Nakushauri Soma Kichina.
Maana soko sio hoja,ila inatakiwa soko lenye kudum.
China ndio inaongoza kuwekeza humu nchini,sasa wachina Kiingereza ni tatizo kwao.Licha ya kwamba wao wakija hapa inaboidi wajifunze kiswahili kwakuwa Tanzania haikuwa na record nzuri ya wanaoongea Kichina.
Mfano mmoja tu nikupe,kwenye Utalii,kama kuna Tour Guide anaongea Lugha ya Kichina basi pesa yake anaelipwa ni ndefu saaana kulinganisha na anaeongea kifaranza au kiitaliano.Na pia wachina wanatoa ajira kwa wenyekujua lugha yao na wanapenda sana ukiwa mtanzania unajua kuongea Kichina.
Leo hii nikikuambia nitafutie watu watatu wenye kujua kichina utakesha,ila nikikuambia wanaojua kifaransa utaniletea teleee,maana Alliance Francie wanatoa watu na Kijerumani pale GOETHE institute nao wanazalisha.
Lugha ngum ndio yenye maslahi,ila hakuna lugha nyepesi wala ngum,hii inategemea na nia yako.
Ukiona kichina Kigum,basi soma Ki Spaniola.
Ila tambua kwamba ndani ya mwaka utakuwa upo kwenye basic tu,maana usiwe na expectations kwamba mwaka mmoja ukimaliza unakuwa unajua lugha,na ndio maana kiingereza watu wanadima hadi wanaingai chuo bado hakijaunga cha kupambana na maisha kipo tu cha kujibia mitihani.