Afisa afya anakuja dukani nakudai vyeti vya afya kwa wauzaji wa dukani

MAPITO Mwanza

JF-Expert Member
Joined
Aug 21, 2018
Posts
4,236
Reaction score
5,907
Mimi ni mjasilia Mali Nina kiduka changu mitaa Fulani hivi Hapa bongo kinauza jumla na lejaleja miaka yote nimefanya sijawahi kukutana na kimbembe nilichokutana nacho

Hivi kalibuni eti afisa afya anakuja dukani nakudai vyeti vya afya kwa wauzaji wa dukani Hebu wenye kujua Juu ya mambo

Haya wanisaidie hili linausawa jamani au nataka kuonewa maana nimeachiwa barua ya wito nifanyeje wana jamii wenzangu?.
 
ni kawaida,maana duka pia ni sehemu ya afya za wateja.

labda huna meza za kuweka vyakula, unachanganya bidhaa za kemikali na vyakula,unauzamo na dawa kuua mende na sumu za panya.

nenda ukiwa vizuri msikilize,atakuelewesha vizuri nini kinatakiwa na kipi hakitakiwi.
 
Nisawa MKUU je hili la vyeti vya afya nalo likoje mkuu hebu nipe ufaham kidogo
 

Mjasilia Mali = Mjasiriamali.
Leja leja = reja reja.
Kalibuni= karibuni.
Hata kama unashindwa kutofautisha r na L wakati wa kuongea jitahidi wakati wa kuandika uandike vizuri.
 
Hiyo ni lazima kama unauza chakula cha binadamu, kwahyo unatakiwa ujue ulikuwa unafanya makosa
 
Mjasilia Mali = Mjasiriamali.
Leja leja = reja reja.
Kalibuni= karibuni.
Hata kama unashindwa kutofautisha r na L wakati wa kuongea jitahidi wakati wa kuandika uandike vizuri.
Haya Mwalimu nimekusoma me nahitaji elimu Juu ya hili nilirolileta hapa
 
Hilo lipo kwenye miongozo tangu zamani za Pontio Pilato sema hawa watu wa afya walikuwa wamelala usingizi. Kikubwa unapoanzisha biashara ni vyema kuisoma miongozo na kuizingatia hata kama jamaa hawafuatilii.

Pole, jiandae Kwa changamoto, ila yapokee mabadiliko Kwa uchanya!
 
Kwangu Mimi na uzoefu niliokua nao sikua najua Kama tunatakiwa kuwa na vyeti vya afya ndugu yangu Sie kina mangi
 
Kwangu Mimi na uzoefu nilikua nao akua najua Kama inatakiwa kuwa na vyeti vya afya ndugu yangu
ndio unakipata baada ya ukaguzi.ambao wewe umefeli hivyo utaanza na fine kwanza,masahihisho kisha cheti.
 

Kama unauza vyakula vilivyopikwa au unauza bidhaa ambazo mhudumu anazishika akiwa amenawa mikono yake na majimaji ambayo yanaweza kusaidia kufanya maambukizi kwa mteja basi wakapime vinginevyo hii itawahusu wafanyakazi wote wa Supermarkets zetu, maduka yote yanayouza unga, maharage, sukari, wauzaji wa magenge wote etc, lakini pia jaribu kuchunguza kama sio biashara yao ya kutunisha pesa za Halmashauri kwani ni hivi juzijuzi mahoteli ya kitalii walipata kukaguliwa na kila mmoja kutozwa faini kwa samaki wao kutokuwa na mhuri wa bwana afya kama mhuri unavyowekwa kwenye nyama ya ng'ombe? la muhimu ni kuwa mwangalifu kwani wao wameshika mpini na kibaya zaidi hao watumishi wametumwa wafanye makusanyo hayo ambayo wakubwa wamekubaliana kwenye vikao halali lakini pia na wao kama binaadamu nao wanachomeka vipengele vya kuwapatia chochote kitu kwani kwenye msafara wa mamba kenge hawakosi
 
Hii imekua mpya kabisa mimi sio mama ntilie Sigara na soda kwenye duka langu ndo vinapatikana rabuda na pipi je hivi vitu ndio vinifanye niwe na cheti cha afya jamani CCM wanatupeleka wapi?
 
Cheti cha afya kinatakiwa kiwepo ofisini kwako kwasababu ww ni mmiliki, ila ningeshangaa kama angeomba cheti cha kidato cha nne. Wengine hawakumaliza hizo kozi wamekimbilia kufungua duka za dawa ndiyo wanaotusumbua mtaani huku.
 
Nenda Nayo Kwa Mkuu wa Magufuli.....
 
Hii imekua mpya kabisa mimi sio mama ntilie Sigara na soda kwenye duka langu ndo vinapatikana rabuda na pipi je hivi vitu ndio vinifanye niwe na cheti cha afya jamani CCM wanatupeleka wapi?

Mkuu tuchukue mfano wa BRELA form TFN 211 kipengele cha 14 kinamuhitaji Afisa wa Afya kutoa mapendekezo yake kwa maombi yote mapya ya Hotel za kawaida,vilabu vya pombe, utengenezaji, uuzaji wa vyakula na vinywaji, sasa linapokuja suala la wahudumu kupima afya zao kila mwaka nafikiri jambo hilo linatakiwa lizingatie mkondo huohuo wa Hotel, vilabu vya Pombe, utengenezaji , uuzaji wa vyakula na vinywaji, lakini pia inabidi uulizie katika Halmashauri yako kama wametunga 'bylaw" zao ili waongeze kipato chao kwani kuuza Sigara na Soda hakufanyi uonekane kuwa unauza chakula
 
kisheria wako sawa,ongea nae vizuri tu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…