Ajichoma moto akipinga 'rushwa na hali ngumu ya maisha'

Ajichoma moto akipinga 'rushwa na hali ngumu ya maisha'

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Joined
Feb 24, 2012
Posts
5,108
Reaction score
10,191
Mwanaume mmoja raia wa Misri amejichoma moto, kisha kuokolewa na polisi na wapita njia katika uwanja wa Tahrir, jijini Cairo, mtu huyo alifanya hivyo kupinga "rushwa na hali mbaya ya maisha".

Mtu huyo alifukuzwa kazi katika benki kwa kuanika vitendo vya rushwa vilivyowahusisha maafisa wa serikali, kwa mujibu wa makala ya Middle East Eye.

Katika matangazo ya moja kwa moja ya Facebook, mwanaume huyo alisema maisha yake yameharibiwa na kuwa hana uwezo wa kupata kipato
Kisha alijimwagia kimiminika chenye uwezo wa kushika moto na kuwaambia maafisa wa usalama uwanja wa Tahrir kuwa wasimkaribie.
Alisema nchi imekuwa ikiharibiwa vibaya na kundi dogo la "wezi".

Mtu huyo alijiwasha moto na kisha alipambana na maafisa wa usalama ambao waliuzima moto huo.
 
Kijana mmoja huko Tunis alijipiga kiberiti 2010 kwa kadhia inayofanana na hiyo, yaliibuka Maandamo hadi mtawala mkongwe wa Taifa hilo akakimbia.
 
Wengine ni ma keyboard warriors tu.........practice what you preach........
 
To be honest....
Mimi hata kama nchi imefukia hali mbaya kwa kiasigani, nikisha iwazia familia yangu tu..... Siwezi kujiwasha moto aiseeee
 
Msongo wa maisha mmbaya sn, yeye aliona bila kazi hawezi tena kuishi, kila anayefukuzwa kazi akichukua fikra hizo sijui itakuaje
To be honest....
Mimi hata kama nchi imefukia hali mbaya kwa kiasigani, nikisha iwazia familia yangu tu..... Siwezi kujiwasha moto aiseeee
 
Back
Top Bottom