shamimuodd
JF-Expert Member
- Jan 28, 2019
- 1,188
- 2,113
Wadau,
Mara ya mwisho kuapa kutopanda bus za Abood ni mwezi wa pili mwanzoni, na hii ilitokana na mara kadhaa unapanda basi Dar na utakuta pale mbele kwa dereva wanajazwa watu kibao.
Na mkifika njiani wanajaza tena kama dala dala, wengine wanasimama kati kati. Na mkifika mizani basi wale abiria wanaambiwa washuke wapande dala dala au zinaandaliwa piki piki, wanakuja kupandia mbele. Wakati mwingine wale abiria wasiokuwa na siti wanaambiwa wasogee katikati.
Lingine lililonikera kabisa, yaani dereva wa hilo gari nililo panda alikuwa anaongea na mtu mwenye jina la kike (Fatuma) na inaonekana walikuwa kwenye mgogoro, dereva alikuwa anaongea na simu karibia muda wote na anajitahidi kumchimba biti Fatuma na wakati mwingine anakuwa na hasira huku gari ipo mwendo kasi sana.
Sasa ukichukulia gari imejaza watu kuzidi kiwango, spidi kubwa, nikaona hapa Abood zinakuja kuua watu wengi sana very soon.
Niliapa tangu siku hiyo Abood basi sintopanda tena labda wajirekebishe
Mara ya mwisho kuapa kutopanda bus za Abood ni mwezi wa pili mwanzoni, na hii ilitokana na mara kadhaa unapanda basi Dar na utakuta pale mbele kwa dereva wanajazwa watu kibao.
Na mkifika njiani wanajaza tena kama dala dala, wengine wanasimama kati kati. Na mkifika mizani basi wale abiria wanaambiwa washuke wapande dala dala au zinaandaliwa piki piki, wanakuja kupandia mbele. Wakati mwingine wale abiria wasiokuwa na siti wanaambiwa wasogee katikati.
Lingine lililonikera kabisa, yaani dereva wa hilo gari nililo panda alikuwa anaongea na mtu mwenye jina la kike (Fatuma) na inaonekana walikuwa kwenye mgogoro, dereva alikuwa anaongea na simu karibia muda wote na anajitahidi kumchimba biti Fatuma na wakati mwingine anakuwa na hasira huku gari ipo mwendo kasi sana.
Sasa ukichukulia gari imejaza watu kuzidi kiwango, spidi kubwa, nikaona hapa Abood zinakuja kuua watu wengi sana very soon.
Niliapa tangu siku hiyo Abood basi sintopanda tena labda wajirekebishe