Ahmed Ally awaomba radhi mashabiki wa Simba, awasihi kurejea nyumbani kwa utulivu baada ya mechi kuahirishwa

Ahmed Ally awaomba radhi mashabiki wa Simba, awasihi kurejea nyumbani kwa utulivu baada ya mechi kuahirishwa

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Meneja wa Habari wa Simba SC, Ahmed Ally, amewasilisha ujumbe wa pole kwa mashabiki wa klabu hiyo kufuatia kuahirishwa kwa mechi yao leo.

IMG_3438.jpeg
Kupitia taarifa yake, Ahmed Ally ameomba radhi kwa mashabiki wote wa Simba, hususan wale waliotoka mikoa mbalimbali kwa ajili ya kushuhudia mchezo huo. Ameeleza kuwa uamuzi uliofanywa na viongozi wa klabu ni kwa maslahi ya timu na mpira wa miguu kwa ujumla, hivyo mashabiki wanapaswa kuupokea kwa utulivu.

Soma: Bodi ya Ligi kuu yaahirisha Mechi ya Derby kati ya Yanga dhidi ya Simba

Aidha, amewasihi mashabiki waliokuwa tayari wamefika uwanjani kurejea nyumbani kwa utulivu ili kuwahi futari, huku akiwatakia safari njema wale wanaorejea mikoani.

Ahmed Ally amesisitiza kuwa licha ya kuahirishwa kwa mechi hiyo, mashabiki wa Simba wasikate tamaa kwani, kwa mujibu wa ujumbe wake, "haki imeshinda."

IMG_3437.jpeg
 
Waoga wakubwa mikia katikati ya materkow [emoji2959][emoji2959][emoji2959]
Ujinga wa aina yako ndio mtaji mkubwa wa chama tawala nchini. Unatukana matusi ya nguoni kisa ujinga wa timu yako kutuma wahuni kuzuia timu kuingia uwanjani..Sasa hujioni ulivyo na low level thinking capacity mana matusi ni dalili ya mtu aliye na fikra hafifu na zaidi mhuni wa kitaa.
 
Ujinga wa aina yako ndio mtaji mkubwa wa chama tawala nchini. Unatukana matusi ya nguoni kisa ujinga wa timu yako kutuma wahuni kuzuia timu kuingia uwanjani..Sasa hujioni ulivyo na low level thinking capacity mana matusi ni dalili ya mtu aliye na fikra hafifu na zaidi mhuni wa kitaa.
Binti mbona hata haueleweki unachokiandika kwahiyo tatizo ni Yanga au meneja wa uwanja kutokuwa na taarifa ya ujio wa kundu la msimbazi?
 
Uungwana ni vitendo...
Nitaendelea kusema kuna watu wana roho mbaya na sifa kubwa ya Watz wengi tuliojificha nyuma ya upole na amani.

Naanza na Meneja wa uwanja na jumiya nzima ya michezo.Hao ni watu wasiojali utu wa watu tuliotoka mbali kwa kupata burudani.
Wakalegeza kende zao na egos zao pasipo sababu za maana.

Wanahisi hela zitatoka kwenye ma**ko yao na ni rahisi sana.

UHUNI huo ukemewe kwenye hii Nchi.
Bodi hii ivunjwe wapewe watu wenye akili.
 
Back
Top Bottom