Absalom Kibanda: Serikali yenyewe ndio inatengeneza mazingira ya uwepo wa ‘Fake news’

Absalom Kibanda: Serikali yenyewe ndio inatengeneza mazingira ya uwepo wa ‘Fake news’

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
Mwanahabari mkongwe Absalom Kibanda ametoa maoni yake kuhusu umuhimu wa Serikali kufanya kazi kwa ukaribu na Vyombo vya Habari ambapo kwa asilimia kubwa amelaumu mazingira ya tata baina ya pande hizo mbili.

Akitoa maoni katika Kongamano lililohusisha Wadau wa Habari, Serikali na Waandishi likiwa na kaulimbiu ya "Habari kwa Maendeleo Endelevu",jana Desemba 17, 2022 alisema:

“Mwaka 2016/17 nilipata tofauti na Rais Magufuli nilipojaribu kumshauri ni vizuri turithi kile kizuri ambacho marais wastaafu walitufundisha katika sekta ya habari.

“Kwanza Wanahabari tumewahi kutoa Rais mwanahabari ambaye ni Benjamin Mkapa, huyu alikuwa anakosoa sana Wanahabari lakini alitoa fursa sana kwa Media kupata taarifa.

“Tunaongea kuhusu fake nyuzi leo lakini hilo suala halijaanza na Mitandao ya Kijamii, ni suala la kihistoria.

“Hatujiulizi kwa nini wakati wa Mkapa au Kikwete kulikuwa na kiwango kidogo cha fake news, hata katika katika media kubwa kwa sasa inatokea fake news zinashika kasi, hiyo ni kwa kuwa waandishi wa habari hawapo sehemu nyingi za matukio.

“Mfano Rais Samia yupo Marekani ameandamana na waandishi wangapi? Nani wa Daily News ameambatana naye, vipi kuhusu TBC, Azam TV au Clouds FM, huo ndiyo mwanzo wa fake news.

“Rais alienda kuzindua Royal Tour, lakini mambo ya ajabu kabisa, Msigwa anamhoji Dkt. Abbas, huo ni uandishi gani wa habari! Tunafungua wenyewe mlango wa fake news kwa kuwa waandishi wetu hawatumiki inavyotakiwa.

“Hatujiulizi kwa nini media nyingi zinazoanzishwa leo ni za burudani na michezo, sababu upande wa serious news tumeuua.

“Leo hii vyumba vya habari Tanzania kuna generation gape, nani anawalea hao wadogo kitaaluma? Media inashindwa kwa kuwa Serikali ambaye ndiye mdau mkuu imeacha kuhusisha media ndiyo maana hazina uwezo kiuchumi.

“Kama kwenye Royal Tour, Rais aliweza kuksanya Tsh. Bilioni 7 za bajeti ya mradi huo, je mlishindwa kutenga hata Tsh. Milioni 200 kuandamana na Rais Marekani au kule Zanzibar, nadhani hapo ndipo tumekosea, naomba nitoe dokezo.”
 
Rais alienda kuzindua Royal Tour, lakini mambo ya ajabu kabisa, Msigwa anamhoji Dkt. Abbas, huo ni uandishi gani wa habari! Tunafungua wenyewe mlango wa fake news kwa kuwa waandishi wetu hawatumiki inavyotakiwa.
 
Sawa,, lakini angeweka bajeti hiyo milioni 200 ajili ya wanahabari, watu hapa wangekuja kusema matumizi mabaya ya hela,,
Lakini bado tunahitaji uwazi zaidi ili kyondokana na serikali kutoa ufafanuzi mara kwa mara,,
Ndio sababu ya Rais kuwahimiza viongozi watoke kuisemea serikali inavyifanya maendeleo,, badala ya kusubiri wapinzani kuibua issues🤷‍♂️
 
Serikali ya Tanzania inawsgharimia waandishi aina ya Musiba....
 
Kila mtu anapenda uhai wake. R.i.P anzory
 
je mlishindwa kutenga hata Tsh. Milioni 200

Vyombo vya habari mtapata uhuru gani ktj kazi ikiwa chombo chenu cha media kitapewa fedha za safari na mhimili wa serikali.

Pia huwa ktk press conference zenu na serikali huwa naona waandishi wa habari hupiga makofi kushagilia, hii sijawahi kuona CNN, BBC, Al Jazeera au White House press conference waandishi walio huru huwa wanapiga makofi kutokana na kila jibu analotoa msemaji wa ikulu /serikali / CEO wa TANESCO n.k ni waandishi wa Tanzania ndiyo hujisahau kuwa wao ni mhimili wa nne na kupigia makofi wale mnaowahoji.
 
Sasa mwandishi analinganisjaje kipindi cha mkapa ili hata simu tu ya kitorchi hazikuwepo kwa watu wengi achilia mbali hiyo smart phone
 
Yaani serikali ilipe posho za safari kwa waandishi wa habari- ili vyombe vyao viapte habari, vitangaze hiyo habari, na wapate hela wale wao- WAANDISHI hivi mtajitegemea lini?
 
19 December 2022
Iringa, Tanzania

MAKAMU WA RAIS : AWAASA WAHARIRI WATU HAWAELEWI, HATA DOKUMENTARI NZURI ....



KONGAMANO LA WAHARIRI NA WADAU WA UHIFADHI MAZINGIRA 19 DECEMBER 2022

Wadau wa uhifadhi mazingira kuhusiana na changamoto ya uharibifu wa mazingira uliosababisasha Mto The Great Ruaha kutotirisha maji kwa zaidi ya siku 100 na kuathiri Ikolojia ya Hifadhi ya Taifa Ruaha. Hayo yamesemwa na kujadiliwa leo katika Kongamano la wahariri na wadau wa Uhifadhi mazingira na utunzaji wa vyanzo vya maji linaloendelea katika Ukumbi wa Masiti mjini Iringa, Tanzania .
1671450553827.png

Picha : Habibu Mchange akiteta jambo na makamu wa rais Mh. Isdori P. Mpango mjini Iringa leo 19.12.2022
Bw. Habibu Mchange Mwenyekiti wa Kituo Cha Wanahabari Watetezi wa Rasilimali na taarifa MECIRA aliwasilisha taarifa yake ya kina kwenye Kongamano la Wahariri na Wadau wa Uhifadhi, Mazingira na utunzaji wa vyanzo vya maji linalofabyika kwenye ukumbi wa Masiti Gangilonga Mkoani Iringa Leo Disemba 19,2022 ambapo Mgeni rasmi ni Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Philip Isdori Mpango.
 
19 December 2022
Iringa, Tanzania

MAKAMU WA RAIS : AWAASA WAHARIRI WATU HAWAELEWI, HATA DOKUMENTARI NZURI ....



KONGAMANO LA WAHARIRI NA WADAU WA UHIFADHI MAZINGIRA 19 DECEMBER 2022

Wadau wa uhifadhi mazingira kuhusiana na changamoto ya uharibifu wa mazingira uliosababisasha Mto The Great Ruaha kutotirisha maji kwa zaidi ya siku 100 na kuathiri Ikolojia ya Hifadhi ya Taifa Ruaha. Hayo yamesemwa na kujadiliwa leo katika Kongamano la wahariri na wadau wa Uhifadhi mazingira na utunzaji wa vyanzo vya maji linaloendelea katika Ukumbi wa Masiti mjini Iringa, Tanzania .
View attachment 2451802

Bw. Habibu Mchange Mwenyekiti wa Kituo Cha Wanahabari Watetezi wa Rasilimali na taarifa MECIRA aliwasilisha taarifa yake ya kina kwenye Kongamano la Wahariri na Wadau wa Uhifadhi, Mazingira na utunzaji wa vyanzo vya maji linalofabyika kwenye ukumbi wa Masiti Gangilonga Mkoani Iringa Leo Disemba 19,2022 ambapo Mgeni rasmi ni Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Philip Isdori Mpango.

Chawa Mchange katika ubora wake
 
Sawa,, lakini angeweka bajeti hiyo milioni 200 ajili ya wanahabari, watu hapa wangekuja kusema matumizi mabaya ya hela,,
Lakini bado tunahitaji uwazi zaidi ili kyondokana na serikali kutoa ufafanuzi mara kwa mara,,
Ndio sababu ya Rais kuwahimiza viongozi watoke kuisemea serikali inavyifanya maendeleo,, badala ya kusubiri wapinzani kuibua issues🤷‍♂️
Kwa upande wangu, kuanzisha chombo cha habari kisichotegemea upande wowote halafu chombo hicho hicho kikategemea kubebwa na wenye taarifa hapo bora hivyo vyombo vya habari visiwepo.
 
Wao watajijua wenyewe sie taarifa za kweli zinatufikia na kwa wakati.
 
Back
Top Bottom