Waafrika hatujijui hatujitambui. Wao "wahisani" wanachangia bajeti yetu yaani pesa za matumizi yetu ya ndani wanatusaidi ni sawasawa na wewe unasaidiwa matumizi ya nyumbani kwako kwa mkeo na watoto pesa ya kula na kulipia umeme na maji pili pesa za maendeleo yaani nyumbani kwako mnanunuliwa nguo na viatu sio peke yako ni pamoja na mkeo na wanao tatu madawa ya ukimwi tatu pesa za maendeleo ya elimu pesa zinatoka hukohuko uzunguni. Wasiwasi wao zaidi baada ya mradi athari zitakazo tokea hamtaziweza kuzimudu itabidi wao watoe mapesa mengi zaidi ya kuwatatulia matatizo mlioyasababisha ninyi wenyewe. Wao ni ushauri tu wameutoa kwa sababu bi "mdau" wa "kula" na "maendeleo" yetu. Usishangae kwanza uelewe hao "wahisani" kwa nini watujadili mipango yetu?Nimekutana na taarifa kwamba bunge la Ujerumani limekaa vikao kujadili mradi wa umeme wa Stiegler George kule Tanzania, na wakapiga kura ya kuupiga chini huo mradi. Hizi taarifa nimeshindwa kuzimeza maana zimenipa hasira, utani wa jadi pembeni, yaani wazungu wakalie vikao mradi ambao haupo hata kwenye bara lao huko Ulaya, kha Afrika kweli tuna shughuli, tena ndefu.
Maskini Watanzania, haya mjiandae kupokea amri kutoka kwa bwana mkuu, maana Mjerumani bado anawamiliki hata baada ya kusemekana kaachia enzi za ukoloni.
--------------------------------------
Ujerumani: Mradi wa umeme wa Tanzania wapigiwa kura bungeni
Bunge la Ujerumani limepitisha mswada wa kuitaka serikali ya Ujerumani itafute njia mbadala ya mradi wa Tanzania wa kuzalisha nishati ya umeme kwenye bonde la Stiegler ili kulinda turathi na asili.
Vyama vilivyomo katika serikali ya mseto ya Ujerumani vimeitaka serikali itafute njia nyingine badala ya ile ya mradi wa kuzalisha nishati ya umeme kwenye bonde la Stiegler kwenye mto rufiji kusini mwa Tanzania Wabunge wa vyama vya CDU/CSU, Kijani na AFD walishiriki katika kupiga kura hiyo lakini chama cha mrengo mkali wa kulia cha AfD, hakikushiriki. Azimio la vyama vya CDU,CSU na SPD pia linatokana na mapendekezo ya kamati ya serikali ya Ujerumani ya ushirikiano wa kiuchumi.
Azimio lililopitishwa bungeni na vyama hiyvo vilivyomo katika serikali ya mseto ya Ujerumani linaitaka serikali kuu isaidie katika masuluhisho ya kukidhi mahitaji ya nishati ya Tanzania bila ya kuathiri mazingira. Katika azimio lao vyama hivyo vimesema mradi huo mkubwa wa kuzalisha nishati ya umeme utavuruga mfumo wa mto mmojawapo mkubwa barani Afrika.
Tanzania inakusudia kujenga bwawa kubwa la kuzalisha nishati ya umeme kwa kutumia nguvu ya maji kutoka kwenye mto rufiji. Sehemu hiyo ni muhimu kwa shughuli za kilimo za wakaazi. Ikiwa mradi huo utaendelea mbele bonde la Stiegler ambalo limewekwa miongoni mwa turathi za shirika la Umoja wa mataifa la UNESCO litapoteza hadhi yake na huenda likasababisha athari kubwa katika raslimali zilizopo kwenye sehemu hiyo.
Katika ombi lao kwa serikali ya Ujerumani wabunge wa vyama vya CDU,CSU na SPD wamesema sehemu hiyo ya mbuga ya wanyama ya Selous nchini Tanzania ni eneo kubwa kabisa na kongwe la hifadhi ya wanyama pori barani Afrika.
Wabunge hao wamesema mradi huo wa bwawa la nishati utahitaji sehemu kubwa sana itakayotokana na kukatwa kwa miti na hivyo kusababisha athari kubwa katika mazingira, tabia nchi na katika uchumi.
Wabunge wa chama cha upinzani cha FDP wameshauri kujengwa kinu cha nishati kutokana na gesi kwa sababu Tanzania inayo gesi ya kutosha iliyogunduliwa hivi karibuni. Chama hicho cha upinzani cha FDP kilichopinga azimio hilo kimeitaka serikali ya Ujerumani ifanye mazungumzo na serikali ya Tanzania.
Mwandishi/Zainab Aziz/Daniel Pelz/DW Berlin
Mhariri: Yusuf Saumu
Ujerumani: Mradi wa umeme wa Tanzania wapigiwa kura bungeni | DW | 18.01.2019
Umesema wabunge wa ujerumani wanaojadili kuhusu mambo yetu ndio waliotuachia katiba, sasa unabisha wakati comment yako ipo page ya kwanza? 😂😂😂😂 Huyu Mungiki vipi? Unataka kuichallenge technology? Ogopa Mungu na technology? Go back to the first page of this Thread incase kama gongo ipo higher voltage now compared to previous.Nimesema katiba ni ile ile mlioachiwa na mkoloni, ambaye ni muingereza. Sijataja mjerumani popote. Azimio la arusha ndio ilikuwa katiba mpya? Aisee, MK254 muelimishe huyu Madenge.
Kwa hiyo mto unaozalisha megawatts zaidi ya 2000 kwako ni mdogo? Ni wapi Nile umetajwa hapo? Rufiji ni kati ya mito mikubwa sana Africa.
Ambacho hujaelewa ni nini? Na unavyosikia au kusoma neno/msamiati ajabu unalielewaje?Nimekusoma japo sijakuelewa vizur,wewe na Magu nani and akili za ajabu
Sent using Jamii Forums mobile app
Mto Nike utaathirika kivipi?wakati unafundishwa geography darasani hukua makini haya ndio madhara yake...
Sent using Jamii Forums mobile app
Wewe jamaa unaongea vitu gani hapa? Umesema German Wanahofia kuharibika mto Nile, nimekupa darasa kwamba mto Rufiji hauna uhusiano na mto Nile, ukaniletea ka phrase kuhusu "moja ya mito mikubwa Africa" nikakuambia mto wenye uwezo wa kuzalisha zaidi ya megawatts 2000 sio mto mdogo, sasa unataka nini?Unapozungumzia mito mikubwa Barani Africa hiyo ndiyo mikubwa...
1) River Nile - 6,650km
2) River Congo - 4,700km
3) River Niger - 4,200km
4) River Zambezi - 2,693km
5) River Ubangi - 2,270km
6) River Kasai - 2,153km
7) River Orange - 2,92km
8) River Limpopo - 1,800km
9) River Sengal - 1,600km
Alafu tuangalie:
River Rufiji unaousemea - 600km hichi ki ka-bwaya tuu
Tatizo bindamu wa siku hizi ni wabishi sana. Mnatetea hata ujinga.
Cc: mahondaw
Wewe jamaa unaongea vitu gani hapa? Umesema German Wanahofia kuharibika mto Nile, nimekupa darasa kwamba mto Rufiji hauna uhusiano na mto Nile, ukaniletea ka phrase kuhusu "moja ya mito mikubwa Africa" nikakuambia mto wenye uwezo wa kuzalisha zaidi ya megawatts 2000 sio mto mdogo, sasa unataka nini?
We sepa bana nishakwambia Nile na Rufiji are two different planets, inatosha.
Ramani ya River NileWapi nimesema German wanahofia kuharibika River Nile.
Nimenukuu mwandishi alichosema... nikasema wanahofia kuharibu River Nile...
Soma vizuri kilichandikwa na mwandishi, elewa alafu ndiyo ujibu kulingana na bandiko...
Jioni njema...
Cc: mahondaw
Hujui kusoma? Rejea kwenye comment yenyewe hutaona popote nilipotaja mjerumani kando na kuongea kuhusu wakoloni niliposema 'hao hao'. 1977 mlifanya 'ammendments' kwenye katiba ya Tz, kwa mara ya nne. Ammendments unajua maana yake ni nini? Sio katiba mpya acha ushamba. Soma kuhusu nchi yako usije ukajiabisha tena.Umesema wabunge wa ujerumani wanaojadili kuhusu mambo yetu ndio waliotuachia katiba, sasa unabisha wakati comment yako ipo page ya kwanza? Huyu Mungiki vipi? Unataka kuichallenge technology? Ogopa Mungu na technology? Go back to the first page of this Thread incase kama gongo ipo higher voltage now compared to previous.Halafu hata hujiulizi ni kwanini tunakuambia katiba yetu ni ya 1977 na sio ya 1961 au unafikiri hatujui kwamba 1961 - 1976 tulikua tupo huru? Huwezi kutufundisha watanzania history yetu au unafikiri unahojiana na Mungiki wenzio huku?
Ramani ya River Nile View attachment 1000343
Ramani Rufiji River View attachment 1000344
Yaani sijui hata unaongea nini hapo, mmoja unaelekea kaskazini mwingine Mashariki na imetengana kwa umbali wa zaidi ya kilometers 2000.
Dah hizi shule hizi
Hujui kusoma? Rejea kwenye comment yenyewe hutaona popote nilipotaja mjerumani kando na kuongea kuhusu wakoloni niliposema 'hao hao'. 1977 mlifanya 'ammendments' kwenye katiba ya Tz, kwa mara ya nne. Ammendments unajua maana yake ni nini? Sio katiba mpya acha ushamba. Soma kuhusu nchi yako usije ukajiabisha tena.
Hujui kusoma? Rejea kwenye comment yenyewe hutaona popote nilipotaja mjerumani kando na kuongea kuhusu wakoloni niliposema 'hao hao'. 1977 mlifanya 'ammendments' kwenye katiba ya Tz, kwa mara ya nne. Ammendments unajua maana yake ni nini? Sio katiba mpya acha ushamba. Soma kuhusu nchi yako usije ukajiabisha tena.
Mto mmojawapo mkubwa barani Afrika ndio mto Nile?
Mimi nimekuuliza "Mto mmojawapo mkubwa barani Afrika" ndio mto Nile? Bado hujajibuKwa mtazamo wako wewe ni mto upi hapo mkubwa Barani Africa uliyopo au unaoanzia Tanzania?
Cc: mahondaw
Taahira wewe, katiba ya kikoloni inawezaje kutumika kwenye Taifa la kidemokrasia la kijamaa? Acha uchoko kudiscuss mambo yaliyokuzidi akili