WomanOfSubstance
JF-Expert Member
- May 30, 2008
- 5,457
- 963
Wana JF,
Nadhani wengi wetu tumeshawahi kukumbwa na mateso au adha na karaha zilizotokana na majaribio ya wanasiasa na viongozi wetu toka tupate uhuru hadi leo. Nadhani kama tungepata wasaa wa kubadilishana uzoefu... basi tungepata mambo mengi sana - machungu, ya kuchekesha na kusikitisha.
Mifano michache ni sera zifuatazo?
1.Azimio la Arusha - Utaifishaji wa mali na njia kuu za uchumi - watu walipoteza mali zao na wengine hata kupatwa magonjwa kama presha n.k
2.Mwongozo - Kiongozi asiwe mnyampala - matokeo yake hakuna aliyejisikia kuwajibika maana kumwajibisha mtu ilikuwa ni unyampara na consequences zake ziliweza kuwa mbaya
3. Vijiji vya ujamaa - nadhani tumeshasoma mengi katika thread ya Dr Kleruu - japo tunahitaji kusikia visa na mikasa zaidi
4.Operesheni Maduka - Watu walilazimishwa kuwa na maduka ya ushirika badala ya maduka binafsi
5. Azimio la Musoma - Vijana walitakiwa kufanya kazi miaka miwili kwanza baada ya kidato cha sita ikabla ya kujiunga na chuo kikuu - na ilibidi upate barua kutoka tawi la chama na anayekuandikia barua hiyo pengine hata hajawahi kumaliza darasa la saba!
6.Operesheni kuondoa nguo fupi, nguo za kubana, kuvaa mawigi n.k. Hii nimesahau ilikuwa inaitwaje kwa usahihi
7.Nguvu Kazi -
8.Uhujumu uchumi
Na nyingine nyingi.
Nadhani wengi wetu tumeshawahi kukumbwa na mateso au adha na karaha zilizotokana na majaribio ya wanasiasa na viongozi wetu toka tupate uhuru hadi leo. Nadhani kama tungepata wasaa wa kubadilishana uzoefu... basi tungepata mambo mengi sana - machungu, ya kuchekesha na kusikitisha.
Mifano michache ni sera zifuatazo?
1.Azimio la Arusha - Utaifishaji wa mali na njia kuu za uchumi - watu walipoteza mali zao na wengine hata kupatwa magonjwa kama presha n.k
2.Mwongozo - Kiongozi asiwe mnyampala - matokeo yake hakuna aliyejisikia kuwajibika maana kumwajibisha mtu ilikuwa ni unyampara na consequences zake ziliweza kuwa mbaya
3. Vijiji vya ujamaa - nadhani tumeshasoma mengi katika thread ya Dr Kleruu - japo tunahitaji kusikia visa na mikasa zaidi
4.Operesheni Maduka - Watu walilazimishwa kuwa na maduka ya ushirika badala ya maduka binafsi
5. Azimio la Musoma - Vijana walitakiwa kufanya kazi miaka miwili kwanza baada ya kidato cha sita ikabla ya kujiunga na chuo kikuu - na ilibidi upate barua kutoka tawi la chama na anayekuandikia barua hiyo pengine hata hajawahi kumaliza darasa la saba!
6.Operesheni kuondoa nguo fupi, nguo za kubana, kuvaa mawigi n.k. Hii nimesahau ilikuwa inaitwaje kwa usahihi
7.Nguvu Kazi -
8.Uhujumu uchumi
Na nyingine nyingi.