#COVID19 Aishitaki hospitali kwa kumbambikizia Corona

#COVID19 Aishitaki hospitali kwa kumbambikizia Corona

Webabu

JF-Expert Member
Joined
Apr 29, 2010
Posts
8,870
Reaction score
14,258
Nipo Mascut nchini Oman. Nimeingia kwenye chumba cha mahakama asubuhi hii kusikiliza kesi ya mmoja wa wanafamilia. Kabla kesi yetu kutajwa nikasikia kesi mchanganyiko.

Iliyonivutia ni hii ya jamaa aliyeamua kupambana na hospitali ya serikali na daktari waliomtangazia kuambukizwa corona na kumpa dawa na kumuweka karantini ya wiki 2 na ilhali hana shida hiyo.

Tulipotoka nje ya mahakama ndipo akatusimulia mkasa wake. Anasema alijihisi na homa na uchofu ulioambatana na kutoka makamasi, akaamua kwenda hospitali.

Alipofika haraka akachukuliwa vipimo na majibu yakaja ana corona. Akapewa dawa za kutumia na masharit akajifungie ndani bila kuonana na watu kwa wiki mbili zinazofuatia.

Kwa vile hakuhisi kitu kigeni sana mbali na mafua anayopata baadhi ya siku hakuridhika na matokeo yale na akaamua kwenda kuchukua vipimo kwenye hospitali nyengine binafsi zilizoruhusiwa kupima corona.

Matokeo kwenye hospitali tatu yakaonesha hana corona na hata mafua nayo si makali sana. Ndipo alipoamua kufungua kesi.
 
Mkuu ni kweli kwamba waarabu wa huko siyo binadamu kabisa kwa watu wa nchi nyingine hasa watu kutoka Afrika?Nipe experience yako tafadhali!
 
Hunijibu hapa,utanijibu wapi mkuu?
Ingia kwenye nyuzi nyengine nyingi hapa hapa zenye mada kama hiyo.Au anzisha wa kwako uuite Waarabu si watu nitakuja kukujibu huko tuone kama utakuwa na hoja za maana.
Vyenginevyo subiri nikija safari hii nikutolee viza tuje pamoja ili uone kwa macho yako na uje uwasimulie ndugu na jamaa iwapo waarabu ni watu au ni wanyama.
 
Ingia kwenye nyuzi nyengine nyingi hapa hapa zenye mada kama hiyo.Au anzisha wa kwako uuite Waarabu si watu nitakuja kukujibu huko tuone kama utakuwa na hoja za maana.
Vyenginevyo subiri nikija safari hii nikutolee viza tuje pamoja ili uone kwa macho yako na uje uwasimulie ndugu na jamaa iwapo waarabu ni watu au ni wanyama.
[emoji706][emoji706][emoji706]
 
Mkuu ni kweli kwamba waarabu wa huko siyo binadamu kabisa kwa watu wa nchi nyingine hasa watu kutoka Afrika?Nipe experience yako tafadhali!
Ukisikia fitna na majungu ndio hayo
 
Back
Top Bottom