34% ya Wagonjwa Hospitalini wanasumbuliwa na Magonjwa Yasiyoambukiza

34% ya Wagonjwa Hospitalini wanasumbuliwa na Magonjwa Yasiyoambukiza

BARD AI

JF-Expert Member
Joined
Jul 24, 2018
Posts
3,591
Reaction score
8,826
e8edf8df5e3a7ff770dd6a227b7ec9d6.jpg


Mwenyekiti wa Mtandao wa Magonjwa Yasiyoambukiza, Prof. Andrew Swai, ameyataja baadhi yanayosumbua Watu wengi kuwa ni pamoja na #Kisukari, #Saratani, Magonjwa ya #Akili, #Figo, #Macho na Shirikizo la Damu.

Kwa mujibu wa Mkurugenzi wa Magonjwa Yasiyoambukiza, Prof. Paschal Rugajo, sababu kuu za kuongezeka kwa Magonjwa hayo ni pamoja na Wananchi kupuuza Ushauri wa Wataalamu kuhusu kubadili Mtindo wa Maisha hasa #LisheBora na #Mazoezi.

Takwimu za Wizara ya Afya zinaonesha mwaka 2017 Magonjwa Yasiyoambukiza yalichangia Vifo 134,600 sawa na 33% ya Vifo vyote vilivyotokea. Aidha, gharama zilizolipwa na NHIF kwa Magonjwa hayo zikifikia Tsh. Bilioni 99.09 kwa mwaka 2021/22.
 
Mifumo mibaya ya maisha inachangia kwa kiasi kikubwa , mamlaka ya chakula na madawa nao wamelala usingzi wa pono , tbs kuna uozo mtupu , apa haujaja kwenye ugumu wa maisha changamoto za ndoa na mahusiano , apa unakosaje kisukari pressure na sonona?
 
Hivi bajeti ya kukimbiza mwenge ni sh ngp
Bajeti ya kuwalisha dawa watumia unga sh ngapi
Bajeti kwa wagonjwa was ukimwi ni sh ngapi
Bajeti ya kuendesha shirika la ndege ni sh ngapi.

Mambo yote haya ni liability kwa serikali ambayo inaweka vipaumbele kugharamia anasa au madhara yanayotokana na anasa.

Ukijua hilo utaungana na familia zenye wagonjwa wa magonjwa haya dume, Sarakani, Figo.
Wa kutoa,wito kwa Serikali kutoa msamaha wa matibabu kwa magonjwa haya. Kama kweli hii ina watendaji wenye dini.
 
Back
Top Bottom