Viol
JF-Expert Member
- Dec 15, 2009
- 25,420
- 18,298
Abdallah Bitembo ni mchezaji aliyeichezea timu ya CRDB FC Arudha ilipokuwa daraja la kwanza na hatimaye Meru FC,alicheza ligi enzi kukiwa na timu 16 kwenye ligi kuu,anaelezea kwamba hakuweza kwenda kucheza simba au Yanga maana kule kulikuwa na vipaji vikubwa wakati huo kama kina Lunyamila.
Anaelezea mpira haukumpa maisha mazuri hivyo aliamua kwenda kufanya kazi kwenye saloon ya kaka yake dar ,wakati huo mashine za kunyoa hazitoka ,na wateja wake wengi walikuwa wachezaji kwa sababu alikuwa anawanyoa walipokuwa kwenye ligi na hivo akafungua saloon yake mwenyewe "BITEKO SALOON".
Kwa sababu saloon yake ilijulikana kwa wachezaji basi aliweza kupata wateja ambao ni masters wa bongo kama kina Alichoki,Nyoshi El Sadat na pia walimrusha kwenye nyimbo zao na kujulikana zaidi.
Kwa wasanii waigizaji msanii wa ambaye ni mteja wake wa kudumu ni Vicent Kigosi ,kigosi akamleta kanumba na sasa hivi wasanii wengi wa bongo fleva wananyoa kwakwe.Pia alimnyoa Koffi Olomide alipokuja bongo.
Kwenye miaka ya 2000 mwanzoni alipelekwa Dubai na mchezaji wa Coastal Union ambaye ana asili ya kiarabu ,alienda kunyoa Saudi Arabia kwa mkataba wa miaka 3 na kusomea mambo ya urembo wa nywele (certificate).
Kwa sababu enzi hizo Geogre Weah alikuwa anacheza Abu Dhabi na kati ya saloon za kiafrica saloon aliyokuwa anafanyia kazi ilikuwa na jina basi alikuwa anamyoa George Weah ambaye kwa sasa ni Rais wa Liberia.
Anaelezea mpira haukumpa maisha mazuri hivyo aliamua kwenda kufanya kazi kwenye saloon ya kaka yake dar ,wakati huo mashine za kunyoa hazitoka ,na wateja wake wengi walikuwa wachezaji kwa sababu alikuwa anawanyoa walipokuwa kwenye ligi na hivo akafungua saloon yake mwenyewe "BITEKO SALOON".
Kwa sababu saloon yake ilijulikana kwa wachezaji basi aliweza kupata wateja ambao ni masters wa bongo kama kina Alichoki,Nyoshi El Sadat na pia walimrusha kwenye nyimbo zao na kujulikana zaidi.
Kwa wasanii waigizaji msanii wa ambaye ni mteja wake wa kudumu ni Vicent Kigosi ,kigosi akamleta kanumba na sasa hivi wasanii wengi wa bongo fleva wananyoa kwakwe.Pia alimnyoa Koffi Olomide alipokuja bongo.
Kwenye miaka ya 2000 mwanzoni alipelekwa Dubai na mchezaji wa Coastal Union ambaye ana asili ya kiarabu ,alienda kunyoa Saudi Arabia kwa mkataba wa miaka 3 na kusomea mambo ya urembo wa nywele (certificate).
Kwa sababu enzi hizo Geogre Weah alikuwa anacheza Abu Dhabi na kati ya saloon za kiafrica saloon aliyokuwa anafanyia kazi ilikuwa na jina basi alikuwa anamyoa George Weah ambaye kwa sasa ni Rais wa Liberia.