Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 3,984
- 13,760
Jambo hilo lilisababisha kuitwa na Aaskari wa Jeshi la Polisi na kukamatwa na kupelekwa Ofisini na baadaye akapelekwa Polisi Bunda.
Akifafanua kuhusu kilichotokea, Mjumbe wa ACT Bunda, Mayunga Kilanga amesema "Walimvamia Keranga wakaanza kumshambulia kisha wakapiga simu Polisi wakidai yeye ndiye kasababisha fujo, wamemkamata na kumpeleka kituoni tangu jana (Novemba 27, 2024). Tunawasiliana na ACT Taifa ili kuoata Wanasheria wa kusimamia suala lake.
"Walipomchukua huku nyumba wakamtangaza Mgombea wa CCM kuwa mshindi bila ya upande wa pili kusaini fomu ya makubaliano."
===============
UPDATES...ACT WATAKA UCHAGUZI URUDIWE KATA YA HUNYARI
Mjumbe wa ACT Bunda, Mayunga Kilanga amesema "Hatimaye Keranga amefanikiwa kutoka asubuhi hii, Polisi wamemruhusu na kumtaka arejee kesho kituoni hapo, mpango uliopo kwa sasa ni kumpeleka Hospitali kwa kuwa bado ana maumivu, walimuumiza sana walipomshambulia.
"Baada ya hapo tuna mpango wa kukata rufaa uchaguzi urudiwe kwa kuwa Wakala wetu aliondolewa kihuni na hakukuwa na haki iliyotendeka, tumeshaanza mchakato ili tuhakikishe Uchaguzi unarudiwa.