Thamani Academy
New Member
- Jul 25, 2020
- 4
- 3
Ninatambua sana kwamba, wamekufundisha na kukuambia "Utafute Role Model" na uige kile anachokifanya ili uweze kufanikiwa kama yeye. Wamekufundisha pia kusoma vitabu vya Mafanikio na kufuata kile kilichoandikwa humo.
Mimi leo ninataka kukuambia ukweli. Ukweli utakaobadili maisha yako. Upo tayari kusikia ukweli huu?
"𝘜𝘯𝘢𝘶𝘢 𝘶𝘸𝘦𝘻𝘰 𝘸𝘢𝘬𝘰, 𝘶𝘯𝘢𝘶𝘢 𝘶𝘣𝘶𝘯𝘪𝘧𝘶 𝘸𝘢𝘬𝘰 𝘯𝘢 𝘶𝘯𝘢𝘶𝘢 𝘬𝘪𝘱𝘢𝘫𝘪 𝘤𝘩𝘢𝘬𝘰 𝘬𝘸𝘢 𝘬𝘶𝘪𝘨𝘢 𝘫𝘪𝘯𝘴𝘪 𝘢𝘯𝘢𝘷𝘺𝘰𝘧𝘢𝘯𝘺𝘢/𝘢𝘭𝘪𝘷𝘺𝘰𝘧𝘢𝘯𝘺𝘢 𝘮𝘵𝘶 𝘮𝘸𝘪𝘯𝘨𝘪𝘯𝘦"
Kuna tofauti kubwa sana kati ya kujifunza namna ya kufanikiwa na kujenga Biashara au mfumo utakaokusaidia kufikia mafanikio halisi
Hii ni sawa na utofauti uliopo katika ya "Kipaji" na "Juhudi". Kuna watu wengi sana wenye vipaji, lakini hawana mchango wowote hapa duniani (Kwa sababu ya kutotumia vipaji vyao). Na kuna watu hawana kabisa vipaji vikubwa, lakini wanamchango mkubwa sana hapa duniani (Kutokana na Juhudi zao).
Ni sahihi kabisa kupata Maarifa na Kujifunza kutoka kwa watu waliofanikiwa. Lakini SI SAHIHI "Kuiga" kile walichokifanya/wanachokifanya.
Kuna msemo wa Kiingereza unasema "The Struggle is REAL" Maana yake, zile changamoto utakazozipitia kwa kujenga kitu chako, kwa kutumia ubunifu wako, juhudi na Maarifa, ndio chachu ya Mafanikio yako
Kwa maana hiyo, ni muhimu sana upitie changamoto Halisi kwa kujenga mfumo utakaokufaa wewe mwenyewe, kitu ambacho watu wengi hukimbia na kuishia kuiga vile wanavyofanya watu wengine.
Mafanikio hayana Fomula inayofanana kwa kila mtu. Kujifunza njia aliyopita mtu mwingine haina maana na wewe ni lazima upite njia hiyo hiyo. Katika mafanikio, wewe una sehemu yako, na ni wewe tu ndio utakaepita njia hiyo na wala si mtu mwingine.
Hebu niambie, Ulishawahi kuiga Jinsi anavyofanya mtu mwingine? Matokeo yalikuwaje?
Let's Meet again[emoji1666]
#weweniwathamani (Mtu mwingine Asikuambie Tofauti).
Mimi leo ninataka kukuambia ukweli. Ukweli utakaobadili maisha yako. Upo tayari kusikia ukweli huu?
"𝘜𝘯𝘢𝘶𝘢 𝘶𝘸𝘦𝘻𝘰 𝘸𝘢𝘬𝘰, 𝘶𝘯𝘢𝘶𝘢 𝘶𝘣𝘶𝘯𝘪𝘧𝘶 𝘸𝘢𝘬𝘰 𝘯𝘢 𝘶𝘯𝘢𝘶𝘢 𝘬𝘪𝘱𝘢𝘫𝘪 𝘤𝘩𝘢𝘬𝘰 𝘬𝘸𝘢 𝘬𝘶𝘪𝘨𝘢 𝘫𝘪𝘯𝘴𝘪 𝘢𝘯𝘢𝘷𝘺𝘰𝘧𝘢𝘯𝘺𝘢/𝘢𝘭𝘪𝘷𝘺𝘰𝘧𝘢𝘯𝘺𝘢 𝘮𝘵𝘶 𝘮𝘸𝘪𝘯𝘨𝘪𝘯𝘦"
Kuna tofauti kubwa sana kati ya kujifunza namna ya kufanikiwa na kujenga Biashara au mfumo utakaokusaidia kufikia mafanikio halisi
Hii ni sawa na utofauti uliopo katika ya "Kipaji" na "Juhudi". Kuna watu wengi sana wenye vipaji, lakini hawana mchango wowote hapa duniani (Kwa sababu ya kutotumia vipaji vyao). Na kuna watu hawana kabisa vipaji vikubwa, lakini wanamchango mkubwa sana hapa duniani (Kutokana na Juhudi zao).
Ni sahihi kabisa kupata Maarifa na Kujifunza kutoka kwa watu waliofanikiwa. Lakini SI SAHIHI "Kuiga" kile walichokifanya/wanachokifanya.
Kuna msemo wa Kiingereza unasema "The Struggle is REAL" Maana yake, zile changamoto utakazozipitia kwa kujenga kitu chako, kwa kutumia ubunifu wako, juhudi na Maarifa, ndio chachu ya Mafanikio yako
Kwa maana hiyo, ni muhimu sana upitie changamoto Halisi kwa kujenga mfumo utakaokufaa wewe mwenyewe, kitu ambacho watu wengi hukimbia na kuishia kuiga vile wanavyofanya watu wengine.
Mafanikio hayana Fomula inayofanana kwa kila mtu. Kujifunza njia aliyopita mtu mwingine haina maana na wewe ni lazima upite njia hiyo hiyo. Katika mafanikio, wewe una sehemu yako, na ni wewe tu ndio utakaepita njia hiyo na wala si mtu mwingine.
Hebu niambie, Ulishawahi kuiga Jinsi anavyofanya mtu mwingine? Matokeo yalikuwaje?
Let's Meet again[emoji1666]
#weweniwathamani (Mtu mwingine Asikuambie Tofauti).