LGE2024 Abbas Mtemvu: Wana-CCM ambao hawajateuliwa kura za maoni watulie na kuongeza nguvu kazi kwenye uchaguzi

LGE2024 Abbas Mtemvu: Wana-CCM ambao hawajateuliwa kura za maoni watulie na kuongeza nguvu kazi kwenye uchaguzi

Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024

The Sheriff

JF-Expert Member
Joined
Oct 10, 2019
Posts
747
Reaction score
2,112
Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Dar es Salaam Abas Mtemvu amewataka wanachama wa CCM wasioteuliwa katika kura za maoni kutulia na kuongeza nguvu kazi kwenye uchaguzi.

Mwenyekiti Mtemvu ameyasema hayo katika ziara ya Mlezi wa Chama Cha Mapinduzi na Katibu wa Itikadi, Uenezi na Mafunzo, Amos Makala wilayani Kigamboni.

Amesema wana-CCM wote waungane ili Chama Cha Mapinduzi kishinde katika uchaguzi wa serikali za mitaa ambao ni msingi wa mwaka 2025.

Mwenyekiti Mtemvu amesisitiza wanachama wote ambao majina yao hayajateuliwa wawe na subira na wasihame chama chao kwani CCM ni taasisi kubwa.

SOMA PIA: Matukio ya Mikoa yote Tanzania Bara inayoshiriki katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024

Ameeleza kuwa ushindi wa Chama Cha Mapinduzi unatokana na uimara, umoja na mshikamano kwa viongozi na wanachama.

Akizungumzia juu ya Mwaka 2025 Mtemvu ameendelea kuunga mkono msimamo wa Chama Cha Mapinduzi kwa nafasi ya Urais ni Dokta Samia Suluhu Hassan kwa salamu maarufu ya Samia mitano tena.

Ziara ya Mlezi wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Dar es Salaam Katibu wa Itikadi, Uenezi na Mafunzo Amos Makala inaendelea tena novemba 8 katika wilaya ya temeke kabla ya kuelekea Mkoa wa Pwani kwa siku mbili na kuhitimisha kwa mkutano maalum Mkoani Dar es Salaam.

CCMs-Dar-es-Salaam-Regional-Chairman-Abbas-Mtemvu-.jpeg

Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Dar, Abbas Zeberi Mtemvu (Picha hii si ya tukio linaloelezwa katika taarifa hii)
 
Mijizi na mijitu yenye roho mbaya na mikatili ambayo ipo tayari kufanya chochote ili mradi ipate madaraka tu inatiana moyo!
 
Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Dar es Salaam Abas Mtemvu amewataka wanachama wa CCM wasioteuliwa katika kura za maoni kutulia na kuongeza nguvu kazi kwenye uchaguzi.

Mwenyekiti Mtemvu ameyasema hayo katika ziara ya Mlezi wa Chama Cha Mapinduzi na Katibu wa Itikadi, Uenezi na Mafunzo, Amos Makala wilayani Kigamboni.

Amesema wana-CCM wote waungane ili Chama Cha Mapinduzi kishinde katika uchaguzi wa serikali za mitaa ambao ni msingi wa mwaka 2025.

Mwenyekiti Mtemvu amesisitiza wanachama wote ambao majina yao hayajateuliwa wawe na subira na wasihame chama chao kwani CCM ni taasisi kubwa.

SOMA PIA: Matukio ya Mikoa yote Tanzania Bara inayoshiriki katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024

Ameeleza kuwa ushindi wa Chama Cha Mapinduzi unatokana na uimara, umoja na mshikamano kwa viongozi na wanachama.

Akizungumzia juu ya Mwaka 2025 Mtemvu ameendelea kuunga mkono msimamo wa Chama Cha Mapinduzi kwa nafasi ya Urais ni Dokta Samia Suluhu Hassan kwa salamu maarufu ya Samia mitano tena.

Ziara ya Mlezi wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Dar es Salaam Katibu wa Itikadi, Uenezi na Mafunzo Amos Makala inaendelea tena novemba 8 katika wilaya ya temeke kabla ya kuelekea Mkoa wa Pwani kwa siku mbili na kuhitimisha kwa mkutano maalum Mkoani Dar es Salaam.

View attachment 3149460
Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Dar, Abbas Zeberi Mtemvu (Picha hii si ya tukio linaloelezwa katika taarifa hii)
Huyu jamaa ndiye aliyezunguka kwenye vyama kibao kama marehemu Hiza Tambwe?
 
Mijizi na mijitu yenye roho mbaya na mikatili ambayo ipo tayari kufanya chochote ili mradi ipate madaraka tu inatiana moyo!
Nasema hivii,wanaccm wote mk
liofanyiwa rough,mliodhulumiwa kwa matumizi ya fweza,Mliokatwa majina isivyo halali,hameni ili wajue mchezo wao nyumbani kwenu na kwa mahirani zenu hamuupendi na mmeukataa.Kumbujeni ccm siyo baba yenu wala mama yenu.Chukueni hatua kunusuru chama chenu mlichokipenda awali na linusuruni taifa lenu,linusuruni taifa letu.Ilindeni japo chambe ya kinachoitwa demokrasili kilichosali.Mtakuja kuyakumbuka yote haya pindi pamekucha.Ni hayo tu.
 
Back
Top Bottom