Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 3,984
- 13,760
Abiria waliotarajia kusafiri kwa ndege iliyopata ajali Jumapili nje kidogo ya Uwanja wa Ndege wa Bukoba, sasa wataondoka leo kuelekea Dar es Salaam na Mwanza.
Wasafiri hawa ambao idadi yao ni 21 wa ndege ya Kampuni ya Precision, tangu Jumapili walikuwa Bukoba wakikaa hoteli ya ELCT, waliyopangiwa na kampuni hiyo baada ya ndege yake kutua kwa dharura ndani ya Ziwa Victoria, mita 180 kufika barabara ya kutua.
Katika ajali hiyo, jumla ya watu 19 walipoteza maisha, huku 26 wakiokolewa na wavuvi.
Abiria hao waliokwama Bukoba, hata hivyo hawatapanda dege kwenye uwanja wa mji huo, bali watabebwa na mabasi hadi Mwanza ambako wataendelea na safari ya Dar es Salaam na wale wanaoishia Mwanza, ndiyo watakuwa wamefika.
Mmoja wa Watendaji wa JamiiForums aliyekuwa miongoni mwa abiria waliotarajia kupanda ndege hiyo anaeleza kuwa Kampuni ya Precision imewataarifu leo kwamba wataondoka saa 4 kwa mabasi hadi Mwanza.
Anasema kuwa uongozi wa Precision umewaeleza kuwa watapanda ndege ya saa 3.15 usiku kutokea Mwanza kuelekea Dar es Salaam.
Wasafiri hawa ambao idadi yao ni 21 wa ndege ya Kampuni ya Precision, tangu Jumapili walikuwa Bukoba wakikaa hoteli ya ELCT, waliyopangiwa na kampuni hiyo baada ya ndege yake kutua kwa dharura ndani ya Ziwa Victoria, mita 180 kufika barabara ya kutua.
Katika ajali hiyo, jumla ya watu 19 walipoteza maisha, huku 26 wakiokolewa na wavuvi.
Abiria hao waliokwama Bukoba, hata hivyo hawatapanda dege kwenye uwanja wa mji huo, bali watabebwa na mabasi hadi Mwanza ambako wataendelea na safari ya Dar es Salaam na wale wanaoishia Mwanza, ndiyo watakuwa wamefika.
Mmoja wa Watendaji wa JamiiForums aliyekuwa miongoni mwa abiria waliotarajia kupanda ndege hiyo anaeleza kuwa Kampuni ya Precision imewataarifu leo kwamba wataondoka saa 4 kwa mabasi hadi Mwanza.
Anasema kuwa uongozi wa Precision umewaeleza kuwa watapanda ndege ya saa 3.15 usiku kutokea Mwanza kuelekea Dar es Salaam.