8th Sullivan Summit Arusha Tanzania

Samahani kwa kudisrupt mada.S&DsL nashukuru kwa ushauri wenu,na dk wangu amenisaidia pia.

I was sober ktk matukio niliyoeleza awali ila ilibidi niwashughulikie baada ya kuona wanataka niwape hongo.I am not ready to buy my rights,not at all, because I know them.Siwezi kuuza uhuru wangu hata siku moja.Wakuu wao walinielewa sana kama mdau makini na ndiyo maana waliyazima haraka.

Back to the topic ni kwamba huyu AY ni nyoka na hatutakiwi kumpa nafasi ya kutema sumu yake tena, hata kama ni Afroamerican..to hell.Hatumtaki kabisaaa kwenye society yetu!Possibly is W.Africa descendant maana amefanya mengi ukanda huo.Hao watu nimewahi kuishi nao, but everybody has to be extra careful because they are not reliable at all.Nadhani wengi mnajue au mmesikia vituko vyao sehemu mbalimbali za dunia. Binafsi nilikuwa nahakikisha passport iko mwilini mwangu punde walipotembelea kwangu maana ilikuwa moja ya target zao siku hizo.

Ninaanza kujiandaa namna ya kum-boycott huyo AY hapo Arusha.
Mungu anijalie uzima.

Nilikuwa najiuliza kulikoni, mbona viongozi wengine kutoka Africa wamekataa mwaliko wa kuhudhuria hiyo summit.Nahisi walishtukia kuwa hilo ni bomu.

Hii issue ya ndugu zatu kufukiwa live imeniuma sana.Siku zile Mrema akisumbuliwa sikuweza kuelewa uzito wa madai yake maana hoja ilitekwa na kupewa sura ya uchochezi dhidi ya serikali ili kutoa negative perception kwenye society.

But no way, hii kitu lazima tuifufue upya.Huu unyama tuukatae kwa nguvu zote.Hawa ndugu zetu waliofukiwa kikatili inabidi tutumie means tuwafukue!Tunaweza!!With all evidence, we can look forward towards justice.Inaniuma sana kwa kweli.
 
Huyu AY appears to be very well connected! Lakini ni kweli wamemshtukia wengi. Nina uhakika after the Nigeria fiasco wengi wamemkimbia. Hata hii summit ya Abuja ambapo Kikwete alipewa torch na Obasanjo, ukiangalia marais waliokuja ni rais wa Sudan! Mauritania! and Rwanda... Kagame naye atakuwa na dili na akina AY.
Hii Sullivan summit ni bomu! Haitatuongezea kitu! Watuambia watu na kampuni za maana zilizo-confirm participation.
Ingekuwa kama Doha trade talks sawa! Lakini cheki CNN, BBC etc uliona ile Abuja summit inakuwa mentioned?
 
Talk about briefcase investors! Unatoa mobile phone number!
Jamani! Watanzania WAKE UP!

..phone number from a mobile operator,how about that?

..makampuni ya simu za mobile hufunga simu maofisini pia,ukiziangalia utadhani ni landlines.
 
Naomba nikiri kwamba kunakitu nimeandika hapo juu na kisha nimesoma data nimekuta this information inayoonyesha, maybe AY can pull some important people to the summit. But tukumbuke Clinton ana special relationship, Chevron ni client wake through GoodWorks INternational, Wolfowitz ni mshikaji wake na mentor yao alikuwa George Schultz etc. But kinachonishangaza ni kuwa hata visit ya Bush haikuwamentioned on CNN na BBC kwamba pia alihudhuria Sullivan summit
Anyway wamekuwa na hiyo summit mara 2 in Abuja due to the special relationship of Obasanjo and AY (check earlier posts zangu). So does JK and AY have a 'special relationship' too? Let's wait and see, I cannot speculate...
 
..phone number from a mobile operator,how about that?

..makampuni ya simu za mobile hufunga simu maofisini pia,ukiziangalia utadhani ni landlines.

Ok, point taken. But I have a feeling that it is a mobile phone not ya ofisini! But I would like to point out that kama wewe mbongo ukitoa mobile phone only kwa kampuni au mtu yeyote na unasema that you are a serious company, wengi watakushangaa, especially as TTCL line siku hizi ni kitu rahisi sana kupata. Also kwa ofisi ya maana kama hiyo they should have fax number as well. Sijuii hiyo contact address imekaa kiaina aina!
 
Susuviri:
Tunashukuru sana kwa data zinazotuwezesha kuunganisha 'vidoti.'

Lakini wakati tukifanya hivyo, tujiulize pia katika hali ya leo ya utandawazi, hivi ni kweli watu wa namna hii tunaweza kuwaepuka? Ingekuwa inawezekana kuepukana nao, mimi ningekuwa wa kwanza kabisa kuwapiga madongo hawa. Lakini, ndugu yangu, kama unavyojua, tunaambiwa leo kuwa hatuwezi kuwa na maendeleo bila ya kuwa na wawekezaji,......sasa wawekezaji wazuri tuuuuu ni akina nani, na wapo wapi? Hasa waTanzania tumelemaa mno sasa na dhana hii ya kuamini kuwa hatuwezi kujiletea maendeleo sisi wenyewe bila ya kuwategemea wawekezaji. Na lililo baya zaidi kuliko yote, ni hawa viongozi wetu kutokuwa na msimamo wa kuweka maslahi ya nchi yetu mbele zaidi kuliko kujitafutia sifa wao wenyewe na kujishibisha zaidi. Tofauti kubwa sana iliyopo kati ya mtu kama Kiwete na Kagame iko wazi. Hawa Sullivan wakienda Rwanda, usitegemee kuwa hawatabanwa ipasavyo ili waonyeshe maendeleo watakayowapatia waNyarwanda. Kwetu watakuja tu kuvuna kwa kutuibia na kuondoka. Hili ndilo linalosikitisha zaidi.

WaTanzania, kila mara tusisahau - hakuna atakayetuletea maendeleo.
 

..hiyo namba itakuwa ya jill!

..refer post yangu ya kwanza!
 
Thanks DSL kwa information
Naomba kuuliza nimepata jina la mtu anaitwa Richard Swai. Yeye ni Chief Investment Officer wa Souther African Entreprise DEvelopment Fund (SAED). Je ni Mtanzania (I think 'yes') na ana uhusiano gani na issue hizi. I am sure there's a connection lakini sioni, kwani katika SAED, Chairman kama nilivyoandika ni AY alafu member mwingine ni Carlton MAsters ambaye yuko na AY katika Sullivan Summit na walianzisha pamoja Good Works. SAED iko chini ya USAID na ilianzishwa na Clinton but it smells fishy!
So who is Richard Swai? Anybody?
 
NImepata data zifuatazo:
No mention kama ni mtanzania. Picha yake iko kwenye website
link
http://www.saedf.org.za/main.php?id=02&subid=03
 
Where is Nyerere guys? We need him desparately back!

absolutely agree with you! Nyerere alikuwa hataki upumbavu huu na alikuwa anaona mbali! Lakini jinsi ninavyozidi kufanya research nazidi kupata hasira, but I am channeling this into something positive kwa sababu nazidi kutafuta. Sasa naomba waandishi wanaotembelea JF wafanyie kazi hili suala! If you expose this I am sure itakuwa another case! We are not doing anything just asking questions!
 

Susuviri:
Richard Swai ni CIO wa hiyo SAEDF; na inaelekea ni mwanachama mwenzetu hapa JF ingawaje naona huwa hachangii sana.
Mara ya mwisho alitembelea hapa 11 Dec. 2007 at 02:59 AM. Alijiunga na JF 7 Oct. 2007.
Alitumia jina lake hilo hilo la Richard Swai, na unaweza kumpelekea e-mail kupitia humu JF.
Wasifu wake wote upo wazi; kwa mfano shule alizosoma akiwa huko Marekani na sehemu alizowahi kufanya kazi.
Inaelekea kwenye uchaguzi wa 2005, naye alichujwa katika kinyang'anyiro cha ubunge kupitia CCM, huko Korogwe.

Sioni kashfa kubwa na huyu mtu, ila nadhani ndio yumo njiani kutumika na wakubwa katika mipango yao.
 
Where is Nyerere guys? We need him desparately back!

Rev. Kishoka, kwani unadhani kupata asimia 80 ya kura zilizopigwa ni jambo rahisi tu? Watu walidhani wamempata Nyerere mdogo. Jamaa aliweza kujibana vizuri sana miaka yote hiyo, kiasi kwamba hakuna aliyekuwa na wasiwasi naye kabisa. Sasa hivi ndipo watu tunajaribu kupitia kwenye nyayo zake tuone dalili zozote zilizotuhadaa wengi; lakini hatuambulii kitu.

Sasa sijui kama tutaendelea kupagawa hivyo hivyo hapo ifikapo 2010! Labda wakati huo tutakuwa tumepata sababu nyinginezo za kutufanya tuwe hivyo.
 
Na wawekezaji wanaamini wamempata Nyerere wao in Kikwete. Yaani ungesikia misifa aliyomiminiwa juzi na AY, sikuamini kabisa.Susuviri, Richard Swai ni Mtanzania. Hivi sasa anafanya kazi Afrika Sauz. Nadhani ameajiriwa na Goodworks International, au kampuni inayomwajiri ina uhusiano wa karibu naye. Wameshanunu Mount Meru Hotel pale Arusha
 

Kuna post niliweka kwenye thread nyingine, mwaka 2005 kabla ya uchaguzi nilipita pita kwenye GSU AYSPS forums, baadaye AY akawa anamzungumzia Kikwete kusema kweli inaonekana anamjua vizuri.
 
Duh! hapa ndipo napochoka na Wabongo..
Damn, ndio maana Wakenya wamechukua mlima Kiimanjaro, sisi tumebaki kulaumu tuuu hata kama hatufahamu nini malengo ama minutes za mkutano mzima. Yaani huu mkutano tu umeyazua yote haya na kama hayupo Bush ama kiongozi mweupe anayejulikana basi hili ni deal la walaji!...wakati tumesha liwa sana na wa South, Waarabu wakaingia Wagiriki na Wataliani, waingereza na mwisho Wa - Canada wotenao wanatumaliza bado tu wasiwasi wetu mkubwa ni mtu mweusi mwenzake..Ni tabia ambayo imefanya Watanzania tuogopane hata huko nchi za nje hatuna ushirikiano kabisa zaidi ya upishi wa majungu...
Ukitazama saana hii ni tamaduni yetu Wabongo kuwa ni bora apate mtu wa nje (hasa mzungu ama mweupe) lakini sio rafiki ama ndugu yako!..Na atakayepata ni zake binafsi hazina ubia na mtu.
Kutokana na hali kama hii kamwe hatuwezi kuendelea kwani huu sio ujanja hata kidogo ila ni kuwa insecure na maradhi yanayotokana na inferiority complex. Mara nyingi ni vigumu kwetu ku question utajiri, elimu ama uwezo wa Mhindi, mzungu ama mwarabu lakini inapofikia kuwa ni mmatumbi mwenzetu.... Loooh! hata kamati za ufundi zitatembelewa...
 
Mkandara,

Sasa hivi hapendwi mtu! Awe Mmanga, Mbulushi, Mchina, Mthailnd, Mzungu au Mnugu!

Tatizo si nia ya AY au Sullivan ambao wote ni lobbyist walioko ule mtaa maarufu pale DC K Street. Tatizo ni what does Tanzania get or benefit out of this?

Ukiangalia picha ya Karamagi, Mahiga, Young (board Member wa Barrick) na huyo mtasha (is is Sinclair?) ambayo ilipigwa mwaka jana, halafu February ya 2007 Karamagi anaingia mkataba wa miaka 50 ambao mnufaikaji wa 99% ni Barrick na si Tanzania, then you have to be suspicious of everything that is happening at current state of Tanzania.

Kasungura ana jeshi lake la kula na kukwapua bila huruma (IPTL, TDC, DAWASCO) na Muungwana ni Mtwana wa Sinclair, Barrick, Tudor kupitia Karamagi.

Kama Pundit alivyosema awali, Muungwana si lazima awe na meno makali kama Kasungurabali yeye ni facilitator mkubwa kwa cheo chake (ama kwa kujua au bila kujua).

Sasa ukisoma maneno ya Cynthia Mckinney, itabidi ujiulize, Bulyanhulu walizikwa watu wakati Muungwana alikuwa waziri wa madini. Sinclair altamka hadharani 2004 kuwa Rais ajaye wa TZ ni rafiki yake wa Takriban miaka 17 (Sutton ilishaingia Tanzania at that time na waziri wa madini aliyeshughulikia Sutton ni Muungwana), Karamagi kasaini mkataba 2007 halafu 2008 Kongamano laja kutaliii Arusha na watakaa kwenye hoteli yao Mount Meru, jee ni faida gani Mtanzania anapata? is this the win win situation?

Jee Kamati ya Bomani wanaweza kufanya kazi yao kwa makini kuhusu mambo ya madini ikiwa principle mkuu wa yote haya anapewa sifa na Board Members wa Barrick?

On the other hand, kama wao (Sullivan, GoodWorks) ni lobbyist, na mshikaji Richard anafanya kazi nao, ni vipi walituachia tukazama mkenge na RDC, Buzwagi au hili skendo la ATC?
 
Eeeh, sasa naona 'dots' zinaunganishwa hasa! Rev. Kishoka, hizi ndizo nadharia za 'conspiracy' zisemwazo nini?

Mwelekeo una-make sense, unless proved otherwise!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…