Abdu Fatah Mussa Mtangazaji wa Radio Tehran Iran

Abdu Fatah Mussa Mtangazaji wa Radio Tehran Iran

Mohamed Said

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2008
Posts
21,967
Reaction score
32,074
ABDU FATAH MUSSA MTANGAZAJI WA RADIO TEHRAN IRAN

Ulikuwa mwaka wa 2000 Uchaguzi Mkuu wa Pili baada ya uchaguzi wa kwanza 1995.

Niko Tanga.

Sikumbuki vipi tulifahamiana lakini ninachokumbuka ni kuwa siku moja wakati wa kampeni za uchaguzi zikiendelea alinipigia simu akaitambulisha Sauti ya Iran na yeye mwenyewe kuniomba anihoji kuhusu siasa za Tanzania.

Huu ukawa ndiyo mwanzo wa usuhuba wetu.

Ikawa mara kwa mara ananipigia simu tunafanya mahojiano na mazungumzo yetu yanarushwa na Radio Tehran Iran.

Mimi sikujua.

Nilikuja kujua baadae sana kuwa namna yangu ya kueleza matokeo ya siasa na historia ya Tanzania ilikuwa tofauti sana na namna wengine walivyokuwa wanaeleza.

Radio Tehran Idhaa ya Kiswahili inasikilizwa Arabuni ambako kuna wasemaji Kiswahili wengi.

Sasa baada ya mimi kuwa mmoja wa wachambuzi wa siasa kutoka Tanzania vipindi hivi nilivyokuwa nikifanya na Abdul Fatah vikavutia wasikilizaji wengi.

Radio Tehran Idhaa ya Kiswahili ikapanda chati ikawa iko juu.

Radio nyingine mashuhuri wasikilizaji watasikiliza lakini mwisho watafungua Radio Tehran kusikiliza na wao wana lipi kuhusu taarifa hiyo.

Abdul Fatah ni mtangazaji hodari Mashaallah anayejua kuhoji yale ambayo wewe muhojiwa hukutegemea.

Atakuchukua ngazi baada ya ngazi mnapanda na kila kidato kinazua kisa kipya.

Abdu Fatah anakuwa mwanamasumbwi anaemperemba mpinzani wake amtwange sumbwi litakalomwangusha chini na kumaliza pambano.

Wako wanaoghadhibishwa na maswali chokonozi kipindi kikawaka moto muhojiwa akamaliza hasira zake kwa mtangazaji wakaagana.

Hicho ndicho mtangazaji alichokuwa akikitafuta na kakipata bure kabisa.

Akizima digital yake na kuvua headphones anaangua kicheko cha furaha.

Kapata kipindi burudani kwa wasikilizaji wake.

Milton Obote alimfokea mtangazaji wa BBC na akawakomesha wasimpigie simu tena kumletea upuuzi wao.

Siku hizo mwisho wa uhai wake yuko Zimbabwe.
Abdu Fatah akiniwekea staha lakini akiniangushia makombora mazito.

Miaka ya mwanzo ya vyama vingi toka kurejeshwa siasa za vyama vingi zilikuwa moto hasa Zanzibar.

Uchaguzi wa 1995 CCM Zanzibar ilikuwa imeshindwa uchaguzi na waandishi wengi wakihofu kulieleza hili.

Abdu Fatah ataniperemba kwa upole kabisa kunilainisha tuangalie hali ya baadae ya visiwani.

"Sikiliza Abdu mimi panya sifunzwi kula sufi..."

Atacheka.
Nazungumza na Mswahili tena Mzanzibari.

Keshanifahamu.
Ikawa Radio Tehran inapendeza.

Nilipata mshtuko nilipokutana na Abdu Fatah Tehran akaniambia kuwa yeye shahada yake ni ya Uhandisi.

Huyu ndiye Injinia Abdu Fatah Mussa wa Idhaa ya Kiswahili Radio Iran Tehran.

1717516989694.jpeg

Abdu Fatah Mussa​
1717516873775.jpeg

 
ABDU FATAH MUSSA MTANGAZAJI WA RADIO TEHRAN IRAN

Ulikuwa mwaka wa 2000 Uchaguzi Mkuu wa Pili baada ya uchaguzi wa kwanza 1995.

Niko Tanga.

Sikumbuki vipi tulifahamiana lakini ninachokumbuka ni kuwa siku moja wakati wa kampeni za uchaguzi zikiendelea alinipigia simu akaitambulisha Sauti ya Iran na yeye mwenyewe kuniomba anihoji kuhusu siasa za Tanzania.

Huu ukawa ndiyo mwanzo wa usuhuba wetu.

Ikawa mara kwa mara ananipigia simu tunafanya mahojiano na mazungumzo yetu yanarushwa na Radio Tehran Iran.

Mimi sikujua.

Nilikuja kujua baadae sana kuwa namna yangu ya kueleza matokeo ya siasa na historia ya Tanzania ilikuwa tofauti sana na namna wengine walivyokuwa wanaeleza.

Radio Tehran Idhaa ya Kiswahili inasikilizwa Arabuni ambako kuna wasemaji Kiswahili wengi.

Sasa baada ya mimi kuwa mmoja wa wachambuzi wa siasa kutoka Tanzania vipindi hivi nilivyokuwa nikifanya na Abdul Fatah vikavutia wasikilizaji wengi.

Radio Tehran Idhaa ya Kiswahili ikapanda chati ikawa iko juu.

Radio nyingine mashuhuri wasikilizaji watasikiliza lakini mwisho watafungua Radio Tehran kusikiliza na wao wana lipi kuhusu taarifa hiyo.

Abdul Fatah ni mtangazaji hodari Mashaallah anayejua kuhoji yale ambayo wewe muhojiwa hukutegemea.

Atakuchukua ngazi baada ya ngazi mnapanda na kila kidato kinazua kisa kipya.

Abdu Fatah anakuwa mwanamasumbwi anaemperemba mpinzani wake amtwange sumbwi litakalomwangusha chini na kumaliza pambano.

Wako wanaoghadhibishwa na maswali chokonozi kipindi kikawaka moto muhojiwa akamaliza hasira zake kwa mtangazaji wakaagana.

Hicho ndicho mtangazaji alichokuwa akikitafuta na kakipata bure kabisa.

Akizima digital yake na kuvua headphones anaangua kicheko cha furaha.

Kapata kipindi burudani kwa wasikilizaji wake.

Milton Obote alimfokea mtangazaji wa BBC na akawakomesha wasimpigie simu tena kumletea upuuzi wao.

Siku hizo mwisho wa uhai wake yuko Zimbabwe.
Abdu Fatah akiniwekea staha lakini akiniangushia makombora mazito.

Miaka ya mwanzo ya vyama vingi toka kurejeshwa siasa za vyama vingi zilikuwa moto hasa Zanzibar.

Uchaguzi wa 1995 CCM Zanzibar ilikuwa imeshindwa uchaguzi na waandishi wengi wakihofu kulieleza hili.

Abdu Fatah ataniperemba kwa upole kabisa kunilainisha tuangalie hali ya baadae ya visiwani.

"Sikiliza Abdu mimi panya sifunzwi kula sufi..."

Atacheka.
Nazungumza na Mswahili tena Mzanzibari.

Keshanifahamu.
Ikawa Radio Tehran inapendeza.

Nilipata mshtuko nilipokutana na Abdu Fatah Tehran akaniambia kuwa yeye shahada yake ni ya Uhandisi.

Huyu ndiye Injinia Abdu Fatah Mussa wa Idhaa ya Kiswahili Radio Iran Tehran.

View attachment 3008452
Abdu Fatah Mussa​
View attachment 3008451
Mungu ni mwenyezi
 
Mzee said angekuwa sio mdini angekuwa mtu wa kuigwa na jamii,lakini udini umemwelemea mzee wa watu mpaka hata maandiko yake ni udini mtupu.
Sam...
Unaitisha nafsi yako bila sababu.
Unaona tabu kusoma historia ambayo imejaa majina ya Kiislam.

Hakuna lingine.

Ingekuwa mimi natangaza Uislam nisingeadhimishwa hapa JF mara mbili kama Mwandishi Bora.

Nisingealikwa kwenye vyuo maarufu Marekani na Ulaya.

Nisingealikwa kuzungumza VoA, BBC, DW, SABC, TBC, ITV, AZAM na vituo vingi vingine.
 
Sam...
Unaitisha nafsi yako bila sababu.
Unaona tabu kusoma historia ambayo imejaa majina ya Kiislam.

Hakuna lingine.

Ingekuwa mimi natangaza Uislam nisingeadhimishwa hapa JF mara mbili kama Mwandishi Bora.

Nisingealikwa kwenye vyuo maarufu Marekani na Ulaya.

Nisingealikwa kuzungumza VoA, BBC, DW, SABC, TBC, ITV, AZAM na vituo vingi vingine.
Mohamed Said mimi ni moja ya wasomaji wakala zako,iko hivi wewe ni mwandishi mzuri sana na mahiri lakini historia unayoandika umeifinya kwa makusudi ili kuutweza upande fulani,hilo lipo wazi.
 
Leo naona,dully skyes,nyerere na historia mpya tanganyika vimepumzishwa,ila hujasahau kujisifu na kujigamba kwamba wazungu wanakukubali,mzee unapenda kujisifia sana kumbe ni🚮
 
ABDU FATAH MUSSA MTANGAZAJI WA RADIO TEHRAN IRAN

Ulikuwa mwaka wa 2000 Uchaguzi Mkuu wa Pili baada ya uchaguzi wa kwanza 1995.

Niko Tanga.

Sikumbuki vipi tulifahamiana lakini ninachokumbuka ni kuwa siku moja wakati wa kampeni za uchaguzi zikiendelea alinipigia simu akaitambulisha Sauti ya Iran na yeye mwenyewe kuniomba anihoji kuhusu siasa za Tanzania.

Huu ukawa ndiyo mwanzo wa usuhuba wetu.

Ikawa mara kwa mara ananipigia simu tunafanya mahojiano na mazungumzo yetu yanarushwa na Radio Tehran Iran.

Mimi sikujua.

Nilikuja kujua baadae sana kuwa namna yangu ya kueleza matokeo ya siasa na historia ya Tanzania ilikuwa tofauti sana na namna wengine walivyokuwa wanaeleza.

Radio Tehran Idhaa ya Kiswahili inasikilizwa Arabuni ambako kuna wasemaji Kiswahili wengi.

Sasa baada ya mimi kuwa mmoja wa wachambuzi wa siasa kutoka Tanzania vipindi hivi nilivyokuwa nikifanya na Abdul Fatah vikavutia wasikilizaji wengi.

Radio Tehran Idhaa ya Kiswahili ikapanda chati ikawa iko juu.

Radio nyingine mashuhuri wasikilizaji watasikiliza lakini mwisho watafungua Radio Tehran kusikiliza na wao wana lipi kuhusu taarifa hiyo.

Abdul Fatah ni mtangazaji hodari Mashaallah anayejua kuhoji yale ambayo wewe muhojiwa hukutegemea.

Atakuchukua ngazi baada ya ngazi mnapanda na kila kidato kinazua kisa kipya.

Abdu Fatah anakuwa mwanamasumbwi anaemperemba mpinzani wake amtwange sumbwi litakalomwangusha chini na kumaliza pambano.

Wako wanaoghadhibishwa na maswali chokonozi kipindi kikawaka moto muhojiwa akamaliza hasira zake kwa mtangazaji wakaagana.

Hicho ndicho mtangazaji alichokuwa akikitafuta na kakipata bure kabisa.

Akizima digital yake na kuvua headphones anaangua kicheko cha furaha.

Kapata kipindi burudani kwa wasikilizaji wake.

Milton Obote alimfokea mtangazaji wa BBC na akawakomesha wasimpigie simu tena kumletea upuuzi wao.

Siku hizo mwisho wa uhai wake yuko Zimbabwe.
Abdu Fatah akiniwekea staha lakini akiniangushia makombora mazito.

Miaka ya mwanzo ya vyama vingi toka kurejeshwa siasa za vyama vingi zilikuwa moto hasa Zanzibar.

Uchaguzi wa 1995 CCM Zanzibar ilikuwa imeshindwa uchaguzi na waandishi wengi wakihofu kulieleza hili.

Abdu Fatah ataniperemba kwa upole kabisa kunilainisha tuangalie hali ya baadae ya visiwani.

"Sikiliza Abdu mimi panya sifunzwi kula sufi..."

Atacheka.
Nazungumza na Mswahili tena Mzanzibari.

Keshanifahamu.
Ikawa Radio Tehran inapendeza.

Nilipata mshtuko nilipokutana na Abdu Fatah Tehran akaniambia kuwa yeye shahada yake ni ya Uhandisi.

Huyu ndiye Injinia Abdu Fatah Mussa wa Idhaa ya Kiswahili Radio Iran Tehran.

View attachment 3008452
Abdu Fatah Mussa​
View attachment 3008451
Jee yupo hai.
 
Mzee said angekuwa sio mdini angekuwa mtu wa kuigwa na jamii,lakini udini umemwelemea mzee wa watu mpaka hata maandiko yake ni udini mtupu.
Sam...
Unaitisha nafsi yako bila sababu.
Unaona tabu kusoma historia ambayo imejaa majina ya Kiislam.

Hakuna lingine.

Ingekuwa mimi natangaza Uislam nisingeadhimishwa hapa JF mara mbili kama Mwandishi Bora.
 
Mohamed Said mimi ni moja ya wasomaji wakala zako,iko hivi wewe ni mwandishi mzuri sana na mahiri lakini historia unayoandika umeifinya kwa makusudi ili kuutweza upande fulani,hilo lipo wazi.
Sam...
Vipi historia zilioandikwa kabla ya mimi kunyanyua kalamu.

Unalo lolote la kusema?
 
Nakushauri wewe kama miongoni mwa waandishi nguli niliowahi wafuatilia uweke uweredi mbele na kutovutwa na udini,ni hayo tu.
Sam...
Nakueleza kuwa ingekuwa mimi naandika Uislam Dini nisingekuwa ndani ya Dictionary of African Biography (DAB) nikiwa mmoja wa waandishi 500 walioandika kamusi hilo la volume 6 mradi wa Harvard na Oxford University Press, New York.

Nisingepata nafasi ya kitabu changu kuwa ndani ya Cambridge Journal of African History.

Nisingealikwa Northwestern University, Chicago kuzungumza na vyuo vingine vingi ndani na nje ya mipaka yetu.

Ni hayo tu.
1717526220832.png

1717526309671.jpeg

Northwestern University, Evanston Chicago​
 
Back
Top Bottom