Kasie
Platinum Member
- Dec 29, 2013
- 22,379
- 41,294
Habari za jumapili,
Basi bana sina hili wala lile, leo sikuwa na mpango wa kuamka mapema kwa sababu kadha wa kadha.
Ghafla nakatishwa usingizi na simu asubuhi asubuhi aaagghhh kuangalia namba mpya. Nikaachana nayo nikarudi kulala nikasema ntaipiga baadae nikiamka.
Baada ya hiari yangu na kupata stafutahi nikashika kilongalonga nirejeshe simu na jumbe zilizoingia. Oohhh laalaah kumbe ile simu ilikuwa ya Ahmes from Egypt.
Huyu Ahmes tulikutana huku Tanzania kwenye tour sites flani hivi. Mie nilienda kivyangu ila tulijikuta tuko kundi moja na tour guide alikuwa mmoja, wao walikuwa wengi.
Sasa macho yake sijui yaliona nini, siku tumemaliza tour akaniomba namba ya simu, sikuona hiana nikampa. Aahahahahaha Ahmes sijui amelewa haluwa, ananialika nikatembelee moja ya maajabu saba ya Dunia Egypt kwa gharama zake.
Na Covido hii hata sithibutu, wali harage bado mtamu π . Nimemwambia afanye maandalizi ntafika huko mwisho wa mwaka (Desemba) nikiwa likizo.
Ila Ahmes anajua kudekeza kwenye simu looh hadi nikajikuta narembua.
Natumai ntachomoka salama...π
Mahaba Matata.
Basi bana sina hili wala lile, leo sikuwa na mpango wa kuamka mapema kwa sababu kadha wa kadha.
Ghafla nakatishwa usingizi na simu asubuhi asubuhi aaagghhh kuangalia namba mpya. Nikaachana nayo nikarudi kulala nikasema ntaipiga baadae nikiamka.
Baada ya hiari yangu na kupata stafutahi nikashika kilongalonga nirejeshe simu na jumbe zilizoingia. Oohhh laalaah kumbe ile simu ilikuwa ya Ahmes from Egypt.
Huyu Ahmes tulikutana huku Tanzania kwenye tour sites flani hivi. Mie nilienda kivyangu ila tulijikuta tuko kundi moja na tour guide alikuwa mmoja, wao walikuwa wengi.
Sasa macho yake sijui yaliona nini, siku tumemaliza tour akaniomba namba ya simu, sikuona hiana nikampa. Aahahahahaha Ahmes sijui amelewa haluwa, ananialika nikatembelee moja ya maajabu saba ya Dunia Egypt kwa gharama zake.
Na Covido hii hata sithibutu, wali harage bado mtamu π . Nimemwambia afanye maandalizi ntafika huko mwisho wa mwaka (Desemba) nikiwa likizo.
Ila Ahmes anajua kudekeza kwenye simu looh hadi nikajikuta narembua.
Natumai ntachomoka salama...π
Mahaba Matata.