Airtel matapeli zile 5% za timiza akiba hamtoi kweli

Airtel matapeli zile 5% za timiza akiba hamtoi kweli

Mwananchi hewa

JF-Expert Member
Joined
Dec 27, 2016
Posts
226
Reaction score
274
Utapeli wao ni hivi
Mimi niliweka kiasi cha shilingi laki mbili kwa mwezi mmoja katika timiza akiba yao, na wao walisema mteja atakayeweka pesa ndani ya mwezi mmoja bila kutoa basi atapata asilimia tano ya kiasi cha pesa alichoweka ndani ya mwezi huo lakini katika laki mbili niliyoweka nimepewa tsh 73 tu japo sikuweka hela kwa mkupuo.
Kwanini naamini wamenitapeli?
Baada ya kupata kiasi hicho kidogo cha fedha nisichotegemea kwa maana mimi nilitegemea kupata kama elfu kumi hivi, nilienda katika akaunti zao za mitandao ya kijamii sikujibiwa tena swali langu linarukwa wanajibiwa wengine.
Ila kali zaidi ya kuonesha ni matapeli nimepiga simu tofauti tatu kwa siku tofauti huduma kwa wateja kila simu moja ina ufafanuzi tofauti kuhusu mnyambuliko wa kuipata asilimia tano
Ya kwanza
Hii nilijibiwa kuwa hiyo asilimia tano unaipata kidogo kidogo kutokana na ulivyoweka hela katika akaunti yako. Yaani kwa mfano umeweka pesa tarehe 3,5,7,12,27, basi mwezi ujao zikifika hizo tarehe unalipwa hela yako kutokana na tarehe ulizoweka. Mimi nikakubali nikawa nasubiri hela yangu ila ni tofauti mpaka leo kiasi ni kile kile cha mwanzo hakuna kilichozidi, ikabidi nipige simu tena

Ya pili
Hii nikauliza 5% mteja anaipata vipi na nikawaambia kiasi changu nilichoweka, huyu akanijibu hivi
Kiasi nilichoweka ndani ya mwezi mzima kinagawanywa mara 12 halafu hiko kiasi kilichopatikana asilimia tano yake ndio nalipwa, hapa ndipo huu utapeli nikatulia siku kadhaa leo nikapiga tena.

Ya tatu
Simu niliyopiga leo nikajibiwa kuwa kiasi nilichoweka kwa mara ya kwanza 5% yake ndiyo nitakayopewa.
Sasa hapo nikaamini ni utapeli maana simu zote tatu ufafanuzi ni tofauti.
Siyo kwamba naumia ila wamevunja makubaliano waliyosema.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huyo aliyekupa jibu la 2 ndio yuko sawa,kwa msingi kwamba hio 5% ni interest ya mwaka zima(annual interest).

So ilikupata interest unayostahili kupata kwa mwezi 1 lazima agawe kwa miezi 12.Hesabu inatakiwa iwe:

200,000×5%/12=Tsh.833

Sasa imekuwaje ukapewa sh.73 badala ya sh.833 hapo ndipo sijaelewa mkuu.
 
Huyo aliyekupa jibu la 2 ndio yuko sawa,kwa msingi kwamba hio 5% ni interest ya mwaka zima(annual interest).

So ilikupata interest unayostahili kupata kwa mwezi 1 lazima agawe kwa miezi 12.Hesabu inatakiwa iwe:

200,000×5%/12=Tsh.833

Sasa imekuwaje ukapewa sh.73 badala ya sh.833 hapo ndipo sijaelewa mkuu.
Na hapo ndipo nahisi huo ni utapeli

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ulisoma masharti yao kabla ya kuweka pesa? Hiyo asilimia tano ni ya mwaka pesa ukiweka ikakaa mwaka mzima sio ya mwezi
 
Huyo aliyekupa jibu la 2 ndio yuko sawa,kwa msingi kwamba hio 5% ni interest ya mwaka zima(annual interest).

So ilikupata interest unayostahili kupata kwa mwezi 1 lazima agawe kwa miezi 12.Hesabu inatakiwa iwe:

200,000×5%/12=Tsh.833

Sasa imekuwaje ukapewa sh.73 badala ya sh.833 hapo ndipo sijaelewa mkuu.
Sababu ya kupata 73 badala ya 833 ni kuwa pesa aliziweka tarehe tofauti tofauti kuna hela zingine Bado hazikaa kwenye akaunti mwezi hazijafikisha mwezi.Zilizofikisha mwezi ndio hizo kapewa 73.Ni hela nyingi kwani angeiokota barabarani hiyo 73?
 
Sababu ya kupata 73 badala ya 833 ni kuwa pesa aliziweka tarehe tofauti tofauti kuna hela zingine Bado hazikaa kwenye akaunti mwezi hazijafikisha mwezi.Zilizofikisha mwezi ndio hizo kapewa 73.Ni hela nyingi kwani angeiokota barabarani hiyo 73?
Sawa!
 
Sababu ya kupata 73 badala ya 833 ni kuwa pesa aliziweka tarehe tofauti tofauti kuna hela zingine Bado hazikaa kwenye akaunti mwezi hazijafikisha mwezi.Zilizofikisha mwezi ndio hizo kapewa 73.Ni hela nyingi kwani angeiokota barabarani hiyo 73?
Angeiokotea kwny kampeni za CCM.
 
Unaijua 5% kwa mwezi mkuu au unaropoka tu? Hakuna kampuni yenye uwezo wakulipa 5% dunani
 
Back
Top Bottom