Ada ya mja hunena uungwana ni vitendo, kwa hili la Simba mimi Yanga wacha tu niseme

Ada ya mja hunena uungwana ni vitendo, kwa hili la Simba mimi Yanga wacha tu niseme

Komeo Lachuma

JF-Expert Member
Joined
Oct 31, 2014
Posts
7,926
Reaction score
17,030
Kawaida yetu watanzania ni fitina, chuki, husda na unafiki.

Leo najitia katika sifa hizo. Simba mmeonesha kitu ambacho Yanga tunapaswa pia kuiga. Najua Yanga wenzangu hili litawakera. Acha mi niseme. Sipendi kuwa mnafiki na kwenda kusemea chooni Mfalme ana masikio ya punda.

Yanga tunawekeza sana kwenye propaganda. Sana kwenye vyombo vya habari na wacha-mbuzi. Pia kuna kipindi tunanunua matches. Najua hili hamtalipenda mi napasua jipu. Si tunataka kupona?

Tucheze mpira bila kelele. Tucheze mpira Uwanjani. Sisi tulipo sasa. Simba walishatoka huko. Ndito maana huoni wakipiga sana kelele. Huoni wakisifiwa hata kwenye ujinga. Sisi tunadekezwa na kujidekeza sana.

Sikutegemea Simba wangekuwa na utulivu waliokuwa nao Angola. Tuna la kujifunza. Simba wanapokuwa na mapungufu hukubali wanayo. Sisi hatukubali na wakati mwingine tunamtafuta wa kumwangushia jumba bofu. TFF.

Tumebaki na madeko tu timu yetu inafanya vizuri mechi za ndani sababu timu zetu hizi tunazifahamu, njaa pamoja na marefa wetu.

Tukaze msuli. Simba tunawanoa sisi wenyewe. Sisi tunapambana sana kuifunga Simba. Simba inachukulia mechi yetu kama mechi nyingine yoyote. Ndiyo maana kwao kwa sasa kutufunga au kufungwa nasi si ishu kubwa.

MIMI NIMESEMA. KAMA UTATOKWA NA POVU LITOE TU.

NIMEKAA PALE 👉
 
Kojoa Kisha lala bhan ,bado tuna nafsi kdg hakika yanga wametizama mpira wa Simba leo nadhni hawatatuangusha ugenini

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
 
Siku ushahidi wa kununi mechi ukiletwa hadharani ndo ntaamini hizi porojo.

Hivi Yanga wananunua mechi kwa kombe la 100m +500m za Azam na huku bajeti ya mishahara na matumizi mengine kwa mwezi ni 400m!! Hivi nani anafanya biashara kichaa namna hii? Atoe Hela ambayo hajui inarudije?

Unaposema Yanga hawakubali mapungufu yao ?? Wakati kila mwana Yanga toka msimu huu unaanza alikua anajua timu inamapungufu kwenye beki na kiungo wa chini ( namba 6)

Kinachoiponza Yanga ni kukosa uzoefu wa namna ya kucheza michuoano ya CAF na kutoheshimu wapinzani wao.

Wewe ndo umeleta propaganda
 
IMG_20221009_220010.jpg
 
Bora umeyasema haya..tulikuwa tunakutafuta kule kwenye Uzi wako wa awali
 
Hongera kwakuliona hilo. Kuna mwenzako mechi ya ndani kati ya Simba na Dodoma jiji alisema Simba ikiifunga Dodoma jiji aitwe ASHURA. Naona yupo kimya mpaka sasa huyo Ashura kitu ambacho si kawaida yake.
 
Kawaida yetu watanzania ni fitina,chuki,husda na unafiki.

Leo najitia katika sifa hizo. Simba mmeonesha kitu ambacho Yanga tunapaswa pia kuiga. Najua Yanga wenzangu hili litawakera. Acha mi niseme. Sipendi kuwa mnafiki na kwenda kusemea chooni mfalme ana masikio ya punda.

Yanga tunawekeza sana kwenye propaganda. Sana kwenye vyombo vya habari na wacha-mbuzi. Pia kuna kipindi tunanunua matches. Najua hili hamtalipenda mi napasua jipu. Si tunataka kupona?

Tucheze mpira bila kelele. Tucheze mpira Uwanjani. Sisi tulipo sasa. Simba walishatoka huko. Ndo maana huoni wakipiga sana kelele. Huoni wakisifiwa hata kwenye ujinga. Sisi tunadekezwa na kujidekeza sana.

Sikutegemea Simba wangekuwa na utulivu waliokuwa nao Angola. Tuna la kujifunza. Simba wanapokuwa na mapungufu hukubali wanayo. Sisi hatukubali na wakati mwingine tunamtafuta wa kumwangushia jumba bofu. TFF. tumebaki na madeko tu team yetu inafanya vizuri matches za ndani sababu teams zetu hizi tunazifahamu njaa pamoja na marefa wetu.

Tukaze msuli. Simba tunawanoa sisi wenyewe. Sisi tunapambana sana kuifunga Simba. Simba inachukulia match yetu kama match nyingine yoyote. Ndo maana kwao kwa sasa kutufunga au kufungwa nasi si issue kubwa.


MIMI NIMESEMA. KAMA UTATOKWA NA POVU LITOE TU.


NIMEKAA PALE 👉
1665344807162.png
 
Back
Top Bottom