Ada ya saini na mihuri ya wanasheria

Muadilifu

Senior Member
Joined
Sep 26, 2007
Posts
149
Reaction score
23
Wakuu naombeni msaada kidogo kuhusu haya malipo wanayodai wanasheria pindi unapopeleka nyaraka zako waziidhinishe. Hivi, sheria inasemaje, ni halali kuwalipa kwa kazi hiyo, na kama ni halali ni shilingi ngapi wanatakiwa kulipwa kisheria. Manake kuna wakati nilipeleka fomu zangu mahakamani zisainiwe na kugongwa muhuri, Karani wa mahakama akanipokea na kuniambia nmpe Shilingi 15, kwa kuwa ada ya kira muhuri ni shilingi 5,000. Nilikuwa nahitaji mitatu. Nilipomuomba risiti, akaniambia hiyo mihuri yenyewe ndio risiti tayari, inajitosheleza. Nikashindwa kumbana zaidi. Msaada tafadhali
 
Ungefungua mashtaka ya matumizi mabaya ya ofisi hapo hapo.
Mihuri ya mahakamani ni sh. 500/= na unapewa risiti yako ya njano.
 
Ungefungua mashtaka ya matumizi mabaya ya ofisi hapo hapo.
Mihuri ya mahakamani ni sh. 500/= na unapewa risiti yako ya njano.

Muadilifu anataka kujua Sheria zinazohusika, wewe unamwambia tu afungue mashtaka! Mihuri ya mahakamani ni Sh 500/- kwa Sheria ipi? Tujulishe tafadhali!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…