Afande sele a.K.A Simba Mzee mwenye meno makali, mkali wa mashairi kutoka mji kasoro bahari..

Afande sele a.K.A Simba Mzee mwenye meno makali, mkali wa mashairi kutoka mji kasoro bahari..

ukwaju_wa_ kitambo

Senior Member
Joined
Sep 15, 2024
Posts
150
Reaction score
173
UKWELI HIPHOP IMEKUFA?

Najiuliza NA kujipa majibu mepesi japo swali ni gumu sana!

MONI CENTROZONE Anasema "HIPHOP is DEAD" lakini sijaona vijana wa new school kama wanamjibu au tuseme wako bize na Amapiano?

Swali jingine "Je ni kweli hayupo mfalme wa rhymes mwingine mpaka leo zaidi ya MFALME SELEMANI?

Ninaomba jibu ni yupi anaweza pewa U-King huu tena?

AFANDE SELE - MIAKA 10.

Intro ..

Oooh miaka 10 imefika ya mfalume mimi imepita viumbe wanakuja wanazaliwa wanakufa wanaondoka shwaa!! Dunia hudumu Daima weweee!!
Chuki ya nani? usinitanie..

Verse 1.

Sasa ni miaka 10 Tangu niwe mfalume/ lakini Bado ni mimi ndio ninayeimarisha Ngome/ simba Dume najiamini na amini kwenye fani na waumini/ wanaoamini kile ninachofanya mimi/Hapa chini ni madini hata kama hayachibwi chini/ yanachibwa kichwani na mchibaji namba one bwana msindi suleimani/ fundi wa vina mizani kutoka mji kasoro pwani/ niliaza kitambo kwa kuonyesha tofauti ya mwanajeshi na mgambo"sure"/ kwa kufanya mambo kutunga sana nyimbo/ zenye ujumbe kwa mafumbo na vijembe/zikapendwa na warembo na masela kila pembe zikavuka mpaka ng'ambo/ wakaniita nikaimbe muziki wangu ukawa nembo/ nyumbani ukaleta sembe ukaleta ugali miwali mikachumbali/ na ukanipa mwana mwali sajali na watoto wawili/ nikaaza kuvaa viatu badala ya kandambili/ kuwa na pear mbili tatu ikawa tena sio habari sio stori/Kweli maisha ni safari muziki ni kama bahari/ mashairi yangu ndio meli na mimi kama msafiri/ tayari nimeshakiri pamoja na ukweli ya kwamba mimi ni mkali/wa kuandika haya mashairi amini bado sijawahi/ kupata tuzo ya dili/ lakini sio hatari mwakani nita change style/ nami nimwimbie Daring ni mlilie sana sheri/ au nisifie suruali ilimradi tu na mie nipate tuzo hata mbili/ labda vingezo wa badili au vip kadinali/ooh mwanangu!

Chorus...

Yes Believe kumbe wapo wale wanaopenda mimi nipotee/

Am still the king Bado nipo Eeeh!!/ × 2

Yes Believe Bado nipo

Yes blieve Bado nipo × 3

Verse ..2..

Miaka 10 tangu nipate u king/ ni mingi pia sio mingi/ kwa vile bado naandika mambo mengi/tu ya msingi/mtaani hawanipigi wanaamin mimi ndio king/wa ma king/ wananipa heshima nyingi miaka mingi/ ingawa sina shilingi/ nyingi nyingi japokuwa ni msanii wa long/ najiuliza mara nyingi wapi nilikuwa kingiki/ nilipokosea timeming/ sijui ni yule shangigi mitungi au mibangi/ sielewi nilipo bungi ama kupenda mabungi/ kwani ni nani hapendangi labda kama afande bungi/kwani jongoo kwani hawikaki/ mpaka majike hayatangi/ hatuzungi hata kujingi tutamchinja hatumfuki/ na kumdosa kwenye ligi/ ameshiriki miaka mingi lakini kombe Hapataki/ amani kwa soggy doggy rafiki yangu wa long/ alo amini game alinongi pasipo kumdisi king/ kafanya ndio kata logi wakati chuki hazichengi/ kwa mfano 2 pac na biggie wasinge ngombea u king/ kama D.r.e na snoop doggy uwenda leo tungekuwa nao/ japo wangeshakuwa mading "sure"/ lakini bado wange blling wange shine/ ndani ya ring na zaidi wangeshuhudia kutimia kwa ndoto ya luther king/ mweusi kuingia white house kama raisi"obama" nyani mweusi kuitawala amerika...

Chorus..

Yes Believe kumbe wapo wale wanaopenda mimi nipotee/

Am still the king Bado nipo Eeeh!!/ × 2

Yes Believe Bado nipo

Yes blieve Bado nipo × 3

Autro..

Yeh... Kadinali official official miaka 10 ya king wa ryhems king Sele king of king ever and ever mfalume wanaume tukutane tena tushikamane tuishi Eneo letu
Studio record..

Like page yetu Facebook ya UKWAJU WA KITAMBO
Mawasiliano +255767542202
 

Attachments

  • images-3.jpg
    images-3.jpg
    21.4 KB · Views: 6
Sio mwingine
simba dume
Hatoki kwingine
Chimbo Moro mtu pori mwenye mikuki na sime kumiliki mamlaka Hana budi
Ye ndio mfalme
Mkononi ana nyaraka bado anaimarisha Ng'ombe
Amesimama yupo wima mtu mzima
Na kama anasema kitu wengine wanabakia kimyaaa..............


Maskini hafilisiki
 
Ila Afande Sele sio msanii wa hip hop bali Bongo Fleva.
Afande sele ukipenda mzungu wa roho/ na ukipenda baba Tunda,/ ntawakilisha Moro kila pembe nnavyokwenda/ ntatukuza mazuri na mabaya ntayaponda/ mfano kuhusu kilimo Cha mbogamboga matunda/ama kuhusu michezo haswa mpira wa kandanda/Moro inafanya kweli miaka rudi miaka nenda/ukitazama muziki Morogoro ndio nyumbani/ ilianza kushika chati miaka mingi hapo zamani/ enzi za mziki wa dansi ulipovuma kama upepo/ na sisi mpaka sasa tunatesa kwenye hip-hop..

Nyimbo inaitwa " morogoro " ametaja mwenyewe kabisa anachofanya ama kuimba ni muziki aina ya hip hop
 
Afande sele ukipenda mzungu wa roho/ na ukipenda baba Tunda,/ ntawakilisha Moro kila pembe nnavyokwenda/ ntatukuza mazuri na mabaya ntayaponda/ mfano kuhusu kilimo Cha mbogamboga matunda/ama kuhusu michezo haswa mpira wa kandanda/Moro inafanya kweli miaka rudi miaka nenda/ukitazama muziki Morogoro ndio nyumbani/ ilianza kushika chati miaka mingi hapo zamani/ enzi za mziki wa dansi ulipovuma kama upepo/ na sisi mpaka sasa tunatesa kwenye hip-hop..

Nyimbo inaitwa " morogoro " ametaja mwenyewe kabisa anachofanya ama kuimba ni muziki aina ya hip hop
Afande ni Msanii mkali lakini kusema kwamba ndo legend wa hip-hop n uongo wa wazi itoshe kusema n Msanii mkali wa bongo flavor
 
Back
Top Bottom