Abdulkarim Hajj Mussa Jamadar mwenyeji wa Mwalimu Julius Nyerere Kilwa Mtoni wakati wa kupigania Uhuru wa Tanganyika

Abdulkarim Hajj Mussa Jamadar mwenyeji wa Mwalimu Julius Nyerere Kilwa Mtoni wakati wa kupigania Uhuru wa Tanganyika

Mohamed Said

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2008
Posts
21,967
Reaction score
32,074
Mjukuu wa Abdulkarim Hajj Mussa Jamadar amesoma historia ya TANU jinsi
ilivyoingia Jimbo la Kusini (Southern Province) kupitia juhudi za wazalendo kama
Suleiman Masudi Mnonji, Yusuf Chembera, Salum Mpunga na Bi. Shariffa bint
Mzee kwa kuwataja wachache.

Hii ikagonga fikra yake mara moja akaniandikia kunifahamisha kuwa na yeye ana
historia ya babu yake Abdulkarim Hajj Mussa Jamadar mmoja kati ya wazalendo
wa mwanzo kumuunga mkono Mwalimu Nyerere na kusaidia kuiingiza TANU Kilwa
Mtoni na akaniahidi kuniletea picha ya nyumba ambayo Mwalimu Nyerere alikuwa
akifikia kila alipokwenda Kilwa na picha ya pikipiki ambayo babu yake alikuwa
akimpakia Nyerere wakisafiri kwenda kijiji hadi kijiji kuwahamasisha wananchi waingie
TANU kupigania uhuru wa nchi yao.

Haukupita muda Abdulkarim akanitumia picha ya pikipiki ya babu yake ambayo ndiyo
ulikuwa usafiri wao yeye na Nyerere kuvifikia vijiji vya jirani wakati wa kueneza TANU.

Pamoja na picha ya pikipiki akaniletea na picha ya nyumba ya babu yake ambayo
Mwalimu Nyerere alikuwa akifikia na vilevile picha ya nyumba ya Mwinyi Mcheni Omari
ambayo ndipo ikifanyika mikutano ya ndani ya TANU,

Nimemsihi Abdulkarim awasiliane na Makumbusho ya Taifa ili pikipiki hii iwekwe pale kwa
ajili ya kumbukumbu ya Baba wa Taifa katika harakati zake za kudai uhuru.

Hii pikipiki ilihamishwa na mtoto wa Mzee Abdulkarim, Mohamed Abdulkarim na kupelekwa
Mafia Kilindoni.
 

Attachments

  • PIKIPIKI BSA 500 YA JEMDARI 1.jpg
    PIKIPIKI BSA 500 YA JEMDARI 1.jpg
    79.5 KB · Views: 79
  • NYUMBA YA ABDULKARIM HAJJ JAMADAR.jpg
    NYUMBA YA ABDULKARIM HAJJ JAMADAR.jpg
    10.1 KB · Views: 86
Another classic lesson. Shukrani Mzee wangu
 
Mzee Mohameid , Asante sana kwa kumbukizi Jadidi, kama si mujarabu.
 
Classic lesson nimepnda sana maelwzo juu hassan taratibu kule Facebook pia juu ya Sharif abdalla atis.. Zaid mjukuu wake alivyokuwa anachagiza kwenye mjadala ule
 
Hivi Uhuru ulipiganiwa na waislam tu, na Wakristo hawakufanya juhudi zozote kwa Uhuru wa nchi hii? Kama Wakristo walifanya juhudi mbona huwa huziandiki? Naomba jawabu Mzee wangu Mohamed Said, Msomi na mchambuziwa Historia Tanzania
 
Hivi Uhuru ulipiganiwa na waislam tu, na Wakristo hawakufanya juhudi zozote kwa Uhuru wa nchi hii? Kama Wakristo walifanya juhudi mbona huwa huziandiki? Naomba jawabu Mzee wangu Mohamed Said, Msomi na mchambuziwa Historia Tanzania
Nazjaz,
Mwaka wa 1953 Abdul Sykes akifuatana na Ali Mwinyi Tambwe alikwenda
Nansio, Ukerewe kwenda kupata kauli ya mwisho kuhusu Abdul kumpisha
uongozi wa TAA Nyerere ili katika uchaguzi wa 1953 Nyerere ashike nafasi
ya urais wa TAA na 1954 waunde TANU.

Mwapachu alimwambia Abdul kuwa yeye mtu anaemuona anafaa kuongoza
harakati za kudai uhuru ni Nyerere kwa hiyo Abdul amsaidie Nyerere ashike
kiti kile.

Kulikuwa na sababu nyingine za Hamza kumtaka Nyerere katika nafasi ile ya
juu kabisa lakini alilomwambia Abdul ni kuwa Nyerere atafaa sana kwa kuwa
yeye ni Mkristo ikiwa watakwenda kuunda TANU 1954 na Abdul ndiye rais
harakati zile zitaonekana ni za Waislam na hii itavuruga mipango yao yote kwa
Waingereza kufanya propaganda kuwa harakati za uhuru ni vurugu za Waislam.

Kabla ya kuja Nyerere kulikuwa na mazungumzo kati ya Abdul Sykes na Chief
Kidaha
kutaka Chief Kidaha ajiunge na TAA wamchague kuwa Rais na kisha
waunde TANU chnii ya uongozi wa Chief Kidaha Makwaia wa Shiyanga.

Hili halikufanikwa.

Ikutoshe tu kuwa huyo Ali Mwinyi Tambwe alikuwa ndiye Katibu wa Al Jamiatul
Islamiyya fi Tanganyika, yaani Umoja wa Waislam wa Tanganyika.

Si hili tu ndani ya TAA kulikuwa na viongozi wengi sana Waislam kama Sheikh
Hassan bin Ameir, Sheikh Said Chaurembo, Ali Jumbe Kiro, Idd Faiz Mafungo,
Idd Tosiri, Sheikh Mohamed Ramiyya
kwa kuwataja wachache.

Hali ya siasa ilikuwa hivi kwa kuwa Kanisa lilikuwa likiwatisha waumini wake
kutojihusisha nakwa sababu Kanisa na Wakoloni walikuwa washirika katika kuitawala
Tanganyika.

Hii ndiyo sababu Waislam walikuwa wengi katika TANU na kupigania uhuru wa
Tanganyikana ndiyo sababu Waislam wakaacha historia kubwa sana dhidi ya ukoloni.

Umeuliza juhudi za Wakristo katika kupigania uhuru.
Nimeziandika kwingi tu lakini kwa wingi hizo ni chache:

Ingia hapo chini:
Mohamed Said: LAMECK BUGOHE MUASISI WA TANU 1954 KAFARIKI NA KUZIKWA KIMYA KIMYA
Mohamed Said: KUTOKA JF: HISTORIA YA TANU - DK. VEDASTO KYARUZI, KASELLA BANTU NA JULIUS NYERERE
 
Hivi Uhuru ulipiganiwa na waislam tu, na Wakristo hawakufanya juhudi zozote kwa Uhuru wa nchi hii? Kama Wakristo walifanya juhudi mbona huwa huziandiki? Naomba jawabu Mzee wangu Mohamed Said, Msomi na mchambuziwa Historia Tanzania
wakristo wengi walikuwa wako bara huko, waislamu ndio walikuwako mijini na ukanda wote ambao ukoloni ulikita mizizi
 
Siku hizi habari hizi zimepuuziwa sana.sijui kwa nini mzee wangu watu wameamua kukupuuza tu.usikate tamaa lakini...najua inavyokuwa watu wanapokupuuza ila sasa utafanyaje?

😂😂😂😂 Watu wameona huna jipya.
 
Siku hizi habari hizi zimepuuziwa sana.sijui kwa nini mzee wangu watu wameamua kukupuuza tu.usikate tamaa lakini...najua inavyokuwa watu wanapokupuuza ila sasa utafanyaje?

😂😂😂😂 Watu wameona huna jipya.
Kiduku,
Sijapuuzwa,

Hivi karibuni nimefanya vipindi vitatu na Times FM.
Vipindi vitatu na Clouds FM

Nimefanya kipindi kimoja mubashara MUM FM.

Nimeshiriki katika documentary ya Nyerere katika Nyerere Day na East African TV
Nina vitabu kadhaa kwa wachapaji vitakuwa sokoni hivi karibuni In Shaa Allah.

KIa siku zinavyosogea historia hii inazidi kushika kasi.
Bwana Kiduku kuwa mimi nimepuuzwa taarifa hizi umezipata wapi?

Najua historia hii inakuchoma moyo lakini tufanyeje.
Hatuwezi kufuta historia.

 
wakristo wengi walikuwa wako bara huko, waislamu ndio walikuwako mijini na ukanda wote ambao ukoloni ulikita mizizi
Hiyo habari unayompa Nazjaz umeitoa kwenye makalio yako nadhani... Historia huijui hata baba lenu la Uongo lililoleta Mada linakuambia Wakristo walikuwa wakishirikiana na Waingereza kutawala sasa walikuwa wakitawala na Waingereza huko Bara pekee? akili mbili zinawasumbueni sana wavaa vipedo.... Ndio mkipotoshana huko Madrassa kuchukia Wasio Waislam basi mnajaa ujinga maisha yenu yote...

Kina John Rupia Tajiri wa Dar na wengineo walikuwa Waislam? Wadhani yale Makanisa ya St Joseph, St.Luther yalikuwa yanaswaliwa na Wazungu na Waislam enh!
 
Back
Top Bottom