African Champions League Final: TP Mazembe Vs USMA - Nov 8, 2015

bato

JF-Expert Member
Joined
Dec 20, 2012
Posts
3,961
Reaction score
3,466
Watanzania wawili M.Samatta na T.Ulimwengu wanaochezea TP Mazembe jioni ya leo wataweka historia katika ulimwengu wa soka.

Ni katika mchezo wa pili wa fainali kuwania kombe la ligi ya mabingwa Afrika utakaochezwa jijini Lumbumbashi,DRC,Kati ya TP Mazembe(DRC) Vs USM Alger(Algeria).

Mchezo wa kwanza wa fainali uliofanyika Algeria,Oct31,2015 TP Mazembe walishinda 1-2 Mtanzania,Samatta akitupia goli la ushindi 79' kwa penalti.

Samatta mwenye mabao 7 ana nafasi ya kuibukia mfungaji bora wa michuano hiyo. Amelingana mabao na Bakri Al-Madina(El Merreikh-Sudan) ambaye timu yake imeshatolewa.

MUHIMU: Mchezo huu utaonyeshwa Live na TBC 1 kuanzia saa 10.30 jioni(4.30pm) 08/11/3015

Full Time: TP Mazembe vs USM Alger (2-0)

TP Mazembe wamefanikiwa kuchukua kombe la African Champions League baada ya kushinda kwa jumla ya magoli 4 - 1.




 

Attachments

  • 1.jpg
    22.3 KB · Views: 5,079
  • 2.jpg
    23.5 KB · Views: 577
Last edited by a moderator:
...

...bana ba Nzambe igweee !!!!

hapa leo kuprimuzika tuuu....

 
Ni bahati kwangu kuwangalia Hawa watu wawili,
 
Ivi TBC1 ni hii ya Tanzania mbona hawaoneshi?
 

mkuu kwa tangazo lako nipo tbc lkn naona wana yao
 
Hawa TBC bora waache kazi ya broadcasting industry..... Hawapo serious kabisa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…