warumi
R I P
- May 6, 2013
- 16,218
- 18,440
Binafsi uwa ni mpenzi wa hiki kituo cha radio (clouds FM), na uwa nafuatilia sana vipindi vyake kuanzia power breakfast hadi ala za roho. Hivi karibuni nimekuwa nikisikia sijui niite tangazo ama nini, ni program mpya nadhani walioianzisha clouds inaitwa sambaza amani na upendo, uwa nasikia Mara nyingi linah au linex wakiimba , sometimes wanaimba hadi kiluga, binafsi uwa nafurahi sana nikisikia huu wimbo japokuwa hauimbi hadi mwisho ila natamani sana niwe nausikia Mara kwa Mara, ukiachilia mbali message nzuri ya huu wimbo uwa nazimia sana sauti ya lina na Linex kwenye hili Tangazo, napenda sana kusikia sauti Zao , na ni kweli kabisa zinaamasisha amani na upendo, wameimba kwenye hali ya utulivu na kumaanisha wanachokiimba, big up for that,wanaimba nadhani "Hello hello Tanzania, hello hello Mapenzi ya kweli", it sounds Good , swali je? clouds wenyewe wamemaanisha hicho walichowatuma kuimba lina na linex au? Ni kweli wana nia ya dhati ya kusambaza amani na upendo?