Mkalukungone mwamba
JF-Expert Member
- Aug 29, 2022
- 862
- 1,755
Serikali imemfikisha katika mahakama ya hakimu mkazi Arusha Afisa mauzo kutoka kampuni ya royal colour paint limited anayejulikana kwa jina la Silvester Charles akikabiliwa na makosa matatu utakatishaji fedha, kutoa risiti zisizo halali za malipo pamoja na kuisababishia mamlaka ya mapato Tanzania TRA hasara ya zaidi ya bilioni moja nukta nane.
Shauri hilo la uhujumi uchumi namba 4593/ 2025 limefikishwa mahakamani hapo kwa mara ya kwanza na mamlaka ya mapato Tanzania TRA.
Soma Pia: Dar: Mafundi wa EFD wafikishwa Mahakamani kwa kuisababishia Serikali hasara ya Tsh. Milioni 954.5
Wakili wa Jamhuri Godfrey Nugu amesema miongoni mwa makosa hayo kotoa risiti zisizo halali au risiti feki za zaidi ya shillingi bilioni moja na milioni mia nane ambapo mshtakiwa huyo alitoa risiti hizo akionesha kuwa kampuni ya royal paint center limited imefanya mauzo ya kiasi hicho .
Shauri hilo la uhujumi uchumi namba 4593/ 2025 limefikishwa mahakamani hapo kwa mara ya kwanza na mamlaka ya mapato Tanzania TRA.
Soma Pia: Dar: Mafundi wa EFD wafikishwa Mahakamani kwa kuisababishia Serikali hasara ya Tsh. Milioni 954.5
Wakili wa Jamhuri Godfrey Nugu amesema miongoni mwa makosa hayo kotoa risiti zisizo halali au risiti feki za zaidi ya shillingi bilioni moja na milioni mia nane ambapo mshtakiwa huyo alitoa risiti hizo akionesha kuwa kampuni ya royal paint center limited imefanya mauzo ya kiasi hicho .