Ahadi ya ajira milioni moja changa la macho?

Huyu waziri kichaa, anajua maana ya kutengeneza ajira milioni 5?
 
This is the joke, for half of his term hajafikisha what was expected from him the the last half atengeneze 1000% ya kile kilichamshinda kwa half ya kwanza, hivi wabunge wetu wajua kufanyia statistics analysisy especially time analysisy maana inawezekana kunawalipiga makofi.
 
Good signs of a weak leader are everyday's promises while the former ones could not even be implemented.
Fake promises are pitfalls of uncharismatic leaders.Not knowing their obligations and duties to their nation.
 
Huyu waziri kichaa, anajua maana ya kutengeneza ajira milioni 5?

Mkuu Mtanzania usimshangae sana huyu Prof. kakulia humu humu kwenye 'mikakati'. very intresting kila siku utasikia tunaandaa au tumeandaa 'mkakati' loh hakuna utekelezaji!
 
And we keep on wondering why Tanzania is here today????????? Kama viongozi ndio hawa........... Tena professa.... Tusubiri tu 2010 kutakuwa na mbwembwe kibao!!!
 

Huyu waziri ni msomi wa daraja la juu kabisa. Na haya ndiyo mawazo yake. Kuna tumaini lolote la uongozi mzuri nchi hii?
 
Serikali imewahakikishia Watanzania kuwa ajira milioni moja zilizoahidiwa na Rais Jakaya Kikwete wakati wa kampeni mwaka juzi, zitapatikana kabla ya mwaka 2010. Akitoa ufafanuzi wa hoja za wabunge waliochangia hotuba yake, Waziri wa Kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana, Profesa Juma Kapuya alisema jana bungeni kuwa ajira hizo zitapatikana kwa kasi iliyopangwa.

Alisema ajira hizo zinapatikana kupitia Mpango wa Kukuza Uchumi na Kupunguza Umasikini (Mkukuta) ambao unawashirikisha wadau mbalimbali katika kuainisha vyanzo na sekta mbalimbali ambazo zitaleta ajira hizo. Alisema wadau mbalimbali zikiwamo wizara, taasisi za umma, zinakusanya taarifa mbalimbali kupitia Idara ya Takwimu ya Taifa (TBS) kuona maeneo ambayo yatakuwa na ajira nyingi.

Alisema mpango huo unashirikisha pia Shirika la Kazi Duniani (ILO) na Shirika la Maendeleo ya Umoja wa Mataifa (UNDP) ambazo kwa pamoja zimeanzisha programu wa kuainisha ajira ulioanza mwaka jana ili kuhakikisha ajira hizo zinapatikana. Alisema mpango huo unaonyesha kuwa hadi kufikia mwaka 2010, sekta mbalimbali zitakuwa zimeanzisha ajira zaidi ya milioni tano na hivyo kusaidia kupunguza umasikini wa kipato miongoni mwa watu.

Ufafanuzi wa Waziri ulitokana na hofu ya wabunge kuhusu kupatikana kwa ajira 437,205 tu, ambazo ni sawa na asilimia 43.7 ya lengo la kuanzisha ajira milioni moja tangu ahadi hiyo itolewe miaka miwili iliyopita. Aidha, Profesa Kapuya alisema utafiti unaofanywa na wasomi wa Chuo Kikuu Dar es Salaam (UDSM) kuhusu uwezo wa kulipa mishahara ya kima cha chini na athari za viwango vipya vya mishahara katika sekta binafsi, unatarajiwa kukamilishwa mwezi ujao.

Alisema utafiti huo utaangalia kiundani mfumo bora wa kulipa kima cha chini ambacho kitakuwa na tija na kuamsha ari kwa ajili ya kufanya kazi katika sekta hiyo. Katika hatua nyingine, Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa (UN), Dk. Asha-Rose Migiro, leo atakuwa na ziara ya siku moja katika Bunge.

Kutokana na taarifa hiyo iliyotolewa na waziri Kapuya bila ya shaka yeyote ajira zilizoahidiwa na Kikwete zitapatikana wana JF tujenge utamaduni wa kueleza mazuri yanayofanywa na serikali na siyo mabaya tu shiringi ina pande mbili.
 
Hivi hizo ajira Milioni Moja zina uwiano wowote na Watanzania ambao wanaingia katika soko la ajira kila mwaka ama ni Milioni moja namba tu ambayo ilitajwa kwa kuwa ni rahisi kutamkwa?
 
mmh tukisema viongozi hatuna watu mnabisha angalieni sasa.Wachukue pesa zote kutoka kwa mafisadi kisha wawekeze vijijini huko ambako kuna watu wanajiali wenyewe bila kutegemea mgongo wa serikali.
 
Kuna swali jana liliulizwa katika Power Breakfast ya Clouds Fm kwamba je hizo ajira 1,000,000 zinahusisha na ajira ya Vijana ambao wanaosha magari katika bara bara mbalimbali kuu hapa nchini!!!?

Hivi watakuwa katika Sekta isiyo rasmi eeh?
 
NITALETA AJIRA MILIONI MOJA...


ANYWAY SIJAWEZA HATA kuleta hata ajira laki moja/.....

lakini....

MAISHA BORA KWA KILA MTANZANIA YANAWEZEKANA..

TANZANIA YENYE NEEMA INAWEZEKANA...

SORRY GUYS - VUMILIENI MAUMIVU...

NIMEKUMBUKA...

KULETA AJIRA MILIONI TANO KABLA YA MWAKA 2010 INAWEZEKANA...

TEH !! TEH !! WADANGANYANYIKA BWANA!!!!

WENU ....

JANGALA MICHOSHO KIWETE..

CHAGUO la " mungu " AKA "JOHN WALKER
[/SIZE]
[/I]
]

....
 
Ajira zenyewe ni za Polisi,Wanajeshi,Askari magereza ili wahakikishe usalama wa mafisadi na za walimu wale wa kusoma ualimu wiki 6
 

...Hivi huyu JK anashauriwa kabla hajatoa hizi statement zake au inakuwaje?? Kwa kweli tumegeuzwa misukule kabisa....
 
haya yatamalizwa kwa style ile ilyotokea kenya baada ya uchaguzi....amka wewe uliyelala
 
Tanzania ni Taifa lenye rasilimali nyingi,watu wengi ,imekosa siasa nzuri na ina viongozi wabovu.
 
...statement kama hizi ni sababu tosha ya kuwapiga chini CCM 2010 lakini cha ajabu itakuwa landslide kama kawa,sasa hapo kichaa ni nani?
 
Katika hotuba yake ya kuuaga mwaka 2009 na kuukaribisha 2010 Rais Kikwete alisema hivi:


Wakati huo huu tumeambiwa kuwa serikali ya JK imefanikiwa kuvuka lengo lake la ajira milioni moja na kuwa wametengeneza ajira mpya zaidi ya milioni moja ndani ya miaka minne.

Naomba wachumi mnisaidie ni katika mazingira gani nchi inayokabiliwa na athari za recession inatengeneza ajira zaidi ya asilimia 100 ya makadirio yake na wakati huo huo kudai kuwa ina hali mbaya ya kiuchumi?
 
i am not
an economist,
but i know it is possible.

mm mwanakijiji......uchumi wa tanzania
tatizo kubwa sana ni kukosekana kwa takwimu sahihi....

rejea mkurabita.....
kwa hiyo uchumi huu una uwezo wa kutengeneza
hata ajira milioni 5 kwa miaka minne.

kwa hiyo kwa jk kusema ametengeneza ajira milioni moja.
its not a big deal kabisa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…