KakaKiiza
JF-Expert Member
- Feb 16, 2010
- 11,794
- 9,075
TANROADS, SUMATRA, TRAFFIC, ADHABU YA SPIDI HAIKUBALIKI KABISA.
Waraka wa BASHIR YAKUB
+255784482959.
Traffic 30,000, Sumatra 80,000, Tanroads 90,000 =200,000 Tshs. Ni adhabu ya kosa moja tu la kukiuka spidi iliyokubaliwa.Ni taarifa iliyoenea mtandaoni kwa sasa. Ni kuwa kosa moja tu la spidi kila mamlaka kati ya hizo hapo juu itakutoza faini iliyoainishwa.
Binafsi nimeshuhudia risiti ya malipo ya Tanroads ikiwa imetoza kiwango hicho. SWALI ni kama jambo hilo linakubalika kisheria.
1. DOUBLE JEOPARDY.
Hii ni kanuni kati ya kanuni za kisheria za Misingi ya Haki za Asili "Principle of Natural Justice". Ni kanuni inayokataza kabisa kabisa kosa moja kuadhibiwa zaidi ya mara moja.
Tuone DUNIA inasemaje kuhusu Double jeopardy.
a ) HAPA TANZANIA.
Kifungu cha 21 cha Kanuni za Adhabu (Penal Code) kinasema kuwa mtu hataadhibiwa mara mbili au zaidi kwa kosa moja alilofanya chini ya Sheria yoyote.
Maana ya maneno "Sheria yoyote" ktk hicho kifungu ni kuwa, iwe ya usalama barabarani, ya Tanroads au Sumatra , mtu akishaadhibiwa kwa sheria mojawapo kati ya hizo inatosha.Ni mara moja tu.
Pili, Sheria ya Tafsiri za Sheria(The Interpretation of Laws Act), Sura ya kwanza , kifungu cha 70 kinasema, ............. kwa kosa moja, mtu ataadhibiwa mara moja tu.
b ). AFRIKA MASHARIKI.
Kenya. Katiba yao ibara ya 50(2)(o) inasema kuwa itakuwa ni makosa chini ya katiba na Sheria nyingine kwa mtu kuadhibiwa zaidi ya maramoja kwa kosa moja. Ibara hii inasomwa na Sheria ya Mwenendo wa Kesi za Jinai vifungu vya 138- 142 .
Uganda. Kanuni za Adhabu , kifungu cha 21 kinasema kuwa kwa kila kosa , mtenda kosa ataadhibiwa mara moja tu.
C ) . AMERIKA.
Usa. Katika kesi ya Bentom vs Maryland, 395, US 784(1969), mahakama ya juu iliitaja "double jeopardy" yaani mtu kuadhibiwa mara mbili au zaidi kwa kosa moja kama ukandamizaji wa kiwango cha juu kabisa wa haki.
d ). UMOJA WA ULAYA.
Mkataba wa Umoja wa Ulaya wa Haki za binadamu( European Convention on Human Rights) , Ibara ya 4 inasema kuwa, hakuna mtu akayeadhibiwa na dola kwa kosa ambalo tayari ameshakutwa nalo hatia na kutumikia adhabu ya kosa hilo.
e ). MKATABA WA KIMATAIFA WA HAKI ZA KISIASA NA KIRAIA.
Unaitwa "International Covenant on Civil and Political Rights". Tanzania imesaini mkataba huu. Ibara yake ya 14(7) inasema kuwa, hakuna mtu atakayeadhibiwa tena kwa kosa lilelile baada ya kuwa ameadhibiwa kwa taratibu za kisheria za nchi yake.
2. MAKOSA KATIKA ADHABU HII.
Adhabu tatu si tu kosa la kawaida bali pia lililokiuka kabisa kabisa haki za binadamu. Kwa namna yoyote ilivyo kosa moja katu haliwezi kuadhibiwa mara tatu na mamlaka tatu tofauti. Abadan
Sheria zote za ndani na zile za kimataifa zimekataa na sisi pia hatutakubali. Double jeopardy ni kosa duniani kote na Tanzania.
Tunakemea mwendo kasi na mwendo uliokiuka taratibu za barabara husika, lakini tunakemea zaidi ukiukwaji wa sheria na haki za binadamu katika kushughulikia jambo hilo.
3. NASAHA
Lazima iwepo adhabu moja inayotolewa na mamlaka moja. Na adhabu hiyo iwe ya kukadirika(reasonable) na sio ya kukomoa au kulenga kuongeza mapato ya mamlaka/biashara.
Tumezoea ile ya 30,000 ya traffick nadhani inatosha na ni ya kukadirika. Pia imesaidia sana kwani sasa vibao vya spidi vinazingatiwa sana na madereva.
Inawezakana Tanroads na Sumatra mna mpangio wa kuongeza makusanyo/mapato. Na iwe hivyo lakini sio kwa kuvunja Sheria na kuonea Watanzania. Hili hatutakubali.
Samsung SH 8 Mobile Traveller
Waraka wa BASHIR YAKUB
+255784482959.
Traffic 30,000, Sumatra 80,000, Tanroads 90,000 =200,000 Tshs. Ni adhabu ya kosa moja tu la kukiuka spidi iliyokubaliwa.Ni taarifa iliyoenea mtandaoni kwa sasa. Ni kuwa kosa moja tu la spidi kila mamlaka kati ya hizo hapo juu itakutoza faini iliyoainishwa.
Binafsi nimeshuhudia risiti ya malipo ya Tanroads ikiwa imetoza kiwango hicho. SWALI ni kama jambo hilo linakubalika kisheria.
1. DOUBLE JEOPARDY.
Hii ni kanuni kati ya kanuni za kisheria za Misingi ya Haki za Asili "Principle of Natural Justice". Ni kanuni inayokataza kabisa kabisa kosa moja kuadhibiwa zaidi ya mara moja.
Tuone DUNIA inasemaje kuhusu Double jeopardy.
a ) HAPA TANZANIA.
Kifungu cha 21 cha Kanuni za Adhabu (Penal Code) kinasema kuwa mtu hataadhibiwa mara mbili au zaidi kwa kosa moja alilofanya chini ya Sheria yoyote.
Maana ya maneno "Sheria yoyote" ktk hicho kifungu ni kuwa, iwe ya usalama barabarani, ya Tanroads au Sumatra , mtu akishaadhibiwa kwa sheria mojawapo kati ya hizo inatosha.Ni mara moja tu.
Pili, Sheria ya Tafsiri za Sheria(The Interpretation of Laws Act), Sura ya kwanza , kifungu cha 70 kinasema, ............. kwa kosa moja, mtu ataadhibiwa mara moja tu.
b ). AFRIKA MASHARIKI.
Kenya. Katiba yao ibara ya 50(2)(o) inasema kuwa itakuwa ni makosa chini ya katiba na Sheria nyingine kwa mtu kuadhibiwa zaidi ya maramoja kwa kosa moja. Ibara hii inasomwa na Sheria ya Mwenendo wa Kesi za Jinai vifungu vya 138- 142 .
Uganda. Kanuni za Adhabu , kifungu cha 21 kinasema kuwa kwa kila kosa , mtenda kosa ataadhibiwa mara moja tu.
C ) . AMERIKA.
Usa. Katika kesi ya Bentom vs Maryland, 395, US 784(1969), mahakama ya juu iliitaja "double jeopardy" yaani mtu kuadhibiwa mara mbili au zaidi kwa kosa moja kama ukandamizaji wa kiwango cha juu kabisa wa haki.
d ). UMOJA WA ULAYA.
Mkataba wa Umoja wa Ulaya wa Haki za binadamu( European Convention on Human Rights) , Ibara ya 4 inasema kuwa, hakuna mtu akayeadhibiwa na dola kwa kosa ambalo tayari ameshakutwa nalo hatia na kutumikia adhabu ya kosa hilo.
e ). MKATABA WA KIMATAIFA WA HAKI ZA KISIASA NA KIRAIA.
Unaitwa "International Covenant on Civil and Political Rights". Tanzania imesaini mkataba huu. Ibara yake ya 14(7) inasema kuwa, hakuna mtu atakayeadhibiwa tena kwa kosa lilelile baada ya kuwa ameadhibiwa kwa taratibu za kisheria za nchi yake.
2. MAKOSA KATIKA ADHABU HII.
Adhabu tatu si tu kosa la kawaida bali pia lililokiuka kabisa kabisa haki za binadamu. Kwa namna yoyote ilivyo kosa moja katu haliwezi kuadhibiwa mara tatu na mamlaka tatu tofauti. Abadan
Sheria zote za ndani na zile za kimataifa zimekataa na sisi pia hatutakubali. Double jeopardy ni kosa duniani kote na Tanzania.
Tunakemea mwendo kasi na mwendo uliokiuka taratibu za barabara husika, lakini tunakemea zaidi ukiukwaji wa sheria na haki za binadamu katika kushughulikia jambo hilo.
3. NASAHA
Lazima iwepo adhabu moja inayotolewa na mamlaka moja. Na adhabu hiyo iwe ya kukadirika(reasonable) na sio ya kukomoa au kulenga kuongeza mapato ya mamlaka/biashara.
Tumezoea ile ya 30,000 ya traffick nadhani inatosha na ni ya kukadirika. Pia imesaidia sana kwani sasa vibao vya spidi vinazingatiwa sana na madereva.
Inawezakana Tanroads na Sumatra mna mpangio wa kuongeza makusanyo/mapato. Na iwe hivyo lakini sio kwa kuvunja Sheria na kuonea Watanzania. Hili hatutakubali.
Samsung SH 8 Mobile Traveller