututisha? awamu ya tano inamalizika 2025 ndipo tuanze awamu ya SITA...

Kama namwona johnthebaptist na timu nzima ya chawa nyuso zilivyowasawajika.

Hiiiiiiii bagosha!
 
Back
Top Bottom