Kama ni jipu,kwa maana ya jipu kweli,husababishwa na bakteria..
Wanaweza kuingia kwa kupenya ktk ngozi kupitia michubuko ama kupenya tu hata sehemu zisizo na michubuko..lakini pia unaweza ukawa na bakteria ndani ya damu ambapo wanaweza kusababisa jipu sehemu yoyote mwilini..
Kuhusu kujikinga ni changamoto kidogo..kama utaweza kukaa mbali na hawa bakteria ndio njia sahihi ya kujikinga..ila bahati mbaya sioni kama inawezekana..maana tunaishi na bakteria ktk mazingira yetu ya kila siku,hivyo, kujitenga nao haiwezekani..
Lakini hata hivyo,uimara wa kinga ya mwili ni factor muhimu..kutetereka kwa kinga mwilini kunaweka mwili wako ktk hatari ya kushambuliwa kirahisi, si kwa majipu tu,bali na magonjwa mengine..
Dawa ya jipu ni kulipasua linapokuwa limeiva..