AFRICAN BARRICK wamaliza uchimbaji Tulawaka

DOMA

JF-Expert Member
Joined
Mar 17, 2011
Posts
944
Reaction score
366
Jana tarehe 2 kampuni ya African Barrick Gold mine ilifunga operation zake katika mgodi wa tulawaka kati ya migodi mitatu inayomiliki. Migodi iliyobaki ni Buzwagi, bulyakyulu na mgodi wa tarime. Mkurugenzi mkuu wa ABG ameipongeza serikali kwa jinsi ilivyofanikiwa kushirikiana nao katika muda wote wa uchimbaji. Na kwa kuahidi kuendelea kubaki endapo watawaonyesha sehemu nyingine yenye madini ya dhahabu au almas.
ABG wamefunga baada ya madini kuisha katika eneo hilo
source chanel ten
 
Wamesema nini kuhusu kurudisha uoto asilia pale Tulawaka? na kufukia mashimo...

 
Nafikiri ni wakati muafaka kwa serikali sikivu kufanya majumuisho kama tumepata hasara ama faida kutokana na mkataba uo.
 

Mwizi anapoomba aonyeshwe sehemu nyingine yenye mali ili aendelee kuiba!
 
kiruuuuuu?hasara tupu debe tupu ila kuna walioweka sign wamebakia na vijihekalu huko massaki mbezi nadhani ndizo faida za kuwa mwanasiasa..
 
Sasa kama wamemalizi huko si waamie morogoro waanze kuchima Gemstoms....
 

Wamesema nini kuhusu kurudisha uoto asilia pale Tulawaka? na kufukia mashimo...

Mkuu, hapa tz hamna kitu kama hiko.


Waliahidi kurudishia uoto asilia pale. Kwa nini wauchune sasa kuhusu hilo? Tulawaka ipo porini kabisa na kuna mazingira mazuri sana ambayo ingefaa yarudishwe kama asili yake ilivyokuwa. Why the silence?
 
Inhgefurahisha sana kama na wewe ungehamia Mtwara tupambane pamoja, siyo kuwa-support kwa kutumia keyboard tu

Muda best,
But kwenye vita hua kuna wapanga mikakati na wale walioko front line kwenye "battle field", so bado tupo pamoja sana Mkuu wangu @fp
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…