Afariki akijaribu kuiba nyaya za umeme

KJ07

JF-Expert Member
Joined
Dec 17, 2021
Posts
2,370
Reaction score
5,381
#HABARI Kijana mmoja aliyefahamika kwa jina la Adamu Assan (30) mkazi wa Mafichoni Kiteto amepoteza maisha kwa kupigwa na shoti ya umeme akidaiwa kuwa alikuwa anaiba nyaya za umeme.

Marehemu amekutwa chini ya nguzo za umeme zilizobeba transfoma leo April 06. 2024 eneo la Mnadani Partimbo huku akiwa anaonekana kuunguzwa sehemu ya tumboni na umeme

Kwa mujibu wa Kaimu Kamanda wa Jeshi la Polisi Manyara Lucas Mwakatundu ameeleza kuwa kabla ya kifo hicho kulikuwa na jaribio la kukata nyaya za umeme na kwamba chanzo cha kifo hicho ni kupigwa shoti ya umeme


#EastAfricaTV.
 
Vijana tufanye kazi tuache janjajanja katika utafutaji.

No shortcut katika kutafuta.
 
Tena kakutwa ameungua kwenye tumbo๐Ÿค”
 
Laana ya Biteko
 
Vijana wa ccm hao.
Wasipokuwa Chawa wanakuwa Wezi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn moreโ€ฆ