jmushi1
Platinum Member
- Nov 2, 2007
- 26,329
- 25,263
Very sad,she was only 32.
http://movies.msn.com/movies/article.aspx?news=448013>1=28101
http://movies.msn.com/movies/article.aspx?news=448013>1=28101
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Wabongo bwana, hivi kila two bit Hollywood actress atakayejioverdose tutamuweka hapa?
Wabongo wangapi wamekufa na kuumia kwenye tetemeko la ardhi Mbeya ? Tunajua? Tunafuatilia? Au kwa sababu hawana Hollywood glamor?
Una uhakika gani kuwa mie ni MBONGO?
Unafikiri kwa kuwa naandika Kiswahili na kujiita Sikonge basi nimeshakuwa Mbongo? Ni sawa na kuona ng'ombe mweusi na kusema hivyo bila kujua kumbe upande wa pili ana mabaka meupe.
Mwisho ni kuwa binadamu wote husikitika kwa kifo/vifo vya watu wanaowafahamu. Juzijuzi hapa nilifiwa na baba mkubwa. Kijijini huko Sikonge yalikuwa mazishi makubwa sana hasa ukichukulia ni familia ya Mwanangwa. Hapa JF watu waliendelea na story kama hakikutokea kitu. Hata ningeliandika hapa, kuna mtu angelishituka? Zingeliandikwa POLE kadhaa na mchezo ukaisha. Ni tofauti hata tukisema "fulani wa JF" kauguwa kwani ni watu ambao ingawa simfahamu, ukweli ni kuwa ameshakuwa karibu na mimi kwa siku nyingi sasa.
Huyu dada na yeye tumeshakuwa naye kwenye nyumba zetu mara kadhaa. Tumemuona na kusoma habari zake kwenye magazeti. Utake usitake ameshakuwa karibu yetu sisi ingawa yeye hatufahamu. Si yeye tu ila hata hapa Tanzania wapo wengi tu kama marehemu Gama (nilipata bahati ya kumuona na kama RC namshukuru sana kwani kuanzia niliposikia kahamishiwa Tabora, nilifahamu kuwa ataubadilisha Mkoa, na kweli. Nakumbuka kumuona wakisalimiana na Meja Odo wa Msange JKT wakati nikiwa JKT TAbora). Watu kama Amina Chifupa, Sokoine, Nyerere, James mwana wa Dandu, Ramadhani Lenny, School mates wangu Method Mogela na Salehe Sonda (wote wa Simba S.C.), Said Mwamba Kizota (homeboy), na wengine wengi.
Sasa wewe unataka niwalilie watu wa Mbeya ambao hata sijawahi kuwasikia? Umenikumbusha ugomvi wa marehemu shangazi na marehemu baba. Kuna babu yetu sijui kivipi kwenye ukoo alihamia Mwanza na kufika huko akaowa mwanamke fulani na yule mama akafariki. Baba alisikia na akakaa kimya. Shangazi alipokuja kupata habari na yeye na kukuta kumbe kaka yake aliambiwa na hakusema akaja juu kwa Mzee kuwa kwa nini hakuambiwa. Baba akasema ehh, kwani ulikuwa unamfahamu? Shangazi kakaa kimya na ghafla akaruka na kusema "sasa itabidi tufanye msiba". Mzee alimjibu hivi: "kama unapenda sana kulilia watu, redio hiyo na ikifika jioni kuna matangazo ya vifo, chagua mmoja ambaye kifo chake au jina lake umelipenda na UMLILIE".
Mkuu Bluray, kama wa Mbeya waliokufa kwa matetemeko wamekuuma sana, unaweza walilia au hata kujinyima mshahara wako wa mwezi mmoja na uwapelekee na hapo utakuwa umefanya jambo la maana. Sanasana ni kuwa JF kama kawaida, tutakuja na pole na RIP kibao na mwisho wa siku kila mtu anaenda kulala kwake na kusahau. Anyway, ndiyo uzuri wa forrum, ni kubwa saana, na kuna topic kibao unazoweza kuzisoma na kuzichangia. Na uzuri kichwa cha habari kimewekwa wazi na unapoingia unafahamu kabisa unaingia mlango upi. Kama ni wa choo na wewe ulitaka kwenda wa hotel, hapo si kosa letu tena na hakuna tunachoweza kukusaidia ili usiingie kwenye topic zenye kichwa cha habari kilicho wazi na wewe Bado unazamia na ukizamia unapata kichefuchefu...........
Mbona unajicontradict urself???mara wewe sio mbongo then unaleta story za kwenu kijijini!!!!!mara school mates zako!!!au wewe ni mkimbizi???Una uhakika gani kuwa mie ni MBONGO?
Unafikiri kwa kuwa naandika Kiswahili na kujiita Sikonge basi nimeshakuwa Mbongo? Ni sawa na kuona ng'ombe mweusi na kusema hivyo bila kujua kumbe upande wa pili ana mabaka meupe.
Mwisho ni kuwa binadamu wote husikitika kwa kifo/vifo vya watu wanaowafahamu. Juzijuzi hapa nilifiwa na baba mkubwa. Kijijini huko Sikonge yalikuwa mazishi makubwa sana hasa ukichukulia ni familia ya Mwanangwa. Hapa JF watu waliendelea na story kama hakikutokea kitu. Hata ningeliandika hapa, kuna mtu angelishituka? Zingeliandikwa POLE kadhaa na mchezo ukaisha. Ni tofauti hata tukisema "fulani wa JF" kauguwa kwani ni watu ambao ingawa simfahamu, ukweli ni kuwa ameshakuwa karibu na mimi kwa siku nyingi sasa.
Huyu dada na yeye tumeshakuwa naye kwenye nyumba zetu mara kadhaa. Tumemuona na kusoma habari zake kwenye magazeti. Utake usitake ameshakuwa karibu yetu sisi ingawa yeye hatufahamu. Si yeye tu ila hata hapa Tanzania wapo wengi tu kama marehemu Gama (nilipata bahati ya kumuona na kama RC namshukuru sana kwani kuanzia niliposikia kahamishiwa Tabora, nilifahamu kuwa ataubadilisha Mkoa, na kweli. Nakumbuka kumuona wakisalimiana na Meja Odo wa Msange JKT wakati nikiwa JKT TAbora). Watu kama Amina Chifupa, Sokoine, Nyerere, James mwana wa Dandu, Ramadhani Lenny, School mates wangu Method Mogela na Salehe Sonda (wote wa Simba S.C.), Said Mwamba Kizota (homeboy), na wengine wengi.
Sasa wewe unataka niwalilie watu wa Mbeya ambao hata sijawahi kuwasikia? Umenikumbusha ugomvi wa marehemu shangazi na marehemu baba. Kuna babu yetu sijui kivipi kwenye ukoo alihamia Mwanza na kufika huko akaowa mwanamke fulani na yule mama akafariki. Baba alisikia na akakaa kimya. Shangazi alipokuja kupata habari na yeye na kukuta kumbe kaka yake aliambiwa na hakusema akaja juu kwa Mzee kuwa kwa nini hakuambiwa. Baba akasema ehh, kwani ulikuwa unamfahamu? Shangazi kakaa kimya na ghafla akaruka na kusema "sasa itabidi tufanye msiba". Mzee alimjibu hivi: "kama unapenda sana kulilia watu, redio hiyo na ikifika jioni kuna matangazo ya vifo, chagua mmoja ambaye kifo chake au jina lake umelipenda na UMLILIE".
Mkuu Bluray, kama wa Mbeya waliokufa kwa matetemeko wamekuuma sana, unaweza walilia au hata kujinyima mshahara wako wa mwezi mmoja na uwapelekee na hapo utakuwa umefanya jambo la maana. Sanasana ni kuwa JF kama kawaida, tutakuja na pole na RIP kibao na mwisho wa siku kila mtu anaenda kulala kwake na kusahau. Anyway, ndiyo uzuri wa forrum, ni kubwa saana, na kuna topic kibao unazoweza kuzisoma na kuzichangia. Na uzuri kichwa cha habari kimewekwa wazi na unapoingia unafahamu kabisa unaingia mlango upi. Kama ni wa choo na wewe ulitaka kwenda wa hotel, hapo si kosa letu tena na hakuna tunachoweza kukusaidia ili usiingie kwenye topic zenye kichwa cha habari kilicho wazi na wewe Bado unazamia na ukizamia unapata kichefuchefu...........
I take it either unawapenda sana unaowaona kwenye TV au unapenda kulilia watu.
Or possibly both.
This is exactly the plague that is clogging the machinery of JF.
Mbona unajicontradict urself???mara wewe sio mbongo then unaleta story za kwenu kijijini!!!!!mara school mates zako!!!au wewe ni mkimbizi???
Kweli nyani haoni ................
Hata yule anayesema nyani haoni .... anaweza kuwa haoni ....
![]()
Where by X = nyani (c) + Nyani (d).
Merry X-Mas and Happy New Year.
Looping ad infinitum in a groundhog day.