A. Mahimbo apeleka pingamizi kwa Pengo dhidi ya Dr Slaa

Mkuu DALLAI LAMA mtu akidai haki yake basi anakuwa anatumika? Hii kitu kwa Dr. Slaa inaonekana kuwa janga. Mahimbo anatumika, Rose Kamili anatumika!

Mkuu kabla ya kuendelea na hizi 'brouhaha' ambazo ninaamini kwa 100% kuwa zina mkono wa CCM wakidhani ni karata ya kuiangushia CDM, mtueleze kwanza ile kesi aliyofungua Mahimbo wakati wa uchaguzi mwaka 2010 kwa msukumo wa Rajab Makamba na kundi lake iliishia wapi?. Je zile hela walizompatia wakati ule zimeishia? wamemuahidi nyingine?.

Hivi tukianza hasa kuchambua maisha binafsi ya viongozi wa CCM na mawaziri kuna mtu atabaki salama. Si bora Dr slaa yeye ameweka wazi uhusiano wake na Josephine na kuamua kufunga ndoa kuliko wale wanaochukua vibinti vya vyuoni na hata kuwapatia madaraka wake za watu na kuwafanya nyumba ndogo zao?.

Hizi ni politics ambazo CCM will be the biggest loser, maana wananchi wanawafahamu na kuwajua viongozi wote wa CCM vizuri sana linapokuja suala la infidelities.
 
Acha uongo huyu jamaa hana mke,unamzushia bure wacha jamaa adahi mke wake,naomba nikuulize swali la kizushi wewe baba yako angeibiwa mama yako ungefurahi?acha kutetea dhambi ya uzinzi,huyo Josephine ni mzinzi!

unataka kuniambia kuwa huyu jamaa mda wote huo alikuwa hagongi mzigo mwingine?
 
Mkuu Nikupateje.
Kwa hakika umenifumbua akili hata mimi. Asante. God blease you.
 
Mahimbo anatumika kama toilet paper tu ?
 
wewe huwa hutumii? Kama hujawahi fanya ngono utakuwa we ni ccm maana ndo WATAKAVITU..pambav.MNATAFUTA SINGO MPYA KUMSUMBUA DR KILA MARA ILA TUMEWAZOEA.


Wewe sasa hapa itikadi za vyama zinakujaje, kwanini hutaki kukubali kuwa Slaa amechukua mke wa mtu na amemtelekeza mzazi mwenzie?
 
It just a delay tackicks!lilopangwa limepangwa huyo mahimbo na kamili madai yao hayawezi mnyima usingizi Dr.
 

mbona raisi wako anawake wa ndoa wengi na bado anazini na wanawake wengine? Asili haipotei ndugu
 


Mkuu usimvunje moyo mwenzio, umesahau Kipenda roho hula nyama mbichi, hacha apiganie haki yake ya ndoa
 
Mahimbo anafikiri mke ni kama commodity!!! eti Slaa amrudishie mke wake...hahahahahahahahahahaha
 
Nikupateje Mkuu asante kwa ufafanuzi ulioshiba nimejifunza vitu ambavyo nilikua sivijui,ubarikiwe sana.!
 
Last edited by a moderator:
Acheni upotoshaji kama kuna zuio la ndoa unapaswa kupeleka kwa paroko wa mtu na wala sio kwa Pengo.Kanisa katoliki sio kilabu cha pombe, kuna hierarchy
 

Kwa yale aliyoyafanya 2010, na haya anayofanya sasa, ninashawishika kuamini kwa dhati kabisa kuwa ulifanya uamuzi wa busara wa kuachana naye. Kwa saikolojia ya wanaume, kufanya haya anayoyafanya sasa, huyu hayupo sawasawa. Kama kuna jambo ninaloweza kukusikitikia Josephine, ni kutofanya uchunguzi wa kina hata kabla ya kuwa na huyu jamaa, ungekuwa makini ungefahamu kuwa huyu si sawasawa.

Pamoja na yote haya anayoyafanya, nina imani hayasaidii wala kupunguza chochote, ndoa hufungwa moyoni mwa mtu wala si kanisani, mahakamani au kwa Mkuu wa Wilaya. Nadhani mwanaume huyu nia yake kubwa ni kutaka angalao na yeye watu wamfahamu kuwa yupo katika ulimwengu huu.
 
Nikupateje,

Hivi mie na wewe nani kakurupuka? Narudia tena Mahimbo alifunga ndoa na Josephine Sep 7, 2002 kwenye Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Ushirika wa Kijitonyama...sasa kama wewe uitambui utajijua mwenye na wameishapata watoto wa wawili.

Naomba nikuulize kwa hiyo Katoliki wanaruhusu kupora mke wa mtu kwa sababu hawayatambui Makanisa mengine?
 
Last edited by a moderator:

Riztz

Kwa imani ya Kanisa katoliki, Tony Blair alifanya ufuska na mkatoliki aitwaye Chery Blair hadi miaka minne iliyopita Tony Blair alipojiunga na Ukatoliki kutoka Anglican.

Kwa imani hiyohiyo na msingi huohuo, Jakaya Kikwete anafanya ufuska na Salma Kikwete hadi siku Jakaya na Salma watakapoamua kuacha uislam na kujiunga na ukatoliki kama mwenzao Tony Blair alivyojiunga.

Ndivyo ninavyotakiwa kuitetea imani yangu na utaona kuwa tumewastahi vya kutosha tunapokaa kimya tusitetee imani yetu tukiogopa kuwaudhi.

Ila mnapotuudhi kama hivi basi inabidi tu-quote imani yetu na ndipo tujue ni nani anarusha mawe wakati amekaa kwenye nyumba iliyojengwa kwa vioo.
 

mkuu natumia simu ningekugonga like
 

Mods huyu jamaa ametumia maneno ya kuudhi. Naomba muongozo au ban
 
Huyu jamaa anawatia aibu wanaume wenzie; yaani bila lepe la soo eti anirudishie mke wangu.... wanawake wameisha? Au amejaribu wote wanamtolea nje? lol. No wonder dada yangu Josephine kampiga chini; anaonekana ni mwanaume dhaifu. Lol.


Hivi wewe kwa akili yako unaweza kumtaka mwanamke aliyekuacha akaenda kuishi na mwanaume mwingine hadi wamezaa mtoto! Unaweza kuendelea kumwita ni mkeo eti kwakuwa tu una cheti cha ndoa! Unadhani ndoa ni cheti au ni uhusiano!? Shtuka!
 
Nina shida na uelewa wa Mahimbo. Hivyo huyu kweli ni mwanaume!
 
Hii ndoa itakuwa halali kisheria kwa sababu tayari kuna divorce kati ya Mahimbo na Josephine. Hakuna kardinali atakayeweza kuzuia hii ndoa UNLESS
Ndoa kati ya Mahimbo na Josephine ilifungwa kanisa katoliki ... ambalo halina divorce.
Ila kama ilifungwa wilayani au assemblies of god ni Josephine mwenye uamuzi wa kuitambua au kutoitambua ndoa hiyo kabla ya ndoa yake na Dr. Slaa haijafungwa kikatoliki.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…