mwanamwana
JF-Expert Member
- Aug 1, 2011
- 1,309
- 4,798
Katibu Mkuu wa ACT Wazalendo, ndugu Ado Shaibu amejibu kauli ya Ally Hapi kuwa Dola iwashughulikie wanaotaka kuzuia uchaguzi, ambapo amesema kuwa CCM siyo chama cha siasa tena, kwasababu sifa ya chama cha siasa ni lazima kiwe na uwezo wa kuleta ushindani.
CCM hii ya sasa siyo ile tuliyokuwa tunaijua zamani, ambayo kwenye baadhi ya maeneo kweli ulikuwa unashindana nayo. Kuna maeneo CCM ni dhaifu sana, na kuna maeneo unaona kabisa unashindana nayo, ile CCM haipo kwa mujibu wa Halmashauri kuu.
Kupata taarifa na matukio ya kimkoa kuhusu Uchaguzi Serikali za Mitaa ingia hapa: LGE2024 - Special Thread: Orodha ya Mijadala ya Mikoa yote Tanzania Bara inayoshiriki katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024
Sasa hatupambani na CCM, tunapambana na dola. Utofauti wa zamani na wa sasa ni kwamba zamani CCM ilikuwa inatumia dola ili kuweza kuiba uchaguzi. Hali ya sasa ni Dola inaitumia CCM kuiba uchaguzi.
CCM wenyewe kwenye baadhi ya maeneo hawajui uchaguzi uliibwaje, wanaweza wakajua kulikuwa kuna hili na lile, na uchaguzi wa leo huwezi ukasikia eti uchaguzi unashangiliwa. Dola inaipa CCM asilimia hadi wenyewe wanahangaa, wenyewe hawajui.
Kwa hiyo Ally Hapi akisema dola iwashughulikie, sisi tayari tunajua adui yetu tunayepambana naye, atakayekuwa anapanga kutushughulikia, na sisi tunajipanga kukabiliana naye ni Dola.
Pia soma > LGE2024 - ACT Wazalendo: Vyombo vya Dola vilitumika kuweka kura bandia kwenye maboksi ya kura
CCM hii ya sasa siyo ile tuliyokuwa tunaijua zamani, ambayo kwenye baadhi ya maeneo kweli ulikuwa unashindana nayo. Kuna maeneo CCM ni dhaifu sana, na kuna maeneo unaona kabisa unashindana nayo, ile CCM haipo kwa mujibu wa Halmashauri kuu.
Kupata taarifa na matukio ya kimkoa kuhusu Uchaguzi Serikali za Mitaa ingia hapa: LGE2024 - Special Thread: Orodha ya Mijadala ya Mikoa yote Tanzania Bara inayoshiriki katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024
Sasa hatupambani na CCM, tunapambana na dola. Utofauti wa zamani na wa sasa ni kwamba zamani CCM ilikuwa inatumia dola ili kuweza kuiba uchaguzi. Hali ya sasa ni Dola inaitumia CCM kuiba uchaguzi.
CCM wenyewe kwenye baadhi ya maeneo hawajui uchaguzi uliibwaje, wanaweza wakajua kulikuwa kuna hili na lile, na uchaguzi wa leo huwezi ukasikia eti uchaguzi unashangiliwa. Dola inaipa CCM asilimia hadi wenyewe wanahangaa, wenyewe hawajui.
Kwa hiyo Ally Hapi akisema dola iwashughulikie, sisi tayari tunajua adui yetu tunayepambana naye, atakayekuwa anapanga kutushughulikia, na sisi tunajipanga kukabiliana naye ni Dola.
Pia soma > LGE2024 - ACT Wazalendo: Vyombo vya Dola vilitumika kuweka kura bandia kwenye maboksi ya kura