African leadership prize withheld

Chagua jibu sahihi:
A. Mbeki
B. Kuffor
C. Obasanjo.

Wanatofautiana majina, ila wanafana...uanaharakati wao ulikuwa ni waku-copy.

Bravo Mo-Ibrahim's Prize Commitee, vema na haki...sio tuzo ya kifisadi. Ingekuwa bongo wangempa dad-BM
 
Hapana mkuu,

Kitendo cha kuambiwa kuwa kwa mzima wa 2008 Afrika haikuwa na rais aliyetimiza vigezo vya kuwa kiongozi bora siyo cha kufanyia mzaha. Kwa hiyo wale wote wanaosifiwa sifiwa na kukenua meno sasa wanaweza kujiona wana-rank wapi!

Mkuu Dark city
issue ni kwamba kuna viongozi wengine pamoja na uvundo wao bado wanasifiwa na maraisi wa mataifa makubwa ..mfano na utumbo wote unaoendelea chini yake JK leo inawezekana anajihisi ni kiongozi bora na akistaafu hatapata tunzo ya Mo Abraham lakini atatoka na kichwa kikubwa kwa sababu Bush, Obama wame mfagilia...
 
Congo;620750]Sio kweli hata kidogo. Simjui baba yako, lakini rejea mapungufu ya baba yako.



Mkuu ni mtazamo wako tu. Hivi wewe unaweza kuwa na urafiki na jambazi kama wewe siyo mshirika? Unaweza kuwakumbatia mafisadi kama wewe siyo mshirika wao? Just food for thought!

Je, wewe uko tayari kubebeshwa mapungufu hayo kama huna?

Siko tayari. Ndiyo maana nasema kuwa nitajihadhari na kuwa bali naye kwenye yale katika mambo yake ambayo yeye anayafanya na mimi sikubaliani naye! You are either with them or gainst them. Wewe unaonaje?
 

Huo ni mchezo wa kawaida katika maisha. Ni kama vile ambavyo lazima mwanamume atamwambia binti kuwa ni mzuri sana kuliko wote duniani ili apate anachokitaka. Suala la muhimu ni kwa binti kuona kama sifa hizo ni za kweli au gia ya kuingilia town.

Hata hivyo wapo wengi wanaolewa sifa za kizushi kama hizo. Kama JK naye anazikubali basi hana tofauti nao. Hivi mtu unajipima mwenyewe kwanza au unasubiri kuambiwa na watu wa nje? Na kati ya wote wanaokwambia unaweza kung'amua ni wangapi wanasema ukweli (they are sincere)? Kama siyo hivyo basi ni hatari!!
 
Kuna watu wana uelewa wa juu sana wa mambo ya utawala bora, na hata ukijifagilia na kuandaa wapambe, au kusafiri saana ili uonekane uko bize na mambo ya nchi, bado unaonekana kilaza wa kutupwa! Good asses Mo Commitee!
 
siamini..............mbona kikwete ameongoza kwa mvuto barani africa kwa hiyo amevutia tu watu lakini hajaongoza vizuri? wampe mkapa..............
 
Kwa mtazamo wangu Thabo Mbeki asingeweza kupata hii Prize kwa sababu kubwa mbili.

Moja rekodi yake kuhusu HIV/AIDS ilikuwa na doa hasa pale aliposhikilia kwamba haukuwa ugonjwa ila ni jambo la kusadikika. Mtazamo huu iliifanya serikali yake kuchelewa kutoa madawa ya kupunguza makali ya (ARVs) HIV/AID S na hivyo kupelekea watu wengi kufa. Mbeki hakuonyesha uongozi bora kwa hili.

Pili ni kwamba Mbeki alitoka madarakani katika hali ya utata. Ingawa alijihudhuru lakini kimsingi alitolewa (he was recalled) na chama chake ANC. Kwa sasa Mbeki ni “black sheep” katika ANC. Tuzo ya Mo Ibrahim ni ya kisiasa. Kamati ingempa tuzo hii ANC na serikali yake wangejisikiaje? Wangeibeza sana. Kamati imeona mbali kwa kutompa Mbeki na hivyo kuepuka controversy za kisiasa.

Sijui kwa nini Rais John Kufour hakupewa. Tusubiri tuone.
 

Sina hakika lakini nadhani kulikuwa na kelele kidogo wakati wa uchaguzi uliopita nchini Ghana na nadhani Kufour inawezekana alitaka kuingiza mchezo mchafu. Nitamuuliza jamaa yangu mmoja toka Ghana ili nijue ana maoni gani.
 
Message sent to those expecting to leave the office. Aibu kwa viongozi wa Africa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…