Leslie Mbena
JF-Expert Member
- Nov 24, 2019
- 207
- 677
A POLITICAL WATCHDOG:HUMPHREY POLEPOLE MZALENDO ANAKAYEKWENDA KUSIMAMIA UWAJIBIKAJI NDANI YA BUNGE NA KUREPORT KWA MHE RAIS.
Leo 14:45hrs 29/11/2020
Mjumbe wa Halmashauri Kuu Taifa,na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi,Taifa,Ndugu Humprey Polepole,kwa Umakini na Uzalendo wa hali ya juu anakwenda kuwa msimamizi wa uwajibikaji wa wabunge ndani ya Bunge la 12,Ndugu Humprey Polepole kwa Uzalendo, akili na upevu wa kuelewa mambo na uwezo wa kujenga hoja chini ya misingi ya nadharia ya falsafa ya Ujamaa na Kujitegemea kama ilivyoasisiwa na Mwalimu Julius Nyerere, kuendelezwa na Hayati Edward Sokoine na kudumishwa na Rais John Magufuli,
Sasa Uzalendo unakwenda kukua ndani ya Bunge la 12 ambalo litakuwa likitunga sheria za Kizalendo zaidi hasa baada ya Wapinzani kukataliwa na Wananchi kwenye Uchaguzi wa mwezi Oktoba 2020,Ndugu Humprey Polepole anakwenda Bungeni kuonesha namna gani nadharia za kifalsafa za Ujamaa na Kujitegemea zitaweza kuleta chachu ya uwajibikaji, Uzalendo na ufanisi katika shughuli zote za Watanzania,katika usimamizi wa falsafa ya Ujamaa na Kujitegemea,Ndugu Humprey Polepole atatoa muelekeo na uwakilishi wa jamii ya Watanzania kisiasa, kiuchumi na kimaadili katika kipindi chote cha bunge la 12.
-Strategic move
Sera nzuri katika ilani ya CCM zinahitaji umakini,useriousness katika utekelezaji wake,anahitajika mtu perfect union kwa Mheshimiwa Rais atakaesimamia utekelezwaji wa ilani hiyo ndani ya Bunge,halitakuwa Bunge la kulala bali Bunge la utekelezaji wa sera nzuri zilizopo kwenye ilani ya CCM, tumezoea awamu ya mwisho ya Rais aliye madarakani ni awamu ya wabunge wengi kuanza michakato ya chini kwa chini kutaka kumrithi aliye Madarakani,Mara nyingi michakato hii inafanya Serikali pamoja na Chama kuyumba maana wengi watahujumu ili kutafuta uhalali wao,Ndugu Humprey Polepole anakwenda kuwa jicho la chama kwa wabunge wote ndani ya Bunge la 12.
Itoshe tu kusema Polepole ni katika wajengaji hoja Mahiri kupata kutokea katika ardhi hii ya bara la Africa,Ukimuona Ndugu Humprey Polepole unaona picha mbali sana,utaona uadilifu ndani yake,utaona Uzalendo ndani yake,utaona uwajibikaji kwa maslahi ya Taifa letu,akiwa Mbunge asiye na Jimbo,lakini akiwa Mtendaji ndani ya CCM,kwa maana misingi ya kazi ya idara ya uenezi ni ya kiutendaji pia ni kuwa msemaji wa chama,kwa maana hiyo atafanya kazi za Chama kama majukumu ya muda wote.
Kwenye Chama Mbunge ni cheo na kwa nafasi ya maamuzi yanaishia kamati ya siasa ya wilaya na mkoa. Mbunge haingii Halmashauri Kuu taifa,lakini Ndugu Humprey Polepole kwa fimbo ya Katibu wa itikadi na Uenezi,na Ujumbe wa Halmashauri Kuu,Taifa ataingia kwenye kikao cha Halmashauri Kuu ya CCM na kutoa report ya Bungeni,nani mvivu na Wananchi wa Jimbo lake wanasemaje kuhusu Mbunge huyo,kumbuka Halmashauri kuu ya CCM, Taifa ni chombo cha pili kikubwa kwa maamuzi baada ya Kamati kuu ya CCM,Kwa jicho la kibinafsi na kimaslahi nafasi ya ubunge ni kubwa kuliko Uenezi Taifa kwa maana ubunge unakupa promising future ya kisiasa kitaifa, maana mbunge anaweza kuwa waziri na kuingia kwenye Baraza la mawaziri,hili likitokea kwa Ndugu Humprey Polepole,basi atakwenda kureport ndani ya Baraza la Mawaziri,nini kinatendeka Bungeni,Mbunge gani mzembe na hatua gani zichukuliwe,
Nimalizie kwa kuwapa maono yangu juu ya CCM kuwekeza vilivyo kwa Vijana ambao watakuwa Viongozi makini, Wazalendo,wawajibikaji wenye uchungu wa nchi hii ya Tanzania, na ndio maana tumeona uteuzi wa Ndugu Humprey Polepole, uteuzi wa kuaminika ambapo atakwenda kureport kwa Mheshimiwa Rais John Magufuli moja kwa moja kutoka Bungeni,nini kinafanyika Bungeni,nini Mbunge huyu anafanya,mbona Wananchi wake wa Jimbo mfano la Morogoro wanasema hivi,Ndugu Humprey Polepole atakwenda kuwa msimamizi,kwa kizungu "watchdog" kwa kofia ya Mjumbe wa Halmashauri Kuu na Katibu wa Itikadi na Uenezi,Taifa.
Nikiishia hapa,Mimi ni
Msemakweli Chakubanga,
Dar es Salaam.
0755078854
-Bachelor of Business Administration in International Business
-Master of Leadership and Management.
Recent Publication;
-Assessment on the Effects of Micro-Financing on Poverty Reduction.
Leo 14:45hrs 29/11/2020
Mjumbe wa Halmashauri Kuu Taifa,na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi,Taifa,Ndugu Humprey Polepole,kwa Umakini na Uzalendo wa hali ya juu anakwenda kuwa msimamizi wa uwajibikaji wa wabunge ndani ya Bunge la 12,Ndugu Humprey Polepole kwa Uzalendo, akili na upevu wa kuelewa mambo na uwezo wa kujenga hoja chini ya misingi ya nadharia ya falsafa ya Ujamaa na Kujitegemea kama ilivyoasisiwa na Mwalimu Julius Nyerere, kuendelezwa na Hayati Edward Sokoine na kudumishwa na Rais John Magufuli,
Sasa Uzalendo unakwenda kukua ndani ya Bunge la 12 ambalo litakuwa likitunga sheria za Kizalendo zaidi hasa baada ya Wapinzani kukataliwa na Wananchi kwenye Uchaguzi wa mwezi Oktoba 2020,Ndugu Humprey Polepole anakwenda Bungeni kuonesha namna gani nadharia za kifalsafa za Ujamaa na Kujitegemea zitaweza kuleta chachu ya uwajibikaji, Uzalendo na ufanisi katika shughuli zote za Watanzania,katika usimamizi wa falsafa ya Ujamaa na Kujitegemea,Ndugu Humprey Polepole atatoa muelekeo na uwakilishi wa jamii ya Watanzania kisiasa, kiuchumi na kimaadili katika kipindi chote cha bunge la 12.
-Strategic move
Sera nzuri katika ilani ya CCM zinahitaji umakini,useriousness katika utekelezaji wake,anahitajika mtu perfect union kwa Mheshimiwa Rais atakaesimamia utekelezwaji wa ilani hiyo ndani ya Bunge,halitakuwa Bunge la kulala bali Bunge la utekelezaji wa sera nzuri zilizopo kwenye ilani ya CCM, tumezoea awamu ya mwisho ya Rais aliye madarakani ni awamu ya wabunge wengi kuanza michakato ya chini kwa chini kutaka kumrithi aliye Madarakani,Mara nyingi michakato hii inafanya Serikali pamoja na Chama kuyumba maana wengi watahujumu ili kutafuta uhalali wao,Ndugu Humprey Polepole anakwenda kuwa jicho la chama kwa wabunge wote ndani ya Bunge la 12.
Itoshe tu kusema Polepole ni katika wajengaji hoja Mahiri kupata kutokea katika ardhi hii ya bara la Africa,Ukimuona Ndugu Humprey Polepole unaona picha mbali sana,utaona uadilifu ndani yake,utaona Uzalendo ndani yake,utaona uwajibikaji kwa maslahi ya Taifa letu,akiwa Mbunge asiye na Jimbo,lakini akiwa Mtendaji ndani ya CCM,kwa maana misingi ya kazi ya idara ya uenezi ni ya kiutendaji pia ni kuwa msemaji wa chama,kwa maana hiyo atafanya kazi za Chama kama majukumu ya muda wote.
Kwenye Chama Mbunge ni cheo na kwa nafasi ya maamuzi yanaishia kamati ya siasa ya wilaya na mkoa. Mbunge haingii Halmashauri Kuu taifa,lakini Ndugu Humprey Polepole kwa fimbo ya Katibu wa itikadi na Uenezi,na Ujumbe wa Halmashauri Kuu,Taifa ataingia kwenye kikao cha Halmashauri Kuu ya CCM na kutoa report ya Bungeni,nani mvivu na Wananchi wa Jimbo lake wanasemaje kuhusu Mbunge huyo,kumbuka Halmashauri kuu ya CCM, Taifa ni chombo cha pili kikubwa kwa maamuzi baada ya Kamati kuu ya CCM,Kwa jicho la kibinafsi na kimaslahi nafasi ya ubunge ni kubwa kuliko Uenezi Taifa kwa maana ubunge unakupa promising future ya kisiasa kitaifa, maana mbunge anaweza kuwa waziri na kuingia kwenye Baraza la mawaziri,hili likitokea kwa Ndugu Humprey Polepole,basi atakwenda kureport ndani ya Baraza la Mawaziri,nini kinatendeka Bungeni,Mbunge gani mzembe na hatua gani zichukuliwe,
Nimalizie kwa kuwapa maono yangu juu ya CCM kuwekeza vilivyo kwa Vijana ambao watakuwa Viongozi makini, Wazalendo,wawajibikaji wenye uchungu wa nchi hii ya Tanzania, na ndio maana tumeona uteuzi wa Ndugu Humprey Polepole, uteuzi wa kuaminika ambapo atakwenda kureport kwa Mheshimiwa Rais John Magufuli moja kwa moja kutoka Bungeni,nini kinafanyika Bungeni,nini Mbunge huyu anafanya,mbona Wananchi wake wa Jimbo mfano la Morogoro wanasema hivi,Ndugu Humprey Polepole atakwenda kuwa msimamizi,kwa kizungu "watchdog" kwa kofia ya Mjumbe wa Halmashauri Kuu na Katibu wa Itikadi na Uenezi,Taifa.
Nikiishia hapa,Mimi ni
Msemakweli Chakubanga,
Dar es Salaam.
0755078854
-Bachelor of Business Administration in International Business
-Master of Leadership and Management.
Recent Publication;
-Assessment on the Effects of Micro-Financing on Poverty Reduction.