brave one
JF-Expert Member
- Feb 5, 2013
- 4,879
- 7,386
Kiungo mshambuliaji wa zamani wa klabu ya Al
Ahly na Misri, Mohamed Aboutrika ameongezwa
kwenye orodha ya magaidi nchini Misri kufuatia
kutuhumiwa kuwa na uhusiano na kikundi cha
Muslim Brotherhood kilichopigwa marufuku.
Aboutrika anatuhumiwa kukifadhili kikundi cha
Brotherhood kinachotafsiriwa kama kundi la
kigaidi nchini Misri. Katika uchaguzi wa mwaka
2012, Aboutrika alimpendekeza mgombea wa
Brotherhood, Mohamed Morsi ambaye alishinda
urais na kudumu kwa kipindi cha mwaka mmoja
kabla ya kung’olewa madarakani na
kuorodheshwa kwenye orodha ya magaidi nchini
humo.
Aboutrika pia amekuwa akiunga mkono nchi ya
Palestina na kuvaa fulana za kuwaunga mkono
raia wa nchi hio katika vuguvugu dhidi ya Israel.
Wakili wa Aboutrika, Mohamed Osman amesema
Aboutrika ameorodheshwa kama gaidi licha ya
kutofikishwa mahakamani wala kujulishwa
kutuhumiwa.
” Tutakataa rufaa kupinga haya maamuzi,”
Amenukuliwa Osman huku Aboutrika mwenyewe
akikana tuhuma hizo.
Source: soka 360
Ahly na Misri, Mohamed Aboutrika ameongezwa
kwenye orodha ya magaidi nchini Misri kufuatia
kutuhumiwa kuwa na uhusiano na kikundi cha
Muslim Brotherhood kilichopigwa marufuku.
Aboutrika anatuhumiwa kukifadhili kikundi cha
Brotherhood kinachotafsiriwa kama kundi la
kigaidi nchini Misri. Katika uchaguzi wa mwaka
2012, Aboutrika alimpendekeza mgombea wa
Brotherhood, Mohamed Morsi ambaye alishinda
urais na kudumu kwa kipindi cha mwaka mmoja
kabla ya kung’olewa madarakani na
kuorodheshwa kwenye orodha ya magaidi nchini
humo.
Aboutrika pia amekuwa akiunga mkono nchi ya
Palestina na kuvaa fulana za kuwaunga mkono
raia wa nchi hio katika vuguvugu dhidi ya Israel.
Wakili wa Aboutrika, Mohamed Osman amesema
Aboutrika ameorodheshwa kama gaidi licha ya
kutofikishwa mahakamani wala kujulishwa
kutuhumiwa.
” Tutakataa rufaa kupinga haya maamuzi,”
Amenukuliwa Osman huku Aboutrika mwenyewe
akikana tuhuma hizo.
Source: soka 360