Achinjwa Kwa Shoka Kwa Kutembea na Mpenzi wa Mtu

Achinjwa Kwa Shoka Kwa Kutembea na Mpenzi wa Mtu

Herbalist Dr MziziMkavu

JF-Expert Member
Joined
Feb 3, 2009
Posts
42,872
Reaction score
34,363
MKAZI wa Uru Kusini mkoani Kilimanaro, aliyetambulika kwa jina la JAMES Kiwale (28), ameuawa kikatili baada ya kupigwa na shoka ya kichwa kwa kilichodaiwa kuwa ana uhusiano wa kimapenzi na mchumba wa mtu. James alikutwa na mkasa wakati alipokuwa akitoka makaburini kwenye mazishi ya jirani yake.

Akitoa taarifa hiyo, Kamanda wa Polisi mkoani Kilimanjaro, Bw.Lucas Ng'oboko, amesema kuwa marehemu alipigwa na shoka kichwani na kupelekea kutenganishwa kati ya mwili na kichwa na kijana mmoja aliyefahamika kwa jina la Joachim.

Alisema kijana huyo huyo aliamua kumpiga shoka mwenzake baada ya kumshuku kuwa alikiwa akitembea na mchumba wake aitwae Maria kitendo ambacho yeye hakukiafiki na kuchukua maamuzi hayo.

Aliendelea kusema kuwa ilidaiwa kuwa, marehemu wakati wa uhai wake alikuwa akitamba kuwa atahakikisha kuwa anatembea na mwanamke huyo jambo lililomsababishia hasira kali mtuhumiwa na kufanya kitendo hicho cha unyama.

Alisema mtuhumiwa huyo alimwekea mtego marehemu wakati anatoka kumzika jirani yake na kufanikiwa kumpiga shoka ya kichwa na kupelekea kichwa hicho kugawanyika mara mbili.

Alisema mara baada ya kufanya kitendo hicho mtuhumia huyo alikimbia na juhudi za jeshi hilo zinaendelea kumsaka ili hatua za kisheria zifuate mkondo wake

chanzo NIFAHAMISHE Tanzania news portal .: Habari za Tanzania :.

Jamani tuache kuwatongoza wapenzi wa watu mwisho wake ndio huo. Mungu amlaze pema marehemu.
 
MKAZI wa Uru Kusini mkoani Kilimanaro, aliyetambulika kwa jina la JAMES Kiwale (28), ameuawa kikatili baada ya kupigwa na shoka ya kichwa kwa kilichodaiwa kuwa ana uhusiano wa kimapenzi na mchumba wa mtu. James alikutwa na mkasa wakati alipokuwa akitoka makaburini kwenye mazishi ya jirani yake.

Akitoa taarifa hiyo, Kamanda wa Polisi mkoani Kilimanjaro, Bw.Lucas Ng'oboko, amesema kuwa marehemu alipigwa na shoka kichwani na kupelekea kutenganishwa kati ya mwili na kichwa na kijana mmoja aliyefahamika kwa jina la Joachim.

Alisema kijana huyo huyo aliamua kumpiga shoka mwenzake baada ya kumshuku kuwa alikiwa akitembea na mchumba wake aitwae Maria kitendo ambacho yeye hakukiafiki na kuchukua maamuzi hayo.

Aliendelea kusema kuwa ilidaiwa kuwa, marehemu wakati wa uhai wake alikuwa akitamba kuwa atahakikisha kuwa anatembea na mwanamke huyo jambo lililomsababishia hasira kali mtuhumiwa na kufanya kitendo hicho cha unyama.

Alisema mtuhumiwa huyo alimwekea mtego marehemu wakati anatoka kumzika jirani yake na kufanikiwa kumpiga shoka ya kichwa na kupelekea kichwa hicho kugawanyika mara mbili.

Alisema mara baada ya kufanya kitendo hicho mtuhumia huyo alikimbia na juhudi za jeshi hilo zinaendelea kumsaka ili hatua za kisheria zifuate mkondo wake

chanzo NIFAHAMISHE Tanzania news portal .: Habari za Tanzania :.

Jamani tuache kuwatongoza wapenzi wa watu mwisho wake ndio huo. Mungu amlaze pema marehemu.

Hi habari mbaya, na pole kwa wafiwa.
Lakini kung'ang'ania mchumba wa mtu....!mhh inahitaji moyo.

Na huyo mchumba (binti) yuko ktk hali gani
 
mwache auwawe mkware huyu..wala asi rest in peace.
 
Job well done..... This should be taken as a lesson on how much infidelity hurts!
 
Njia za kidemokrasia mara zote zinapendekezwa ili kumaliza migogoro ya aina yoyote. Madhara ya kuchukua hatua kama hii ni mabaya mno.Unaweza usifurahie tena umri wako uliobakia.
 
Laiti kama huyu jamaa hakutamba hapo awali ningekuwa na mtizamo mwingine lakini ilhari alitamba nadhani hilo lilompata Lamfaa sabau kuna wakware wengi hupenda kuharibu mahusiano ya watu bila sababu za msingi.
 
Jamani wanaume mutahadhari na misifa yenu hiyo munayoona kwa kuchukua wachumba za watu.

Hata kama alikuwa hatembei nae ile tabia ya kutamba tu ni ukosefu wa heshima. Kuna wengine hujisifu wametembea na fulani hata kama sio kweli ili kumkera mwenye mali yake. Wengine hasira zao ziko nje nje na matokeo yake ndiyo hayo ya kuuwawa kwa mashoka.

Sio kwamba naona kitendo hicho ni kizuri, ingekuwa vyema kama akafanya uchunguzi, akiona ni kweli akaachana na huyo binti ijapokuwa hapo ni pachungu sana.
 
huyo joachim (muuwaji) angekuwa shujaa au aliamini anafanya jambo la haki
angebaki papo hapo. kwa kutimka anaonyesha ni muoga na hajiamini asilani.
sasa huko alikokimbilia ataendelea kuuwa tu?

huyu anayedaiwa kumegwa ni mchumba na sio hata mke. jamaa angeweza kuchomoa
na kumshukuru mola wake kwa kumuonyesha mapema ukweli (kama kweli maria alikuwa$anamegwa na
mtu mwengine) hivyo kumuepusha na machungu kwenye ndoa.

sasa kaua na amekuwa mtuhumiwa wa mauaji. na akikamatwa kipindi atakachokuwa lupango maria
ataendelea kumegwa na yeye vilevile wasela wa lupango wanaweza kumuwowa vilevile.

ama kweli hasira hasara
 
RIP James, nadhani hukumbaka Maria ni makubaliano tu! Sheria Ichukue mkondo wake na Joachim naye ahukumiwe kufa
 
Dawa ya watu wa tabia hiyo ndio hiyo. Alifikiri ni ushujaa kuiba vya wenzake!!
 
Maisha na wanawake wa siku hizi utachnga wangapi


MKAZI wa Uru Kusini mkoani Kilimanaro, aliyetambulika kwa jina la JAMES Kiwale (28), ameuawa kikatili baada ya kupigwa na shoka ya kichwa kwa kilichodaiwa kuwa ana uhusiano wa kimapenzi na mchumba wa mtu. James alikutwa na mkasa wakati alipokuwa akitoka makaburini kwenye mazishi ya jirani yake.

Akitoa taarifa hiyo, Kamanda wa Polisi mkoani Kilimanjaro, Bw.Lucas Ng'oboko, amesema kuwa marehemu alipigwa na shoka kichwani na kupelekea kutenganishwa kati ya mwili na kichwa na kijana mmoja aliyefahamika kwa jina la Joachim.

Alisema kijana huyo huyo aliamua kumpiga shoka mwenzake baada ya kumshuku kuwa alikiwa akitembea na mchumba wake aitwae Maria kitendo ambacho yeye hakukiafiki na kuchukua maamuzi hayo.

Aliendelea kusema kuwa ilidaiwa kuwa, marehemu wakati wa uhai wake alikuwa akitamba kuwa atahakikisha kuwa anatembea na mwanamke huyo jambo lililomsababishia hasira kali mtuhumiwa na kufanya kitendo hicho cha unyama.

Alisema mtuhumiwa huyo alimwekea mtego marehemu wakati anatoka kumzika jirani yake na kufanikiwa kumpiga shoka ya kichwa na kupelekea kichwa hicho kugawanyika mara mbili.

Alisema mara baada ya kufanya kitendo hicho mtuhumia huyo alikimbia na juhudi za jeshi hilo zinaendelea kumsaka ili hatua za kisheria zifuate mkondo wake

chanzo NIFAHAMISHE Tanzania news portal .: Habari za Tanzania :.

Jamani tuache kuwatongoza wapenzi wa watu mwisho wake ndio huo. Mungu amlaze pema marehemu.
 
Back
Top Bottom