Uchaguzi 2020 ACT-Wazalendo wanaweza kumfukuza uanachama Membe kwa wakati huu?

Uchaguzi 2020 ACT-Wazalendo wanaweza kumfukuza uanachama Membe kwa wakati huu?

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Joined
Feb 24, 2012
Posts
5,108
Reaction score
10,191
Maneno yanayoendelea mtandaoni ni mengi ila inaonyesha Membe kakaza hawezi kuruhusu kuacha kujaribu kutetea ndoto yake ya kuwa rais.

Awali Membe alijiamini kuwa na watu wengi nyuma yake ambao angehama nao, lakini akajikuta ameondoka mwenyewe, wale wachache kutoka CUF na CCM waliojiunga na ACT Lindi na Mtwara, walirudisha kadi kwa mama Samia na kujiunga na CCM.

Hii inaonyesha hata wachache walioamini kuwa kweli ana nguvu wameona hana nguvu za hivyo. ACT ni tofauti na CCM, kwa kuwa Membe sio Mwenyekiti wa ACT ila ni Mshauri, maamuzi yanabaki kuwa ya Mwenyekiti, Mshauri sio lazima ushauri wake ukubalike, sasa hapo utaona kuwa Membe alikuwa anavumiliwa tu.

Lakini je, wakiamua kumvua uanachama Membe kwa hali ya sasa, je ACT Itakuwa na hasara yoyote?

Hujuma dhidi ya Membe zilianza kitambo.

Picha linaanza ule wimbo wa Baba Levo hausikiki, wanaimbaga: "Jamani Membe huyoo, Membe huyooo'" hausikiki nikaona mh! kuna kitu hapa.
 
Mbona vyama vingine vinamuunga mkono Magufuli, haliyakuwa wanawagombea mfano NCCR, TLP, TADEA, UPDP, UDP. Sio dhambi au vibaya ACT wakimuunga mkono Lissu hata kama wanamgombea.

Membe hawezi kufukuzwa, atabaki kwenye karatasi ya uchaguzi lakini hata yeye anamuunga mkono Lissu, hakuna mgombea amemuunga mkono mgombea wa chama kingine hadharani kwa huku bara. Kwahio tulieni hivyohivyo tunaenda na Lissu.
 
Mbona vyama vingine vinamuunga mkono Magufuli, haliyakuwa wanawagombea mfano NCCR, TLP, TADEA, UPDP, UDP. Sio dhambi au vibaya ACT wakimuunga mkono Lissu hata kama wanamgombea....
Vyama vinavyomuunga mkono Magufuli havina mgombea urais ndio maana hata kwenye matangazo wanaweka picha ya mbunge na picha ya Magufuli.

Kwa hiyo hivyo vyama TLP na UPDP havina wagombea urais ndio maana walisema wanampigia kampeni Magufuli, hauwezi kuwa na mgombea wako ukaanza kumpigia kampeni mgombea mwingine.
 
Vyama vinavyomuunga mkono Magufuli havina mgombea urais ndio maana hata kwenye matangazo wanaweka picha ya mbunge na picha ya Magufuli.

Kwa hiyo hivyo vyama TLP na UPDP havina wagombea urais ndio maana walisema wanampigia kampeni Magufuli, hauwezi kuwa na mgombea wako ukaanza kumpigia kampeni mgombea mwingine.
NCCR pia wanamuunga.
 
CCM akili wanazotumia kwenye Siasa ni kubwa sana.

Mapema mwanzoni mwa Uchaguzi Bashiru alisema Kuishinda ACT ni Rahisi kuliko CUF kwa sababu ya Ukubwa wa Kitaasisi.

Kivyovyote vile Zitto ndio amepoteza hii game, cause Nguvu ya ACT imeangukikia mikononi kwa Maalim Seif na Zitto inabidi awe mtumwa wa Seif tu au Ampige Chini Maalimu Zanzibar akaombe Support CCM kuua Nguvu ya Maalim Zanzibar kwa zawadi ya wabunge wachache.

Mwisho wa Siku Zitto amenasa kwenye Tundu Bovu, Maalim na Watu Wake Walikuwa Makini sana na Zitto hadi kumpora chama chake.

Baada ya Uchaguzi naomba turudi tujiulize Ni Lipumba au Kundi la Maalim ndio liliua CUF
 
CCM akili wanazotumia kwenye Siasa ni kubwa sana.

Mapema mwanzoni mwa Uchaguzi Bashiru alisema Kuishinda ACT ni Rahisi kuliko CUF kwa sababu ya Ukubwa wa Kitaasisi.

Kivyovyote vile Zitto ndio amepoteza hii game, cause Nguvu ya ACT imeangukikia mikononi kwa Maalim Seif na Zitto inabidi awe mtumwa wa Seif tu au Ampige Chini Maalimu Zanzibar akaombe Support CCM kuua Nguvu ya Maalim Zanzibar kwa zawadi ya wabunge wachache.

Mwisho wa Siku Zitto amenasa kwenye Tundu Bovu, Maalim na Watu Wake Walikuwa Makini sana na Zitto hadi kumpora chama chake.

Baada ya Uchaguzi naomba turudi tujiulize Ni Lipumba au Kundi la Maalim ndio liliua CUF
CCM ni chama kilichokomaa Sana.Ni mzazi wa vyama hivyo vyote, so kama mzazi anawajua watoto wake vyemaaa. Tanzania mpya inakuja.
 
Ondoeni tamaa za kijinga hafukuzwi mtu hapa huo upolepole na ubashiru hukohuko.
 
Vyama vinavyomuunga mkono Magufuli havina mgombea urais ndio maana hata kwenye matangazo wanaweka picha ya mbunge na picha ya Magufuli.

Kwa hiyo hivyo vyama TLP na UPDP havina wagombea urais ndio maana walisema wanampigia kampeni Magufuli, hauwezi kuwa na mgombea wako ukaanza kumpigia kampeni mgombea mwingine.
Bila kutumia jicho la tatu, huu mchezo huwezi kuuelewa, katika ngumi hiyo ni TKO, kisheria membe lazima aseme vile, kwani sheria za kuungana ni ngumu sana!! Kwa kilichofanyika kati ya ACT, na CDM, ndio njia pekee, na kisheria huwezi kuwabana!!!
 
Back
Top Bottom