65% ya Wazawa Kusugua BENCHI Simba

Amavubi

JF-Expert Member
Joined
Dec 9, 2010
Posts
30,156
Reaction score
13,258


Kama mchezaji umebahatika kuingia kwenye kikosi cha kwanza cha Mcameroon, Joseph Omog ndani ya Simba basi unatakiwa kupambana kwani ukizingua tu, benchi litakuhusu.
Hiyo ni kauli ya Kocha Msaidizi wa Simba, Mganda, Jackson Mayanja, aliyoitoa mara baada ya mchezo wa kirafiki na AFC Leopards ambapo Simba ilishinda kwa mabao 4-0.
Lakini wakati msaidizi akisema hivyo, bosi wake, Joseph Omog amewapa masharti magumu wachezaji wa kimataifa akiwemo Mrundi Laudit Mavugo kwa kuwambia ole wake atakayekaa benchi.
Omog amesema kuwa hakuna mchezaji wa kimataifa ambaye atakaa benchi kutokana na kuonyesha uwezo mdogo, badala yake kila mmoja anatakiwa ajitume ili aweze kupata nafasi ya kucheza katika kikosi cha kwanza.
“Usajili nilioufanya unaendana na uhitaji wa kikosi changu na nimesajili wachezaji wa kimataifa kwa kuangalia kila mmoja anakuwa na kiwango na kila mmoja nahitaji acheze labda itokee mtu awe anaumwa kwani mchezaji wa kimataifa anatakiwa awe na uwezo zaidi ya wazawa.
“Kwa sasa bado sijapata kikosi cha kwanza japokuwa kuna baadhi ya wachezaji wanaonyesha kuwa na kiwango kizuri cha kucheza katika kikosi cha kwanza. ambaye atakaa benchi kutokana na kuonyesha uwezo wa chini huyo atakuwa hatufai,” alisema Omog.
Wachezaji wa kimataifa waliopo Simba ni Vicent Angban, Mavugo, Juuko Murshid, Musa Ndusha, Janvier Bokungu, Fredrick Blagnon na Method Mwanjale.
Upande wa Mayanja alisema usajili wao walioufanya chini ya Omog umekidhi viwango walivyokuwa wanavihitaji kwa ajili ya kuleta ushindani wa namba.

HAYA NDIYO MASHARTI ALIYOPEWA MAVUGO NA WENZAKE NA KOCHA WAO JOSEPH OMOG - SALEH JEMBE

7/11 x 100=64%
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…