Papaa Mobimba
JF-Expert Member
- Jan 27, 2018
- 882
- 3,337
Katibu Mkuu wa ACT Wazalendo ndugu Ado Shaibu ameendelea na kampeni za uchaguzi wa Serikali za Mitaa, na Novemba 21, 2024 alikuwa Jimbo la Mbeya Mjini, Kata ya Ruanda Mtaa wa Makunguru ambapo amepita mtaa kwa mtaa kuwanadi wagombea.
Ameeleza kuwa chama cha ACT Wazalendo kimelenga kuboresha miundombinu ya barabara kwa kutumia viongozi wake wa mitaa ikiwa watapewa ridhaa katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa utakaofanyika Novemba 27, 2024
Amesema ni muhimu kuwa na msingi imara wa viongozi kuanzia ngazi ya chini ambao watasimamia masilahi ya wafanyabiashara wadogo kwa kuwawezesha kupata mikopo, na mazingira mengine mazuri ya biashara.
Ameeleza kuwa chama cha ACT Wazalendo kimelenga kuboresha miundombinu ya barabara kwa kutumia viongozi wake wa mitaa ikiwa watapewa ridhaa katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa utakaofanyika Novemba 27, 2024
Amesema ni muhimu kuwa na msingi imara wa viongozi kuanzia ngazi ya chini ambao watasimamia masilahi ya wafanyabiashara wadogo kwa kuwawezesha kupata mikopo, na mazingira mengine mazuri ya biashara.