Abdallah Tambaza na Mohamed Said pamoja nusu karne na Kumbukumbu ya Shama

Abdallah Tambaza na Mohamed Said pamoja nusu karne na Kumbukumbu ya Shama

Mohamed Said

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2008
Posts
21,967
Reaction score
32,074
ABDALLAH TAMBAZA NA MOHAMED SAID PAMOJA NUSU KARNE NA KUMBUKUMBU YA SHAMA

Alhamdulilah.

Picha ya kwanza kushoto ni Abdallah Tambaza na huyo mwingine ni mimi.

Hapo ni Jamhuri Park Nairobi katika All Africa Trade Fair mwaka wa 1972.

Nilikuwa na miaka 20 na Abdallah 22.

Hiyo picha ya pili kushoto ni Abdallah Tambaza tena na huyo mwingine ni Mohamed Said.

Picha hii katupiga mdogo wetu Ghose Makaburi ya Kisutu majuma machache yaliyopita tulipokwenda kwenye maziko ya mwenzetu Bi. Shama tuliokua sote Kariakoo toka udogo wetu na tukawa pamoja siku zote hadi alipotangulia mbele ya haki majuma machache yaliyopita.

Nataka nisema kitu kifupi.

Wakati mimi na Abdallah tunaagana pale makaburini akanieleza wema ambao Shama alimfanyia.

Mimi nimekaa kimya namsikiliza lakini naomba dua kimoyomoyo Allah amlipe ndugu yetu i. Shama kwa mema yake na amtie katika pepo ya Firdaus.

Ilikuwa kila Ijumaa baadhi yetu tukitoka msikitini hasa ikiwa tumesali Msikiti wa Maamur ambao ni jirani na nyumbani kwake tunapita nyumbani kwa Shama tunakwenda pale kula pilau.

Huu ndiyo ulikuwa uradi wa Bi. Shama.

Hii ni kila Ijumaa.

Na kwa hakika ilikuwa nafasi nzuri sana kwetu sisi tuliokuwa sote Dar es es Salaam hii kukutana na kuzungumza.

Bi. Shama masikini ukimkuta pale Mansfield kwenye duka lake la ice cream jua kali ukasema hebu niingie kivulini hapa nimsalimu Shama na nile ice cream nipoze joto...

Ukisha poza roho hataki ulipe inakuwa zogo wewe unashikilia lazima ulipe na yeye hataki kupokea hela zako.

Wateja wengine wanashangaa, kulikoni?

Sasa fikiria umekwenda na kaumu yako yote siku ya sikukuu kuwanunulia watoto ice cream.

Watoto wakiona ice cream mzuka unapanda macho yote yako ukutani zilipowekwa picha za kutamanisha za ice cream.

Umma unapiga order za fujo watoto wamefurahi.
Wamekula ice cream kefu yao sasa unakwenda kulipa.

Shama anakataa kupokea fedha.

Kisa ati siku nyingi hamjaonana na kuwa ice cream wamekula wanae.

Mama Abdul (anajijua) katika hali kama hii baada ya kuvutana kwa muda mrefu akamwambia, ''Shama unanifukuza dukani kwako.''

Shama wala hamsikilizi yeye anatabasamu tu na cash register haifungui.

Hawa watoto hivi sasa na mababa na mama na naamini bado wanakwenda Mansfield na watoto wao (leo ni wajukuu zetu) kula ice cream kwenye duka la Shama.

Hawa wanetu baadhi yao ni baba na mama zao wametangulia mbele ya haki na najizuia kutaja majina kuchelea kuwaliza ndugu zangu.

Lakini kwa kuwa wao ni sehemu ya historia hii wanajua nimewakusudia nani na nani.

Tunamuomba mola wetu mtukufu awarehemu hawa ndugu zetu wote waliotangulia awaghufurie madhambi yao na sisi tunaosubiri atupe mwisho mwema.

Sasa huyu mdogo wetu Ghose aliyetupiga picha hii ni mmoja wa wadogo zetu aliyekulia mitaa ya Kariakoo yeye na ndugu zake na ni watu mashuhuri.

Najiuliza sijui nini kilimpata akatupiga picha hii na usiku siku ile ile akanirushia.

Mashaallah ana mkono mzuri wa kupiga picha.

Screenshot_20210821-142538_Facebook.jpg
 
Familia ya Tambaza inajulikana sana Upanga, nilikulia Upanga miaka ya late 80s to late 90s

Pia nilisoma madrasa ya Tambaza miaka hiyo wakati wa Maalim Ayeyo, tulikuwa na kina Jumbe Tambaza, Ali Tambaza, Msakala na wengineo wengi.

Sijui sasa wako wapi maana ni muda sana, huwezi kuishi Upanga miaka hiyo bila kuwajua familia ya Tambaza
 
Familia ya Tambaza inajulikana sana Upanga, nilikulia Upanga miaka ya late 80s to late 90s

Pia nilisoma madrasa ya Tambaza miaka hiyo wakati wa Maalim Ayeyo, tulikuwa na kina Jumbe Tambaza, Ali Tambaza, Msakala na wengineo wengi.

Sijui sasa wako wapi maana ni muda sana, huwezi kuishi Upanga miaka hiyo bila kuwajua familia ya Tambaza
Tekno...
Msakala nilikwenda kumuona nyumbani kwake Kinondoni nikiongozana na Abdallah Tambaza ambae yeye ni kaka yake.

Katika zawadi alizonipa siku hiyo ni hii picha ya Baraza la Wazee wa TANU hapo chini:

Screenshot_20210822-044117_Chrome.jpg


Angalia tarehe ya picha.

Haraka nikaipandisha kwenye mtandao ishuhudiwe na dunia nzima.

Watu wa kwanza kuwaonyesha walikuwa wanabarza wa JF.

Picha hii iliwashtua wengi.
Picha hii ilileta mjadala mkali.

Picha hii katika kubwa iliyoleta ni kuwa ilizima na kumaliza ubishi.

Msakala amehifadhi nyaraka kadhaa za babu yake Mzee Jumbe Tambaza.

Alishangaa sana nilipomweleza kuwa mimi nilifahamiana vizuri sana na baba yake Mohamed Tambaza toka Kinondoni katika miaka ya 1970s na tukisali sote Msikiti wa Mtambani ule wa zamani Imam Mkuu Sheikh Mwagavumbi na Muadhini Mzee Hassan.

Rafiki wa baba zake pale Kinondoni walikuwa Mussa Majungu, Mzee Momba, Daraja kwa kuwataja wachache.

Nilimsihi sana kuzitunza nyaraka zile mahali bora zaidi.

Alinieleza mengi sana ya kusikitisha.

Kama alivyokuwa babu yake mwanachama shupavu wa TANU, Msakala ni mstari wa mbele CCM na ni mmoja kwa ajili ya ujana wake tulipoonana akitumiwa sana na chama hicho kama muhamasishaji na mlinzi wa viongozi wakati wa uchaguzi.

Hili lilinirudisha nyuma na mbali wakati wa Bantu Group.

Lakini kwa bahati mbaya Msakala hakuwa anajua mengi katika maisha ya siasa ya babu yake Mzee Tambaza.

Anachokijua ni kuwa babu yake alimsaidia sana Julius Nyerere kukubalika na wenyeji wa Dar-es-Salaam ile ya miaka ya 1950.

Sasa miaka hiyo uliyotaja ya 1980s mimi nikiishi Kitalu ndani ya Muhimbili na nikija kusali Msikiti wa Tambaza imam alikuwa Sheikh mmoja kutoka Pemba.

Hapo msikitini ndipo nilipomfahamu Jumbe Tambaza kwa karibu.

Mtu mpole na mkimya sana husikii hata sauti yake.

Hicho chuo ulichosoma miaka hiyo nakikumbuka sana.

Nashukuru kuwa ule msikiti wa zamani umevunjwa na mahali pake leo umesimama msikiti mkubwa wa kisasa.
 
Tekno...
Msakala nilikwenda kumuona nyumbani kwake Kinondoni nikiongozana na Abdallah Tambaza ambae yeye ni kaka yake.

Katika zawadi alizonipa siku hiyo ni hii picha ya Baraza la Wazee wa TANU hapo chini:

View attachment 1902389

Angalia tarehe ya picha.

Haraka nikaipandisha kwenye mtandao ishuhudiwe na dunia nzima.

Watu wa kwanza kuwaonyesha walikuwa wanabarza wa JF.

Picha hii iliwashtua wengi.
Picha hii ilileta mjadala mkali.

Picha hii katika kubwa iliyoleta ni kuwa ilizima na kumaliza ubishi.

Msakala amehifadhi nyaraka kadhaa za babu yake Mzee Jumbe Tambaza.

Alishangaa sana nilipomweleza kuwa mimi nilifahamiana vizuri sana na baba yake Mohamed Tambaza toka Kinondoni katika miaka ya 1970s na tukisali sote Msikiti wa Mtambani ule wa zamani Imam Mkuu Sheikh Mwagavumbi na Muadhini Mzee Hassan.

Rafiki wa baba zake pale Kinondoni walikuwa Mussa Majungu, Mzee Momba, Daraja kwa kuwataja wachache.

Nilimsihi sana kuzitunza nyaraka zile mahali bora zaidi.

Alinieleza mengi sana ya kusikitisha.

Kama alivyokuwa babu yake mwanachama shupavu wa TANU, Msakala ni mstari wa mbele CCM na ni mmoja kwa ajili ya ujana wake tulipoonana akitumiwa sana na chama hicho kama muhamasishaji na mlinzi wa viongozi wakati wa uchaguzi.

Hili lilinirudisha nyuma na mbali wakati wa Bantu Group.

Lakini kwa bahati mbaya Msakala hakuwa anajua mengi katika maisha ya siasa ya babu yake Mzee Tambaza.

Anachokijua ni kuwa babu yake alimsaidia sana Julius Nyerere kukubalika na wenyeji wa Dar-es-Salaam ile ya miaka ya 1950.

Sasa miaka hiyo uliyotaja ya 1980s mimi nikiishi Kitalu ndani ya Muhimbili na nikija kusali Msikiti wa Tambaza imam alikuwa Sheikh mmoja kutoka Pemba.

Hapo msikitini ndipo nilipomfahamu Jumbe Tambaza kwa karibu.

Mtu mpole na mkimya sana husikii hata sauti yake.

Hicho chuo ulichosoma miaka hiyo nakikumbuka sana.

Nashukuru kuwa ule msikiti wa zamani umevunjwa na mahali pake leo umesimama msikiti mkubwa wa kisasa.
Mzee MS
Kwa nini Msakala hakuwa anajua mengi kuhusu Babu yake?
 
Mzee MS
Kwa nini Msakala hakuwa anajua mengi kuhusu Babu yake?
Plato...
Hili si kwa Msakala peke yake.

Nimekutana na wengi kutoka koo za waliopigania uhuru wa Tanganyika nawauliza vitu wanasema hawajui.

Nadhani sababu kubwa ni huku kufuta historia ya kweli ikapachikwa historia hii rasmi.
Kumbe tuna baba zetu hapa jukwaani!
Mzee Mohamed Said (1952).lTO
 
Isela...
Ulinidhania mimi ni kijana?
Mimi ni mzee In Shaa Allah nikijaaliwa kuiona February 2022 nitakuwa na miaka 70.

Huwa nasikitika sana humu vijana wadogo wanaponivunjia heshima.
tumezaliwa mwezi mmoja wewe ni babu yangu ama baba yangu mkubwa maana mimi 90+ ndio nimeliwa mwezi february 7...
 
Ndugu Mohamed Said

Je kuna uhusiano wowote wa jina la shule Tambaza Sekondari na hii familia ya Tambaza?

Tupe historia yake tafadhari.

Ahsante
 
Mkuu,naona mnafanana utafikiri ni ndugu.

Hamna mahusiano yoyote yale?
 
Mwl.
Uhusiano ni kuwa shule imepewa jina la Mzee Tambaza kwa kuheshimu mchango wake katika uhuru wa Tanganyika.

Shule hiyo zamani ikiitwa HH Aga Khan.
Na baadaye, Mzizima Sec ilipewa jina hili la HH Aga Khan, au?
 
Isela...
Ulinidhania mimi ni kijana?
Mimi ni mzee In Shaa Allah nikijaaliwa kuiona February 2022 nitakuwa na miaka 70.

Huwa nasikitika sana humu vijana wadogo wanaponivunjia heshima.
Pole sana Mzee Mohamed!
Heshima kwako maana wewe na Bi Mkubwa wangu mmepishana miaka miwili tu; yeye kazaliwa 1950.
 
Pole sana Mzee Mohamed!
Heshima kwako maana wewe na Bi Mkubwa wangu mmepishana miaka miwili tu; yeye kazaliwa 1950.
Ise...
Ikiwa Bi Mkubwa ni wa Dar-es-Salaam huenda nikamfahamu.

Mji ulikuwa mdogo na rika moja.
 
Baada ya shule ya Aga Khan kutaifishwa na serikali ndipo Aga Khan wakajenga Shule ya Mzizima.

Mzee Said...
Sio kwamba mimi nilidhani lile eneo lote lilikuwa ni shamba linamilikiwa na familia ya Tambaza na wakajitolea kwa serikali kujenga shule?
 
Back
Top Bottom